Saturday, September 11, 2010

Dk. Slaa akemea majini ya Sheikh Yahya Hussein

Dk. Willibrod Slaa amemkemea mnajimu Sheikh Yahya Hussein (pichani) aliyeahidi kumpa Rais Jakaya Kikwete 'ulinzi wa majini,' ili kukabiliana na nguvu za giza zinazomwandama na kumwangusha majukwaani. Akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Katoro, jimbo la Busanda, Mwanza, Dk. Slaa alisema "nchi haiwezi kuongozwa na uchawi. Haiongozwi na imani za watu, kila mtu ana imani yake, lakini tusifike mahali tukaongoza nchi kwa uchawi."

Alimtaka Rais Jakaya Kikwete kumkemea Sheikh Yahya kwa kauli hiyo iliyotolewa juzi Dar es Salaam, la sivyo wananchi wataamini mnajimu huyo anatumiwa na CCM kuleta hofu katika jamii. Aliwakumbusha wananchi kuwa mwanzoni mwa mwaka huu, Sheikh Yahya alisema mtu yeyote atakayegombea urais na Kikwete, atakufa. Dk. Slaa alisema: "Sisi wengine ni majabali, hatuogopi."

0 comments:

Post a Comment