Sunday, April 10, 2011

Kongamano la CHADEMA Vyuo Vikuu Dodom


MHE ZITTO Na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Central ya mjini Dodoma

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Central ya mjini Dodoma walipotembea Bunge.



Thursday, March 24, 2011

Zitto Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini Kupitia Chadema

Mwenyekiti wa kamati ya mashirika ya umma na hesabu za serikali (POAC) Zitto Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini Kupitia Chadema akitazama madini ya mchuchuma wilayani Ludewa ,madini hayo yapo nje nje kama yanavyoonekana hapa .

Mwenyekiti wa kamati ya bunge hesabu za mashirika ya umma Mhe.Zitto kabwe

Mwenyekiti wa kamati ya bunge hesabu za mashirika ya umma Mhe.Zitto kabwe akiwatuliza wafanyakazi wa mgodi wa Kiwira ,wasihujumu mgodi huo pamoja na serikali kuchelewa kuwalipa mishahara yao

Mbunge wa Arusha(Chadema)Godbless Lema Azitungia Wimbo Vurugu za Arusha

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alipoonyesha CD iliyobeba wimbo alioutunga kuelezea vurugu na vifo vya Arusha,kulia ni Katibu wa Kanda ya Kinondoni Chadema Henry Kilowo. Picha na Mdau Venance Nestory.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC) Mh. Zitto Kabwe (Mb)

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC) Mh. Zitto Kabwe (Mb) (katikati) akitoa tathmini ya ziara ya kamati hiyo kukagua ufanisi wa miradi ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) ya Mchuchuma, Liganga na Ngaka South na Shirika la NSSF kuhusu mradi wa Kiwira. Kulia ni Katibu wa Kamati Bw. Erick Maseke na Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Mh. Deo Filikunjombe.

Zitto Kabwe Atoa Mkono wa Pole kwa Ndugu zetu wa Japan

Mbunge wa Kigoma Kaskazini -Chadema Mheshimiwa Zitto Kabwe akitia saini kitabu cha Maombolezo kwenye Ubalozi wa Japan Nchini Tanzania
Mbunge wa Kigoma Kaskazini -Chadema Mheshimiwa Zitto Kabwe akitoa pole kwa Balozi wa Japan nchini-Balozi Hiroshi Nakagawa