Sunday, September 5, 2010

Slaa ataka Watanzania wapate 'Slaa' mwingine Bungeni

Mgombea urais kupitia Chadema Dk. Willibrod Slaa amewataka wananchi wa Singida Mashariki kumchagua Tundu Lissu kuwa mbunge wao, ili kuziba pengo lake (Slaa) ambaye baadhi ya wananchi wamekuwa wakimlilia kwamba angebaki Bungeni kuwatetea. Dk Slaa alisema Tundu ni kiongozi jasiri, ambaye iwapo atakuwa katika Bunge na Halmashauri atatetea maslahi ya wananchi wote, kama alivyofanya Dk. Slaa kwa miaka 15 mfululizo. Dk. Slaa alisema hayo wakati akimnadi Lissu katika mikutano ya hadhara jimboni mwake, kwenye maeneo ya Makiungu, Dung'unyi, Ntuntu na Mang'onyi mkoani Singida.

0 comments:

Post a Comment