Wednesday, August 18, 2010

wadau wa sekta ya habari wakutana kujadili uchaguzi mkuu 2010 leo

Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO akiongea na wadau wa sekta habari leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa kujadili mwongozo wa maadili ya vyombo vya habari katika kutoa taarifa za uchaguzi mkuu 2010. Pamoja na mambo mengine amewataka kuheshimu Uhuru wa vyombo vya habari uliopo nchini kwa kuepuka kuandika habari za uchochezi na matumizi ya lugha zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani.Bw. Deogratias Mushi mdau katika sekta ya habari akiongoza majadiliano ya mkutano wa wadau wa sekta habari kujadili mwongozo wa maadili ya vyombo vya habari katika kutoa taarifa za uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini mwezi Octoba, 2010 leo jijini Dar es salaam.Wadau wa sekta ya habari nchini wakipiga kura kupitisha baadhi ya maamuzi yatakayozingatiwa na vyombo vya habari kama mwongozo wa maadili kwa vyombo vya habari katika kutoa taarifa za uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini mwezi Octoba 2010.Baadhi ya wadau wa sekta ya habari wakichangia masuala mbalimbali kuhusu Mwongozo wa maadili ya vyombo vya habari katika kutoa habari za uchaguzi mkuu wa 2010 leo jijini Dar es salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamekubaliana kutoa habari zisizopendelea upande wowote ,zenye ukweli na zenye kujali uchunguzi wa hoja.

(Picha na Aron Msigwa -Globu ya Jamii)

0 comments:

Post a Comment