Thursday, August 12, 2010

Salamu Toka Kwa Dr Slaa - Kwa FOS

Leo nilienda kumjulia hali Dr. Slaa pale MOI na nimemkuta anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa operation jana. Nimemwambia mimi ni mmoja wa marafiki zake tunamuombea apone haraka. Alifurahi sana kumpokea mmoja wa rafiki zake ambao alikuwa hajakutana nao kabla. Akaniagiza nitoe salaam kwa marafiki zake wote katika forum yetu, lakini naona ile blog haifunguki tena. Naomba uwasilishe salaam hizi kwa marafiki wote.

Harry J. Mwansembo

1 comments:

Reggy's said...

Mungu amponye haraka ili aweze kufanya kazi tunayotaka afanye.

Post a Comment