Wednesday, August 11, 2010

DR. SLAA ALAZWA KWA MATIBABU

Dr Slaa akiwa wodini

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk. Willibrod Slaa, amelazwa katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili. Blogu hii ilizungumza na Dk Slaa hospitalini hapo, akasema alilazwa jana Jumatatu kwa ajili ya matibabu ya mkono wake uliovunjika mfupa wa juu ya kiwiko wiki moja iliyopita. Kwa maelezo yake, alishauriwa na daktari aliyemfunga 'mhogo' (POP) katika hospitali ya Bugando, Mwanza, kwamba alipaswa kurejea hospitali kwa uchunguzi mwanzoni mwa wiki hii. Alikwenda Muhimbili mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea urais kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, jana Jumanne.

Habari za kulazwa kwa Dk. Slaa zilipowafikia mashushushu wa CCM na marafiki wa mafisadi, zilipokelewa kwa hisia za kishabiki, hata baadhi yao wakadiriki kueneza uvumi kwamba Dk. Slaa yu mahututi. Mwenyewe alipozungumza na blogu hii kwa simu alisema: "Siko mahututi. Ni jambo la kawaida, nililazimika kurudi hospitali kwa ajili ya kufanyiwa matibabu ya ziada, ikiwa ni pamoja na kufungua POP."

Akiwa Muhimbili, Dk Slaa anaweza ama kufungwa POP jingine au kufanyiwa pia upasuaji mdogo ili kuwezesha mkono kupona haraka. Alisisitiza kwamba kulazwa kwake hakuathiri mchakato wa maandalizi ya kampeni zake; na kwamba alikuwa akifanya kazi kwenye kompyuta yake kama anavyoonekana kwenye picha hii, iliyopigwa na Joseph Senga leo Jumanne jioni katika wodi binafsi, F, hospitalini Muhimbili.

HABARI NA ANSBERT NGURUMO/BLOG

0 comments:

Post a Comment