Thursday, October 21, 2010

ZITTO KABWE AUZA NGUO ZAKE MKUTANONI KUMCHANGIA MGOMBEA WA UBUNGE SUMBAWANGA MJINI

Zitto kabwe akionyesha fedha zilizochangwa katika mkutano wake wa kampeni leo ,kushoto ni mgombea ubunge jimbo la Sumbawanga mjini aliyechangiwa na kulia na makamu mwenyekiti wa Chadema Taifa
Baadhi ya fedha zilizochangishwa na Zitto kwa ajili ya kusaidia mgombea ubunge wa Sumbawanga mjini kuwalipa mawakala wake siku ya Octoba 31


Hapa Kabwe akipata picha ya pamoja na wapenzi wa Chadema waliojitokeza kuchangia

Askari polisi ,magereza na mgambo wakilinda mkutano wa kampeni za Chadema ambao alikuwa akihutubia naibu katibu kuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema)Taifa Bw Zitto Kabwe viwanja vya Sumbawanga mjiniNaibu katibu kuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema)Taifa Bw Zitto Kabwe (kulia) akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Sumbawanga mjini mkoani Rukwa Mwalimu Norbart Yamsebo wakati wa kampeni za Chadema mjini Sumbawanga


Naibu katibu kuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema)Taifa Bw Zitto Kabwe akiendesha harambee ya kumchangia fedha za kuweka mawakala wa mgombea ubunge wa jimbo la Sumbawanga mjini Mwalimu Norbart Yamsebo (chadema) ,katiba harambee hiyo zaidi ya shilingi 800,000 zilipatikana huku yeye Kabwe akiuza kwa manadi kombati yake iliyonunuliwa kwa shilingi 200,000


Naibu katibu kuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema)Taifa Bw Zitto Kabwe( kulia) akihesema fedha zilizochangwa katika viwanja vya mkutano wa kapeni vya Sumbawanga mjini wakati wa kampeni zake


Fedha zilizochangwa na wananchi wa jimbo la Sumbawanga mjini kila mmoja alitoa kulingana na uwezo wake ili kusaidia mgombea wa Chadema ashinde na apata fedha za kuweka mawakala


mapokezi ya naibu katibu mkuu wa Chadema Taifa Bw Zitto Kabwe katika jimbo la Sumbawanga mjini leo palikuwa hapatoshi,

KAMPENI za naibu katika mkuu wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Zitto kabwe katika jimbo la Sumbawanga mjini zaendelea kukiweka pabaya chama cha mapinduzi zaidi ya 2000 leo kufanya maandamano ya furaha kwa kumsindikiza mgombea ubunge wa jimbo hilo Mwalimu Norbert Yasembo .
(CCM) baada ya wananachi

Pia wananchi hao jana walitumia mkutano wa kampeni za Chadema kumchangia mgombea huyo fedha za kuwalipa mawakala wake kiasi cha shilingi zaidi ya 800,000 katika harambee iliyoendeshwa na Kabwe ambaye pia alijitolea kuchangia kampeni hizo kwa kuuza kombati yake kiasi cha shilingi 200,000 .

Akihutubia katika mwendelezo wa mikutano ya kampeni ya Chadema mkoani Rukwa katika viwanja vya Rukwa High School jana mbali ya kukataa kata kata dua za wananchi hao kumwombea kuwa spika wa bunge lijalo la muungano wa Tanzania ,Kabwe alisema kuwa lazima CCM itambue kuwa hatua ya wannachi hao kuchangia kiasi hicho cha fedha ni misho mbaya kwake na kuwa isitegemee kushinda kwa miujizi jimbo hilo.

“Nasema napongeza sana kwa mapokezi haya makubwa ambayo mmeonyesha kwangu na huu ni ushadidi kuwa mgombea wa CCM katika jimbo hilo Aesha Hillary si chaguo halisi la wana jimbo la Sumbawanga mjini hivyo si vizuri kwa wachache waliobaki kupoteza kura zao kwa kumpa mgombea ambaye hatakiwi “

Alisema kuwa mkoa wa Rukwa , Kigoma na Tabora ni mikoa ambayo makao makuu yake bado hadi sasa hajaunganisha na lami hali ambayo inahitaji kuwapata wabunge makini watakaoweza kutetea wananchi wa mikoa hiyo kuwa ni sehemu ya wananchi wa mikoa ya Tanzania ambayo kwa sasa imeunganishwa kwa lami .

“Ndugu zangu Tanzania ni moja na mikoa yote ya Tanzania wananchi wake ni walipaji wakubwa wa kodi hivyo kitendo cha serikali ya CCM kuendelea kuwabagua wananchi wa mikoa hiyo ni sawa na kuwaona kuwa hawafai kupewa huduma hiyo na dawa pekee ni wananchi wa mikoa hiyo kuungana kuwanyima kura wagombea ubunge wa CCM na kuwapa wale wa Chadema ambao kupitia Rais mpya wa awamu ya tano kwa Tanzania Dk Willibrod Slaa wananchi wa mikoa hiyo wanapewa haki yao ya lami”

Kabwe alisema kuwa wananchi wa Tabora ,Kigoma na Rukwa wasipo kubali kuunganisha nguvu zao katika kuchagua wabunge wa Chadema bado CCM itaendelea kuwanfaya kuonekana kuwa wanyonge na kuwa katika mkoa wa Kigoma kwa bunge lililopita mbunge wa upinzani alikuwa ni mmoja pekee huku katika mkoa wa Rukwa pia kulikuwa na mbunge moja hivyo ni vizuri Octoba 31 kuongeza idadi zaidi ili wabunge wa mikoa ya kaskazin kuwe na idadi kubwa ya wabunge.

Hata hivyo alisema kuwa kwa upande wake hana tatizo la jimboni kwake kwani tayari ameshinda na anasubiri kuapishwa na Rais wake Dk Slaa.

Katika hatua nyingine Kabwe ameshangawa na hatua ya ulinzi mkali aliowekewa katika jimbo hilo la Sumbawanga mjini ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha askari polisi ,askari magereza pamoja na mgambo kufika kulinda mkutano jambo ambalo hajapata kuona askari magereza wakifika katika mikutano ya kampeni kama jimbo hilo la Sumbawanga mjini na kuwa yawezekana katika mkutano wake huo wafungwa pia wamefunguliwa ili kuja kusikiliza sera za Chadema.

Katika mkutano huo wa Zitto uliomalizaka kabla ya muda wa kampeni kuisha wananchi walifanya maandamano makubwa huku biashara zao zikisimama kwa muda kwa ajili ya kusukuma gari la Zitto Kabwe pamoja na ile ya mgombea ubunge wa Chadema huku wakiimba kuwa wanataka mbunge Msomi wa Chadema sio CCM .

Hatua hiyo ilionyesha kuwapa wakati mgumu askari polisi magereza na wale wa jeshi la polisi nchini kuwatuliza wananchi hao na kuwaomba viongozi wa Chadema kuwatuliza na kuwatawanya wananchi hao zaidi ya 2000 kabla ya mgombea ubunge wa Chadema kuamua kuwatoroka viongozi wenzake ofisini ili waandamanaji hao kutawanyika

0 comments:

Post a Comment