Saturday, October 30, 2010

Kipindi maalumu kwenye ITV na Dk Slaa (Saa 9.30 hadi Saa 10.30)

Kutakuwa na kipindi maalumu cha Dk Slaa katika ITV leo siku ya mwisho wa kampeni kuanzia saa 9.30 hadi saa 10.30 jioni. Katika kipindi hiki Dk Slaa atafanya majumuisho ya kampeni zake na kuwaomba tena watanzania wamchague hiyo kesho.

Awali kipindi hiki kilikuwa kirushwe kuanzia saa 11 hadi saa 12, lakini katika hali ya kushangaza, ghafla ITV wameomba radhi kwamba kipindi hiki hakiwezi kuonyeshwa katika muda uliokubaliwa awali. Habari zilizopo ni kwamba CCM wakiongozwa na Kinana wameenda leo asubuhi kuwaomba ITV wasionyeshe hicho kipindi katika muda huo na wakaomba ITV waungane na TBC kurusha mkutano wa JK live Jangwani. Safari ya ukombozi ni ndefu lakini lazima tuitembee.

0 comments:

Post a Comment