Saturday, October 30, 2010

Mbinu zinazoweza Kutumika Kuiba Kura

Zifuatazo ni mbinu zitakazotumika kuiba kura kesho na zimeanza kutumika mkoani Shinyanga!!!

1.0 Mabalozi wote wa nyumba 10 na viongozi wa serekali za mitaa wanaitwa, wanapewa karatasi 2 za kupigia kura zilizo na vema tayari kwa mgombea wa kijani. Karatasi moja ni ya mume na moja ni ya mke wake. Kesho kila mmoja atakapoingia chumba cha kupiga kura atatakiwa achukue karatasi ingine (ya awali atakuwa kaificha). Akisha piga kura, atadumbukiza kwenye sanduku karatasi zote mbili. Hivyo mjumbe mmoja atapiga kura 2 na mkewe/mumewe kura 2. Jumla 4

Chadema wafanyeje kudhibiti hali hii??? Waweke daftari ambalo kila anaeingia anaandika namba kuanzia 1 hadi mtu wa mwisho. Baada ya kuhesabu kura, zitakazozidi zitakuwa ni zile zilizochakachuliwa!!!!!

Kama itawezekana, kila mpiga kura akaguliwe idadi ya karatasi atakazotumbukiza kwenye sanduku la kupigia kura. Else, wawakague watu kabla hawajawapa karatasi za kupigia kura, kujiridhisha kwamba, hawana vibomu/videsa vya ziada.

Its serious vikao vinaendelea kutimiza azma ya kupiga kura kwa design hiyo, japo maeneo yaliyolengwa ni yale yenye upinzani wa kweli. Mf. Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Mwanza na Mara. DSM inaogopwa sababu ya mwamko na kusambaa kwa taarifa sababu ya teknologia!!

2. Mbinu ya pili ni kutoa karatasi za kupigia kura zisizo na muhuri sambamba na zenye muhuri wa tume ya uchaguzi, ambapo karatasi zisizokuwa na muhuri zitachukuliwa kuwa batili kwa sababu hazijapigwa muhuri wa NEC.

Chadema wafanye nini hapa!!! Kila mtu anapofika kupiga kura, mawakala wapitie kila karatasi anayopewa mpiga kura kuhakikisha kwamba karatasi anayopewa mpiga kura ina muhuri sahihi.

3. Kuchakachua kura zikiwa njiani kwenda kwa msimamizi mkuu wa uchaguzi wa jimbo!!! Kwenye sheria za NEC na taratibu za internal control (Sarbanese Oxley Act), hapa kuna leakage. Hakuna anaeweza kuthibitisha kuto kuchakachuliwa kwa masanduku ya kura njiani kwakuwa mawakala hawana uwezo kusindikiza kura hizo!!!

Naomba kuwashirikisha mbinu hizo chafu kutokea Shinyanga!!! Hali si hali

Mungu awalinde na kuwabariki, awawezeshe nyote kupiga kura kwa umakini na kwa amani na kumpata Raisi wa kutuongoza kwa kipindi kijacho cha miaka mi tano mwenye hekima, akili, busara na hofu ya Mungu ndani yake!!!

0 comments:

Post a Comment