Tuesday, October 12, 2010

Slaa: Sitaki Urais wa Damu

Akiwa mwishoni mwa ziara yake mkoani Kigoma, Dk Slaa aliwataka wananchi kujihadhari na CCM na Kikwete kuhusu kauli za kuwamga damu zinazosambazwa na wanapropaganda wa CCM. Hii ndiyo kauli yake:

“Mimi sitaki kwenda Ikulu kwa kumwaga damu ya Mtanzania yeyote. Sijatamka hata siku moja kumwaga damu. Nataka uchaguzi wa amani na utulivu. Katika mikutano yangu zaidi ya 400 niliyofanya sasa, nimehimiza watu wangu kuzingatia amani…Nyie mkipigwa shavu hili geuza jingine, msiwe chanzo cha vurugu.

“Amani haihubiriwi, bali inajengwa kama vile Chadema inavyowajenga Watanzania katika sera zake. Tunaposema kutoa elimu bure, afya bure na kuboresha makazi ni kwa faida ya Watanzania wote, hatutaki kujenga matabaka….Lakini CCM imekuwa inapeleka vijana wake kwenye makambi kujiandaa kufanya fujo…Lakini wajue kuwa amani itakuwapo kama haki itatendeka.

0 comments:

Post a Comment