Hapa tupo gado akitua tu Dk Slaa tunaye"
Ila hawa wananchi mbona ni wengi sana itakuwaje hawawezi kufanya fujo"
Jamaa hakuna kulala hadi kieleweke twendeni uwanja mwingine kama huu hapa wamezuia"
Mzee salama hapa ama ?kwani kuna nini ni vita ?"
Hapa tupo kamili kwa lolote "kama wanazungumza
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoa wa Iringa wakiwa wamejipanga kwa lolote katika viwanja vya uwanja wa shule ya msingi Mlandege mjini Iringa ambako ulipangwa mkutano wa mwisho wa mgombea urais wa Chadema Dk Willibrod Slaa ambaye hata hivyo hakuweza kutua katika uwanja huo kama njia ya kukepa mbinu za CCM kutaka kuvuruga mkutano wake huo iwapo angetua katika uwanja huo leo asubuhi
Na Francis Godwin,Iringa
NGOMA nzito Iringa mgombea wa urais kupitia Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbroad Slaa amegonga mwamba kutaka kufanya mkutano wa kampeni bila kibali katika viwanja viwili tofauti mjini Iringa, baada ya Polisi wa kutuliza ghasia (FFU) kutanda katika viwanja vyote kuzuia mikutano hiyo kwa madai kwamba haina baraka za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Polisi waliokuwa na silaha kali na mabomu ya kutoa machozi, walifanikiwa kuwatawanya maelfu ya wafuasi wa chama hicho waliokuwa wakiendelea kukusanyika kwa wingi katika uwanja wa Mwembtogwa mjini hapa kuanzia saa mbili na nusu asubuhi.
Baada ya kutawanywa, wananchi hao walielekea katika uwanja wa Shule ya Msingi Mlandege walikotangaziwa kwamba Dk Slaa angetumia jukwaa la mgombea udiwani wa kata ya Kwakilosa, kuwasalimia wananchi wa jimbo la Iringa Mjini kabla hajaendelea na ziara yake ya mikutano ya kampeni katika majimbo ya Njombe Kaskazini, Njombe Magharibi na Songea Mjini.
0 comments:
Post a Comment