Tuesday, February 15, 2011

HOTUBA YA ZITTO KABWE BUNGENI

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchukua fursa hii kwanza, kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa kunichagua tena kuwa Mbunge wao kwa kipindi cha pili. Kitu pekee ambacho napenda kuwaahidi ni kuwatumikia kwa uaminifu na uadilifu mkubwa na kuhakikisha kwamba tunafanya mabadiliko. Wao wanafahamu kwamba miaka mitano iliyopita tuliitumia kwa ajili ya kuimarisha miundombinu. Tumejenga barabara na kufungua maeneo ambayo yalikuwa hayafikiki. Miaka mitano ijayo tutaielekeza kwenye kuhakikisha kwamba vijiji vyetu tunapata nishati, rural electrification ili na watu wa Kigoma nao wajione ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kukupongeza wewe binafsi kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika na napenda kuwapongeza Wabunge wote kwa umoja wetu bila kujali vyama vyetu kwa kuweza kufika hapa Bungeni na kuwa Wabunge wa Bunge hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye kipaumbele namba 2 katika hotuba ya Rais, kipaumbele cha ukuzaji wa uchumi. Na nikipata muda nitagusia kidogo kipaumbele namba 3. Kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita uchumi wa Taifa letu umekuwa ukikua kwa wastani wa asilimia 7. Lakini, takwimu zinaonyesha kwamba katika kipindi hicho hicho hali ya umaskini wa wananchi wetu imepungua kwa asilimia 2.5 tu. Wenzetu Uganda ambao uchumi wao umekuwa ukikua kwa asilimia 6 katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, wapepunguza umaskini kwa asilimia 25. Nchi za South East Asia kama Malaysia ambao miaka ya 1970 tulikuwa nao sawa, ambapo zaidi ya asilimia 56 ya watu wao walikuwa ni maskini, leo ni asilimia 3 tu ya wananchi wao ni maskini. Tanzania asilimia 37 ya wananchi ni maskini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna tatizo kubwa sana la kutoweza kutatua issue ya inequality katika nchi yetu. Tumejikuta tunatengeneza mataifa mawili; taifa la matajiri na taifa la maskini. Na mgawanyiko huu umetanuka mpaka kwenye huduma. Leo kuna shule za maskini na shule za matajiri. Crisis tunayoizungumza leo ya watoto wa kidato cha nne kufeli sana au wa darasa la saba kufeli sana, siyo watoto wa Wabunge, siyo watoto wa watu wenye uwezo, ni watoto wa maskini kabisa. Watoto wa watu wenye uwezo wako kwenye shule za academies n.k.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye afya hali ni hiyo hiyo. wakati zamani ilikuwa huduma ya afya ya msingi ni ya kila raia kuipata, leo wenye uwezo wa fedha wana hospitali zao, maskini wana hospitali zao. huduma za usafiri hivyo hivyo na kila kitu. Kwa sababu tumeshindwa kuhakikisha ukuaji wa uchumi wa Taifa letu una-address hali nzima ya inequality (kutokuwa na usawa). Na hilo hatulizungumzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapata investment nyingi sana, nimesikia kule Mchuchuma na Liganga wanakuja watu, ten billion dollars investment. Lakini, haita-penetrate chini. Hatujawa na sera mahsusi za kuhakikisha tunakuza watu wa chini, na njia pekee, na aliniambia Mahatri Mohammed juzi nilipokuwa Malaysia, hatujengi mikakati ya klu-crate jobs. Vijana wengi sana hawana ajira, na hii ni time bomb, we don’t address this.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais, katika kipaumbele chake cha tatu anazungumzia kujenga middle class. Sina problem na hiyo, mimi ni mjamaa, naamini katika ujamaa. Kwa hiyo, ningepaswa kutokuamini katika kuwa na middle class. Lakini, unajengaje middle class bado hatujaweza ku-address tatizo la watu wa vijijini ambao ndio maskini zaidi! Na reason is very clear, taarifa za Serikali zote zote, Waziri wa fedha yuko hapa, taarifa zote za MKUKUTA, mipango yetu yote inaonyesha kwamba ili tuweze kuwavuta
watu maskini, tuwaondoe, tuwapandishe, ni lazima sekta ya kilimo ikue kati ya asilimia 6 na 8 miaka mitatu mfurulizo. For the last 5 years tumekua kwa asilimia 3.

Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira ya uwekezaji yanazidi kuwa mabaya siku hadi siku, na we a very happy, some of us ni creators wa hayo mazingira, kwa sababu ni lazima tukiri. Na kama wawekezaji kwa maana ya internal na external hawaji kuwekeza, where will people get jobs! Kama private sector haipati mazingira mazuri ya kufungua viwanda, ya kufungua mashamba n.k. where will people get jobs! And this is not addressed. Tutapigana vijembe vya kisiasa tu, lakini tukumbuke hatima yake Watanzania watatuuliza mmekaa miaka mitano, mmefanya nini? Ni lazima sote (both sides of the houses) sisi Kambi ya Upinzani na watu wa Chama cha Mapinduzi tukubaliane tuhakikishe kwamba ni wapi tunataka kulipeleka hili Taifa. Tuweke pembeni kabisa hizi tofauti zetu, otherwise tutaenda kupata matatizo makubwa sana. Na nisingependa niishi katika umri wangu uliobakia nione nchi inasambaratika. Ningependa nione Tanzania inakuwa imara zaidi na zaidi.

Mheshimikwa Naibu Spika, la pili, la energy: Rais amezungumza kuongeza access to electricity mpaka asilimia 30. Sasa hivi Tanzania asilimia 14 tu. Katika kila nyumba 100 Tanzania, ni nyumba 14 tu zina umeme, 50 years after independence. Lakini uzalishaji wetu wa umeme bado ni mdogo na Waziri wa Nishati na Madini kila siku anatutajia miradi humu Bungeni na nje kwenye ma-press conference. Hatuambii ni mradi gani utatekelezwa l
ini! Lazima tukubaliane kama Bunge, tuseme tuchague basi angalau mradi mmoja, tunapofika tarehe 9 Desemba, tunasherekea miaka 50 ya uhuru, tunasema sasa angalau tumevuka 1000MW za umeme zinazozalishwa kwa uhakika. Otherwise we can’t go anywhere, we can’t. Sasa hivi nchi hii ina deficit ya umeme 2000MW, yaani umeme ambao unapaswa uwe umezalishwa hauzalishwi. Haiwezekani na hatuwezi kuendelea. 1992 sisi na Malaysia wote tulikuwa tuna power cut, wote, 1992. Wenzetu leo wana surplus 7000MW, sisi tuna deficit 200MW – 300MW. Lazima tukae tukubaliane ni namna gani ambavyo tunataka kui-transform nchi hii, vinginevyo tutaishia kuwa nchi ya maneno, tutaishia kuwa nchi ya kurushiana vijembe, tutaishia kuwa nchi ya kuzungumza tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi naamini, mimi na vijana wenzangu ambao tuko humu Bungeni, hatutakubali. Na naomba vijana wenzangu wa pande zote mbili tukae, maana hii ndiyo nchi yetu sisi. Sisi ndio tutakaoishi muda mrefu zaidi kama Mungu akipenda. Akina Mzee Cheyo hawa sasa hivi tayari ni Alasiri. Ndio ukweli huo. Tukae, tuone ni namna gani ambavyo tutavuka mbele zaidi. Energy na growth ni very important. Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

0 comments:

Post a Comment