Thursday, October 7, 2010

Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

Nimelala nimekesha, jambo nimefikira
Bongo nimezichemsha, sipati jibu sawia
Hivi kweli Umekwisha Uzalendo Tanzania?
Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

Ona walivyoziuza, rasilimali za mtanzania
Kwa kweli inashangaza, mikataba waloingia
Kisha tukiwauliza, hawana la kutwambia
Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

Rushwa imekuwa ngao, kumdhulumu raia
Ubinafsi kwao nguo, vazi la kujivunia
Hizi ndizo sera zao, katu hawajui njia
Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

Wananchi amkeni, haki kujitafutia
Mtalala mpaka lini?, saa imeishawadia
Uwongo ukataeni Waache kuwatania
Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

Mkipiga kura zenu, chagueni mwenye nia
Waonesheni wanenu, muelekeo na njia
Fanyeni vitu vyenu, tuiokoe Tanzania.
Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

Mchagueni Slaa, kiboko cha Mafisadi
Huyu bwana hana njaa, atatwanga wakaidi
Ni kiongozi shujaa, si mtumwa wa itikadi
Mchagueni Slaa, tuiponye Tanzania

0 comments:

Post a Comment