Monday, February 21, 2011
Dk Wilbrod Slaa Ashiriki Kwenye Misa Ya Watu wa Tatu Wa Familia Moja Waliofariji Kwa Ajali ya Mabomu Gongo la Mboto
Sunday, February 13, 2011
Wabunge wa CHADEMA Wazindua Matawi vyuo Vikuu
Wabunge waliowakilisha Chama ni
1. Prof Kahigi- Bukombe
2.Halima Mdee- Kawe
3.John Mnyika-Ubungo
4.Godbless Lema-Arusha Mjini
5.Rebecca Mgodo-Viti Maalum Arusha
6.Regia Mtema- Vitimaalum Kilombero
Wanafunzi zaidi ya 200 wa Chuo Cha Mt John wamejiunga na CHADEMA sambamba na ufunguzi wa ofisi ya tawi hilo.
Zaidi ya wanafunzi 1000 wa Vyuo vya Mipango na UDOM wamejiunga na CHADEMA Sambamba na ufunguzi wa Tawi.
Wabunge hawa walipokelewa kwa nderemo na vifijo na wanafunzi hao.
Mapambano yanaendelea,Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.
Tuesday, February 1, 2011
TAMKO LA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHADEMA KUHUSU HALI YA TAIFA
Kamati Kuu ya CHADEMA katika kikao chake cha kawaida kilichofanyika tarehe 29-30 Januari 2011 jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa Taifa Mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe (Mb), pamoja na mambo mengine, imepokea, kujadili na kutolea maazimio Taarifa ya Hali ya Siasa na Taifa kwa ujumla. Maazimio haya yapo katika maeneo matano yafuatayo.
1. Mchakato wa Upatikanaji wa Katiba Mpya.
Kamati Kuu imezingatia na kupongeza juhudi za Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni pamoja na wadau mbalimbali wa demokrasia nchini za kudai Katiba Mpya. Aidha, Kamati Kuu imejadili na kutafakari kwa kina maoni ya wadau mbalimbali juu ya mchakato unaofaa katika kupata Katiba Mpya, na kuzingatia kuwa njia sahihi ni ile itakayowashirikisha wananchi kikamilifu na kwa dhati bila kujali tofaui zao za kisiasa, dini, umri, elimu, kabila wala jinsia zao. Kamati Kuu imezingatia pia kwamba Tume ya Rais sio njia sahihi itakayowezesha upatikanaji wa Katiba Mpya yenye kuzingatia utashi, matakwa na mahitaji ya wananchi wa Tanzania. Hivyo basi:
- Kamati Kuu imepinga utaratibu wa kuunda Tume ya Rais katika uundaji wa Katiba Mpya
- Kamati Kuu imeunga mkono utaratibu wa kutumia Bunge katika kutengeneza na kusimamia mchakato utakaoletekeza upatikanaji wa Katiba Mpya
- Kamati Kuu imeipongeza Sekretariati yake kwa kumwagiza Mheshimiwa John Mnyika kuandaa na kuwakilisha Hoja Binafsi inayolitaka Bunge kuandaa sheria itakayoweka utaratibu na mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya
- Kamati Kuu imewahimiza na kuwaomba wabunge wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuunga mkono Hoja Binafsi ya Mheshimiwa Mnyika kwa maslahi ya Taifa.
2. Mauaji yaliyofanywa na Jeshi la Polisi Jijini Arusha
Kamati Kuu imepokea kwa masikitiko taarifa ya vifo vya wananchi watatu wasio na hatia kwa kupigwa Risasi na askari wa Jeshi la Polisi kufuatia vurugu zilizosababishwa na Jeshi hilo katika harakati zao za kuzuia maandamano halali na yenye Baraka zote za Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilayani Arusha. Aidha, Kamati Kuu imesikitishwa na uvurugwaji wa uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha kulikofanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa maelekezo ya Chama cha Mapinduzi na Serikali yake. Katika maazimio yake:
- Kamati Kuu imewapa pole ndugu wa wafiwa wa vurugu za Arusha pamoja na wananchi wa Arusha na watanzania kwa ujumla
- Kamati Kuu imewapongeza Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Mhe Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk Willibrod Peter Slaa, Mbunge wa Arusha Mjini Mhe Godbless Lema na viongozi wengine wa CHADEMA kwa juhudi zao kubwa za kuepusha shari na kutoa uongozi wa kisiasa pale ambapo wananchi wa Arusha walitelekezwa na viongozi wa Serikali ya CCM katika kipindi chote cha matatizo ya Arusha
- Kamati Kuu imeiagiza sekretariati ya CHADEMA kuendelea na harakati za kudai haki za wananchi wa Jiji la Arusha kwa njia za kisiasa.
- Kamati Kuu imewaagiza madiwani wa CHADEMA katika Halmashauri ya Jiji la Arusha kuendelea kuingia katika vikao vya Baraza la Halmahauri hiyo na kuwawakilisha wananchi waliowachagua kikamilifu na wahakikishe kuwa wanatumia nafasi yao kufanikisha uchaguzi wa Meya.
3. Matatizo ya Nishati ya Umeme na Gesi na Malipo kwa Kampuni Hewa ya Dowans
Kamati Kuu imesikitishwa na kupanda holela kwa bei za nishati muhimu za umeme na gesi, pamoja na kushindwa kwa serikali ya CCM katika kuwekeza kikamilifu katika sekta ya nishati hapa nchini. Aidha, Kamati Kuu imesikitishwa na kufadhaishwa sana na uamuzi wa CCM na serikali yake kuridhia kuilipa Kampuni hewa ya Dowans fedha za walipa kodi wa Tanzania zipatazo Shilingi bilioni 94, pamoja na kwamba Kampuni hii ilikwishaharamishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa niaba ya wananchi.
Kamati Kuu imetambua kuwa sakata la Dowans ni mwendelezo wa vitendo vya kifisadi ndani ya CCM na serikali yake ambavyo vimeligharimu taifa hili kwa miongo mitano iliyopita. Hivyo basi:
- Kamati Kuu imewahimiza wana CHADEMA, wabunge na wananchi kwa ujumla kuendelea kupinga kwa nguvu zote malipo ya Dowans
- Kamati Kuu imewaelekeza viongozi pamoja na wabunge wa CHADEMA kuendelea kuwahamasisha wananchi kupinga kwa njia mbalimbali za kisiasa na kisheria malipo ya Dowans na ufisadi mwingine hapa nchini
- Kamati Kuu imewapongeza na kuwashukuru wanaharakati wa taasisi za kiraia kwa ujasiri na moyo wao wa kizalendo kwa uamuzi wao wa kufungua kesi mahakamani ya kupinga malipo ya Dowans
- Kamati Kuu imeiasa Serikali ya CCM kutokuona aibu kutekeleza sera za CHADEMA zilizofanyiwa utafiti kuhusu namna ya kujenga na kuimarisha sekta ya nishati ya umeme na gesi hapa nchini ili nchi yetu iondokane na tatizo la kudumu la umeme.
- Kamati Kuu imeiagiza Secretariat yake kuanza maandalizi ya maandamano ya nchi nzima ya kupinga ongezeko la bei ya umeme, gesi na kuilipa Dowans. Na tarehe 24/02/2011 itakuwa siku ya kuanza maandamano kwenye Jiji la Mwanza na miji mingine kadiri ratiba itakavyotolewa.
4. Matokeo ya Kidato cha Nne
Kamati Kuu imeyapokea kwa masikitiko makubwa matokeo ya Kidato cha Nne yanayoonyesha kuwa nusu ya watahaniwa wote wamefeli Mtihani huo. Aidha, Kamati Kuu imezingatia na kusikitishwa na taarifa kuwa ni asilimia 11.5 tu ya watahiniwa ndio waliopata daraja la I hadi la III. Ndio kusema kuwa karibu asilimia 90 ya vijana wote waliomaliza kidato cha nne mwaka 2010 hawawezi kuendelea na elimu yeyote ya juu na itakuwa ni vigumu sana kwa vijana hawa kupata aina yeyote ya ajira ya uhakika.
Aidha, Kamati Kuu imezingatia kuwa matokeo mabaya ya Kidato cha Nne yamesababishwa na sera dhaifu za serikali ya CCM zenye kulenga kughilibu wananchi kwa ajili ya mafanikio ya kisiasa kwa kukazania wingi wa majengo ya shule badala ya ubora wa walimu na ubora wa shule. Kutokana na hali hii:
- Kamati Kuu imeyatangaza matokeo ya Kidato cha Nne ya mwaka 2010 kuwa ni Janga la Kitaifa
- Kamati Kuu imeitaka Serikali ya CCM isione aibu kutekeleza sera za elimu za CHADEMA zilizoanishwa katika ilani yake ya mwaka 2010, ikiwemo sera ya kutoa elimu bure na kuboresha maslahi na mazingira ya kazi ya walimu ambazo zilielezwa na wataalamu wa elimu kwamba ndio sera sahihi za kufufua ubora wa elimu ya nchi yetu
- Kamati Kuu imeunda timu maalumu ya wataalamu wa elimu kwa ajili ya kutafiti kwa kina sababu za matokeo mabaya ya Kidato cha Nne na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati Kuu katika kikao chake kitakachofanyika kabla ya Mwezi Mei 2011.
5. Kuhusu propaganda za udini hapa nchini
Kamati Kuu imesikitishwa na propaganda zinaendelezwa na viongozi wa juu wa Chama cha Mapinduzi, hususani Rais Kikwete, kuhusu kuwepo kwa mfarakano wa kidini hapa nchini. Kamati Kuu imezingatia kuwa wananchi wa Tanzania wameendelea kuishi kwa amani, upendo na mshikamano mkubwa bila kujali tofauti zao za kidini. Kamati Kuu imezingatia kuwa Viongozi wa juu wa CCM, na hasa Rais Kikwete, ameamua kuficha udhaifu wake wa kiuongozi chini ya zulia la udini ili wananchi waache kujadili mambo ya msingi ya Taifa hili, ikiwemo kushindwa kwa CCM kutekeleza ahadi ambazo imekuwa ikizitoa katika miongo mitano iliyopita. Hivyo basi:
- Kamati Kuu imewahimiza wananchi wa dini zote hapa nchini kuendelea kuishi kwa amani na mshikamano na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii bila kujali tofauti zao za dini, ukabila wala itikadi ya siasa
- Kamati Kuu imewataka viongozi wa juu wa CCM na hasa Rais Kikwete kuacha kuchochea mgawanyiko wa dini hapa nchini kama njia ya kuficha udhaifu wake wa uongozi
- Kamati Kuu imewahimiza viongozi wa dini zote hapa nchini kuendelea kukemea maovu yeyote katika jamii bila woga wala upendeleo kwani hilo ni jukumu lao la msingi.
6. Kuhusu Ushirikiano wa Vyama vya Siasa vya Upinzani
Kamati Kuu imeendelea kuzingatia umuhimu wa vyama vya siasa kushirikiana katika kuimarisha nguvu ya upinzani hapa nchini. Hata hivyo, Kamati Kuu imezingatia kuwa Chama cha Wananchi (CUF) wamejiunga na CCM kuunda Serikali ya Umoja Kitaifa Zanzibar, na kwa kuwa Sheria inayoruhusu uwepo wa vyama vya siasa inahusu pande zote za Muungano, na kwa kuwa vyama vingine vya upinzani vyenye wabunge wamo katika ushirikiano na CUF, Kamati Kuu imeona kuwa CHADEMA haiwezi kuwa na ushirikiano wenye tija na vyama hivyo. Hivyo basi Kamati Kuu imemwagiza Kiongozi wa Kambi ya Upinzani kuunda Baraza la Kivuli kwa kuhusisha wabunge wa CHADEMA pekee.
7. Kuhusu mpango mkakati wa chama 2011-2016.
Kamati Kuu ilijadili na kupitisha mapendekezo ya mpango kazi wa chama kwenye Baraza kuu la chama .Pia ilijadili na kupitisha mpango kazi wa mwaka 2011-2012.
Tamko hili limetolewa leo tarehe 31/01/2011.
Dk Willibrod Peter Slaa
Katibu Mkuu
Sunday, January 30, 2011
Chadema waandaa bajeti kuikabili CCM
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemrejeshea cheo cha Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, na kupanga mikakati ya kukabili CCM katika mikoa yote nchini.
Uamuzi huo ulifikiwa jana na Kamati Kuu ya Chadema, kwenye mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo walipanga bajeti ya kufanikisha mipango yao ya kujiimarisha mikoani.
Zitto alinyang'anywa cheo hicho Novemba mwaka jana kwa kile kilichoelezwa ni kwenda kinyume na uamuzi wa chama.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zilieleza kwamba uamuzi huo ulifikiwa baada ya mjadala mzito.
Baadhi ya wajumbe walimlaumu Zitto kwamba msimamo wake wa kutangaza hadharani kupitia vyombo vya habari hakubaliani na uamuzi wa chama kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, umesababisha kukigawa chama.
Zitto alinyang'anywa cheo hicho kutokana na msimamo wake wa kutounga mkono uamuzi uliopitishwa na wabunge wa chama hicho wa kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete kwa kutoka nje ya Bunge.
Zitto na wabunge wengine hakuingia bungeni siku hiyo na aliweka msimamo wake waziwazi kwenye vyombo vya habari kwamba ingawa chama kimekubaliana hivyo, yeye binafsi haungi mkono.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Zitto pamoja na kurejeshewa cheo hicho, alionywa kwa maelezo kwamba hakupaswa kutangaza msimamo wake hadharani.
Chanzo hicho kilieleza kwamba wajumbe walimuonya wakisema angeweza kukaa kimya na kubakia na msimamo wake na hali hiyo isingekiaibisha chama.
Jambo jingine lililozungumza katika kikao hicho ni mgawanyiko ndani ya chama ambao umesababisha kukosa baadhi ya majimbo kwenye uchaguzi uliopita.
Walisema mgawanyiko ndani ya chama hicho ulisababisha wakose majimbo mengi mkoani Kigoma wakati walikuwa na nguvu kubwa ya kisiasa.
Majimbo matano ambayo chama hicho ilikuwa iyachukue, walisema yalinyakuliwa na NCCR-Mageuzi na wao kuambulia moja tu.
Walitoa mfano kwa jimbo Kigoma Kusini ambalo kama sio kumumfukuza ndani ya chama, David Kafulila, wangeweza kulinyakua.
Kafulila ambaye alionyesha kuwa na ushawishi mkubwa kwenye jimbo hilo baada ya kufukuzwa Chadema alihamia NCCR na kushinda kiti hicho.
Awali katika kikao hicho, ambacho kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Habari wa Chadema, Erasto Tumbo,kitajadili masuala mbalimbali yanayohusu chama hicho, ikiwa ni pamoja na kujadili agenda zilizojadiliwa katika kikao kilichotangulia.
Tumbo alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa, agenda kubwa ya kikao hicho, ambacho alisema watatoa tamko baada ya kumalizika, kitajadili mpango mkakati wa Chadema kwa mwaka 2011.
Katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Septemba, 2010, suala la uteuzi wa nafasi za viti maalum kwa wabunge wa chama hicho ambalo lilizua malalamiko ya kuwepo kwa upendeleo, hatua iliyofanya viongozi waandamizi wa chama hicho kwa nyakati tofauti kulitolea ufafanuzi suala hilo.
Kwa mujibu wa taarifa ya vigezo hivyo vya uteuzi wa wabunge iliyotolewa na Dk Kitila Mkumbo, ambaye alikuwa mwenyekiti wa uteuzi huo, mgombea yeyote ambaye aliwahi kushika wadhifa wa ubunge aliwekewa alama 10 ambacho ni kigezo kimojawapo kati ya sita.
Dk Mkumbo aliongeza kuwa kigezo kingine kilichotumika ni cha uzoefu wa uongozi nje ya siasa, ambacho nacho alifafanua kuwa kilikuwa kimegawanywa katika madaraja mbalimbali.
Kwa Mujibu wa Dk Mkumbo, njia hizo zilitumika ili kuondoa malalamiko mbalimbali yaliyokuwepo, ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa upendeleo wa watu wanaotoka Kanda ya Kaskazini.
Kamati kuu ya chama hicho ilikutana Septemba 25, 2010 kujadili suala hilo lakini haikuweza kufikia muafaka na hivyo kulazimika kuendelea na mkuatano huo Septemba 26.
Mkutano huo ulishindwa kumaliza ajenda zake baada ya makundi kuibuka juu ya njia ya kuwapata wabunge hao.
Makundi hayo yalidaiwa kuegemea vigogo wawili wazito ndani ya chama hicho, jambo ambalo liliipasua pia meza kuu na kuiweka katika mazingira magumu katika kuokoa jahazi.
Chama hicho hatimaye kilipitisha majina ya wabunge 105 wa viti maalum, huku kikiwaacha wanachama 42 walioshindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa.
Majina hayo hayakuwekwa hadharani na badala yake yalipelekwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ambapo baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 31 ambapo Chadema ilisimamisha wagombea wa majimbo 185, na kufanikiwa kutwaa majimbo 25, na kupata viti maalum 23.
Monday, January 24, 2011
TAMKO LA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO CHADEMA MKOA WA DODOMA KULAANI MATUMIZI MABAYA YA NGUVU ZA POLISI MKOANI ARUSHA
UTANGULIZI.
Ndugu Mgeni rasmi, awali ya yote tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema na uzima anaozidi kutujalia. Tumekusanyika hapa leo hii kwa Amani, ili kuweza kuunga mkono Tamko la CHADEMA Taifa juu ya mauaji ya Raia watatu (1) Denis M. Shirima (2) Ismail Omari (3) Paulo Njuguna (Mkenya) wasiokuwa na hatia yaliyofanywa na Serikali dhalimu kupitia Jeshi la Polisi Mkoani Arusha. Lakini pia tunawapa pole wale wote waliofikwa na maafa mbalimbali yaliyosababishwa na vurugu zilizoanzishwa na Jeshi la Polisi
TUSIMAME KWA DAKIKA 1 KUWAKUMBUKA MASHUJAA HAO WATATU WALIOPOTEZA MAISHA.
Ndugu Mgeni rasmi, CHADEMA (Mkoani Dodoma) tunaamini kabisa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 20 (1) na Tamko la haki za binadamu la umoja wa Mataifa ya mwaka 1948, (yaani Universal Declaration of Human Rights) kuwa ni haki ya msingi ya kila Raia kuandamana kwa Amani ndani ya Nchi yake. Na Jeshi la Polisi kuwa kama nyenzo ya kulinda Amani na si kuvuruga Amani. Hii ni haki ya kikatiba ya wananchi wa Tanzania.
Ndugu Mgeni rasmi, imekuwa tabia ya CCM na Serikali kupitia Jeshi la Polisi kuwapora Raia wa Tanzania haki zao za msingi na za Kikatiba kwa kisingizio cha kuvurugika kwa Amani,jambo ambalo halivumiliki na halikubaliki. Watanzania wamejua na wanaamini kuwa Jeshi la Polisi ni chombo cha kuwalinda wao (Wananchi) na mali zao. Jeshi la Polisi kwa sasa limekuwa chombo cha kuvuruga Amani na kupora mali za Watanzania kwa kisingizio cha maono ya “kiintelijensia”. Je Intelejensia” hiyo haiwezi kutumika kwa kutazama madhara ya kuzuia maandamano hayo ya Amani? Maandamano ya mazishi ya wahanga wa mauaji ya Arusha ni ushahidi tosha kuwa dhana ya inteligensia ni fikra potofu na hupikwa na kikundi kidogo cha watu kwa ajili ya maslahi yao.
Ndugu Mgeni rasmi, CHADEMA Dodoma, Tunawapa pole Ndugu na jamaa za mashujaa waliopoteza maisha katika harakati za kudai haki zao na za Watanzania wote kwa ujumla. Vilevile tunawapa pole majeruhi wote walioumizwa na Jeshi la Polisi linalotaka kuingiza Tanzania katika machafuko makubwa. Tunawaombea majeruhi wote wapone haraka na kuwataka wasikate tamaa badala yake waendeleze mapambano mpaka kufikia lengo.
Ndugu Mgeni rasmi, Tunawapa pole na pongezi za dhati Viongozi wetu makini wa chama kitaifa Mwenyekiti Freeman Aikaeli Mbowe, na Katibu Mkuu Dr Wilbrod Peter Slaa, (Katibu Mkuu Taifa), na Wabunge wa majimbo na wa viti maalumu wa CHADEMA walioongoza mapambano dhidi ya Serikali dhalimu inayotumia nguvu nyingi na kodi za Watanzania waliopigika kupora haki zao.
Ndugu Mgeni rasmi, CHADEMA DODOMA tunalaani nguvu za kivita zilizotumiwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha KUPAMBANA NA RAIA WASIO NA SILAHA WALIOBEBA MAJANI NA VITAMBAA VYEUPE, jambo lililopelekea mauaji ya watu watatu wasiokuwa na hatia na kupelekea wengine wengi kubaki vilema na majeraha yasiyokuwa ya lazima. Tunaungana na Viongozi wetu wa CHADEMA Kitaifa kulitaka Jeshi la Polisi kwanza kuwaomba radhi Watanzania kwa kusababisha majonzi makubwa yaliyogharimu maisha ya Ndugu zao, pili kuwataka wahusika wakuu waliosababisha vurugu hizo kuwajibika wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nchi Ndugu
Shamshi Vuai Nahodha, akifuatiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema au Bwana “Intelijensia” na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha (RPC) Thobias Andengenye.
Ndugu Mgeni rasmi, Tunalitaka Jeshi la Polisi nchini kutoendeleza tabia ya kuwanyanyasa Wana wa nchi hii (Watanzania) kwa sababu ya maslahi ya watu wachache hasa Viongozi wa CCM, kinyume na hapo wao watakuwa wa kwanza kuhukumiwa kwa tabia hiyo, kwani Watanzania watashindwa kuvumilia. Tunalisihi Jeshi la Polisi kutoa Ulinzi na kuhakikisha usalama wa Watanzania hasa pale wanapotaka kupaza sauti zao kwa njia ya maandamano ya Amani. Polisi kamwe hawajapata mamlaka ya kisheria ya kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano bali kuweka ulinzi na kuhakikisha sauti za watanzania zinafika mahali husika. Kupitia hadhara hii tunatangaza kusimamia haki zetu.
Sisi kama Watanzania tunaliagiza Jeshi la Polisi kuacha mara moja tabia ya kukurupuka na kutumia silaha nzito kwa Watanzania
wasiokuwa na hatia (vurugu) pindi wanapodai haki zao. Maandamano kama yale ya Arusha na ya wanavyuo mfano Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yalikuwa ya amani na hayakustahili kukambiliana na mashambulizi ya kivita! Tunawapa pole watanzania wote waliokumbana na mikikimikiki kutoka kwa Jeshi la Polisi.
· Kwanza ni kutokuwa na katiba inayoeleza wazi zile haki za msingi za mtanzania na nguvu zake katika kutetea haki hizo.
· Pili ni kutokuwa na viongozi makini na wenye uwezo wa kuthubutu kuheshimu haki za watanzania, wakiongozwa na viongozi wa CCM .
· Tatu ni dharau na ukatili wa viongozi wa jeshi hilo waliokengeuka na kujengeka kifikra kwamba vyeo au madaraka wanayoyapata yametokana na uswahiba wao na viongozi wakuu wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi!
Ndugu mgeni rasmi , sababu hizo, msingi wake hasa ni ubovu wa katiba yetu inayotoa mwanya kwa viongozi wa serikali na jeshi la polisi kutokuheshimu UMMA wa watanzania kwa kuwa katiba hiyo ilitungwa na watu wachache, kwa maslahi ya watu hao wachache na si watanzania wote.
Hivyo basi tunaisihi Serikali na kuitaka kuanzisha mara moja mchakato wa katiba mpya ( siyo marekebisho ) itakayotoa fursa kwa kila mwana wa nchi hii kueleza wazi hasa wanahitaji katiba ya aina gani kwa mstakabali wa Taifa hili.
Ndugu mgeni rasmi, tunapenda kutoa angalizo kwa Serikali kuwa, kutowashirikisha watanzania katika maamuzi juu ya katiba mpya kunaweza kulifikisha Taifa hili katika historia chafu ambayo haijawahi kutokea. Dalili za uchafu huu wa historia zimeanza kuonekana kwa kuwa ni tabia ya Serikali ya CCM kuwapuuza watanzania. Tunasisitiza hili “ Maamuzi ya watanzania yaheshimiwe”.
Ndugu mgeni rasmi , CHADEMA DODOMA tunaungana na Viongozi wetu kitaifa kuwasihi na kuwahamasisha watanzania kudai katiba mpya itakayoweka bayana ni Taifa gani wanalolihitaji watanzania. Tunaungana na umma wa watanzania wote kudai uandikwaji wa katiba utakaoongozwa na BARAZA LA KATIBA na kupinga tume inayotaka kuundwa na Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete. Tunasisitiza kuwa zoezi hili lianze mara moja ili kuzuia uwezekano wa uharibifu wa maendeleo na ustawi wa jamii kuendelea kujitokeza. Haya ni maangamizi kwa taifa. Ndugu mgeni rasmi, ni dhahiri kuwa katiba hii tuliyonayo sasa hivi ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya Taifa letu!
Ndugu mgeni rasmi. Tunaomba watanzania waendelee kuwa imara pasipo kutetereka katika kudai haki zao za msingi na kuendelea
kuwakumbuka Ndugu zetu mashujaa walioandika historia katika nchi hii kwa kufa kishujaa walipokuwa wakitetea haki zao na za watanzania wote kwa ujumla. Tunaomba watanzania wote kuendelea
kudumisha amani tuliyonayo ijapokuwa Serikali na jeshi lake la polisi wanataka na wameanza kuvuruga Amani hiyo.
Ndugu mgeni rasmi, tunalisihi jeshi la polisi kuelekeza nguvu zake na silaha zake nzito nzito kupambana na wahalifu wanaosumbua nchi hii kama majambazi na mafisadi yanayofilisi nchi na siyo kuwa warahisi wa kuwapiga mabomu watanzania waliokuwa huru ndani ya nchi yao kwa kipindi kirefu.
Pia tunaliomba jeshi la polisi kuelekeza nguvu zake za “Kiintelijensia” katika kutabiri na kugundua madhara na athari za mikataba inayoingiwa na Serikali (hilo ndilo la msingi kwa watanzania). Kama vile Dowans, Meremeta, Kagoda kwa kutaja machache tu.
Tunalitaka jeshi la polisi lijenge utamaduni wa kusema ukweli na kuondokana na utamaduni wa kuwabambikia raia kesi mbalimbali ambazo haziwahusu. Mfano wa hili ni mbinu chafu ambazo zinaendelea chini ya jeshi la polisi kuhariri na kurusha kwenye runinga picha zinazoonyesha kuwa CHADEMA ndio chanzo cha vurugu za Arusha! Umma mzima umeshuhudia kuwa maandamano yalikuwa ya amani kwa urefu wa kilomita mbili hadi pale polisi kwa makusudi walipoamua kuanzisha vurugu kwa kuwashambulia waandamanaji kwa
mabomu na risasi za moto. Mkanda huu lakini haukuonyesha polisi walivyodhalilisha na kunyanyasa raia waliowapiga, kuvunja vioo vya
magari, na kupora mali za raia. Tunamtaka kamanda Paul Chagonja kwa niaba ya polisi kuuomba radhi umma wa watanzania kwa juhudi zake za makusudi za kupotosha ukweli na kutetea uovu mkubwa uliofanywa na jeshi la polisi. Tunasisitiza kuwe na tume huru ya kuchunguza mauaji haya. Pia tunasisitiza kuwa viongozi wa CHADEMA na watu wote waliobambikiwa shauri hili wafutiwe kesi, na waachiwe huru bila ya masharti yoyote.
Tunamtaka pia Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda atamke rasmi tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi halali wa Meya wa Jiji la Arusha. Tunamtaka Mh. Pinda atumie wepesi ule ule alioutumia kusimamisha uchaguzi wa meya wa Manispaa ya Kigoma baada ya kulalamikiwa na Chama Cha Mapinduzi. Katika tukio hili Mh. Pinda aliweza hata kupora uhuru wa mahakama na kusimamisha uchaguzi. Maendeleo ya wananchi ni zaidi ya vyeo vinavyong’ang’aniwa na Chama Cha Mapinduzi.
CHADEMA inatoa rai kwa raia wote wa Tanzania kusimama kidete kwa ajili ya haki na maendeleo ya taifa lao. Watanzania wa kada mbalimbali wake kwa waume, wazee kwa vijana, wawe wanasiasa, wasomi, wafanyabiashara, wanafunzi, wakulima na wafanyakazi kuungana mkono na kuhakikisha ustawi wa nchi yetu hauwekwi rehani kwa maslahi ya watu wachache. Tunapaswa kuulinda na kuutetea ustawi wa nchi yetu kwa maslahi ya kizazi hiki na kile kijacho.
Ndugu mgeni rasmi, tunamalizia kwa kusema “Jeshi la polisi litambue kuwa kwa kupitia kodi za raia wa Tanzania, ndipo mishahara yao na posho zinalipwa, pia zana za kazi zao zinanunuliwa. Jeshi la polisi
liwaheshimu watanzania kwani lipo kwa ajili ya kuwalinda wao na mali zao na sio kuwatia ulemavu na kuwapotezea maisha.
Tanzania bila ubabe inawezekana!
Ndugu mgeni rasmi; tunaomba kuwasilisha hoja
“Mungu warehemu mashujaa wetu hawa ISMAL OMAR, DENIS MICHAEL na PAULO NJUGUNA (Mkenya ) wapumzike kwa amani.
MAANDAMANO YA CHADEMA DODOMA
Mkurugenzi wa organaizesheni Ben Kigaila ndiye aliyaongoza na ndiye aliyepokea tamko na kuhutubia. pamoja naye wagombea mbali mbali waliochakachuliwa na kiongozi wa wanafunzi wa udom waliopata nafasi ya kuzungumza na wananchi. Sam Kigaila naye akapewa nafasi ya kuzungumza...Sam ni soo!! sisiemu lazima wamejifunza kuwa hawataweza kuzuia nguvu ya umma kwa kumuangamiza Slaa kwani kuna topaz za uhakika nyuma yake....
Katibu wa mkoa aliweza kutamka rasmi kuwa polisi vihiyo mfano aliyekuwa karani wa mahita akipata cheo ndio mwanzo wa shida. inasemekana wakati maandamano yanaendelea mashuzi yaliwatoka wana ccm na kumpigia RPC kumuuliza kwanini ameruhusu maandamano. Naye aliwajibu kuwa ni ya amani. Polisi waliongoza maandamano yooote kwa uzuri.
Baada ya hapo kamanda kigaila alionana alifungua tawi la chadema kata ya uhuru, akapata kuzungumza na halafu akaonana na wanachadema tawi la UDOM ambao walimueleza mengi yakiwamo manyanyaso wanayofanyiwa na baadhi ya walimu kwa kuwa tu ni wanachadema. Aliahidi kuyafanyia kazi malalamiko hayo..
Baada ya hapo akaenda george town miyuji kuonana na wanafunzi wa chuo cha mipango. akiwa huko alionuyeshwa orodha ya papo kwa papo ya wanafunzi 300 ambao wanatyaka kadi. alihakikishiwa kuwa asilima 95 % ni wana chadema. Uongozi wa muda ulichaguliwa na kuambiwa utafute ofisi na uendelee kuandikisha wanachama. Mheshimiwa Mbowe atakuja kuzindua tawi na kukabidhi kadi..
Wakiwa na wanachuo hao wa mipango, mhenshimiwa dada kunti ambaye ni diwani aliyechakachuliwa wa ipagala aliwataka wanafunzi kuhimiza wanawake na kuanzia magirlfriend wao kuingia CHADEMA kwani ndio tofali lililobaki. Alisisitiza kuwa wanawake wana uwezo mkubwa wa kukinyanyua chama...
Picha za mwisho zinamwonyesha kijana akisimika bendera nyumbani mwa kweleakwelea!
Natuma picha hizi kubatilisha uwongo wa TBCCM kuwa maandamano hayakupata kibali cha wananchi na yalihudhuriwa na watu wachache!
Vyombo vya habari, kazi kwenu!
Naomba kuwasilisha!
Saturday, January 15, 2011
KONGAMANO LA KATIBA UDSM
Waendeshaji wa Mdaharo wa kujadili swala la Katiba mpya ya Tanzania kwa Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA),toka kushoto ni Prof. Issa Shivji,Dr. Kitila Mkumbo pamona ja Ndg. Jenerali Ulimwengu wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa na wajumbe wa mdaharo huo mchana huu katika ukumbi wa Nkurumah,Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Ndg. Jenerali Ulimwengu akizungumza katika mdaharo huo ambao ulikuwa na changamoto nyingi kutokana na mada zilizokuwa zikijadiliwa.
Prof. Issa Shivji azungumza katika Mdaharo huo huku akinukuu baadhi ya maneno yaliyokuwa yakitamkwa na Hayati Mwl. Nyerere kuhusiana na swala la Katiba Mpya.Mdaharo huu umemalizika hivi punde katika ukumbi wa Nkurumah ulipo ndani ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mchana huu.
Mmoja wa Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Mzee Ibrahim Kaduma akichangia mada zilizokuwa zikutolewa na baadhi ya wajumbe waliohudhulia Mdaharo huo kuhisia na swala la kupatikana kwa Katiba mpya ya nchi yetu.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake nchini (TAMWA),Mama Ananilea Nkya akichangia mada katika Kongamano hilo.Thursday, January 13, 2011
meya mpya wa jiji la Mwanza kupitia CHADEMA
Wednesday, January 12, 2011
Maandamano ya CHADEMA Mara
Chadema Mara yaitisha maandamano Jumamosi
George Marato
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Mara, kimeitisha maandamano makubwa utakaohusisha mkoa mzima kupinga kile walichokiita vitendo vya unyanyasaji na ukiukwaji wa haki za raia vilivyofanywa na Jeshi la Polisi mjini Arusha.
Kwa mujibu wa Chadema Mkoa wa Mara, maandamano hayo yatalenga kupeleka ujumbe kwa taifa na dunia kulaani vikali hatua ya jeshi hilo kutumia nguvu kubwa, ikiwamo risasi za moto na mabomu ya machozi kuzima maandamano yaliotishwa na chama hicho hivi karibuni mjini humo.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Nyanza Sibitali, aliliambia Nipashe mjini hapa kuwa maandamano hayo yatafanyika Jumamosi wiki hii yatakayohusisha majimbo saba ya uchaguzi ya mkoa wa Mara na kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kupeleka ujumbe huo.
Alisema Mkuu wa Mkoa ndiye anayetarajia kupokea maandamano hayo kisha kupokea ujumbe huo ingawa alisema bado hawajampata mkuu huyo wa mkoa kumweleza uamuzi huo.
NIPASHE
http://www.ippmedia.com/frontend/fun...le.php?l=25011
Membe: Police killings were wrong
By Rosemary Mirondo
The Citizen Correspondent
Dar es salaam. The minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Mr Bernard Membe, conceded yesterday that the Police in Arusha had acted against their code of conduct when they used excessive force to stop a demonstration by supporters of the Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) in Arusha last Wednesday.
At least three people, including a Kenyan, were killed when police used live ammunition to disperse Chadema supporters who were protesting the election of a CCM candidate to the Arusha mayoral seat.
Mr Membe said this when briefing reporters after his meeting with members of the diplomatic corps.
“The Police Force was supposed to use reasonable force when dealing with civilians in order to ensure that it preserves peace and security,” he said in what he termed as personal views on the Arusha incident in which more than 40 people, including top Chadema leaders, were injured.
He said the Arusha incident has tarnished Tanzania’s image abroad and it would take some time for the government to clean the image.
“During the meeting with ambassadors, they had pressed me to give the government’s stand over the killings... I told them that the government statement would be issued within this week that it was dismayed by the killings,” he said.
He described the deaths as affecting the nation because those who were killed were Tanzanians. “I offer my condolences to the families which lost their loved ones. I also pray for quick recovery for those who have been injured,” he said.
He said the recent Arusha killings were among issues which were extensively debated when he met with the ambassadors at Karimjee Hall.
The diplomats suggested that the Police personnel should be trained on how to handle such incidents so as to avoid casualties in the future, advise which the government was going to work on, he said.
Other reports from the meeting said the envoys blamed the Police for using excessive force when dealing with unarmed demonstrators.
Meanwhile, Prime Minister Mizengo Pinda has said there is a need for strengthening of joint committees between Tanzania and development partners to enable the administration of different activities touching on economic activities, education, culture and trade.
The Premier made the call yesterday in Dar es Salaam during his meeting with Mozambique ambassador to Tanzania, Mr Zacarias Amour Kupela, in his office.
In their meeting the two discussed a wide range of issues that included agriculture, fishery, livestock keeping as well as the growing incidents of piracy in the Indian Ocean.
Mr Kupela told the Premier about a Mozambican vessel that was hijacked by pirates in December 27, last year. Mr Kupela said the vessel which has since been seen in Somali waters contained 24 people, 19 of which were Mozambican, three were Indonesian and one from Spain.
Wednesday, November 10, 2010
DR SLAA ALIPOTINA BUNGENI
Wednesday, November 3, 2010
Sitayatambua matokeo ya urais - Dk. Slaa
Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, alisema wamekuwa wakifuatilia matokeo ya nchi nzima kwa umakini mkubwa na wamegundua kuna wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.
"Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na usalama wa taifa,"alisema Dk Slaa.
http://mwananchi.co.tz/
Tuesday, November 2, 2010
TAMKO LA DR SLAA
Dr. Wilbrod Slaa | Facebook
Sunday, October 31, 2010
NAMBA ZA MAKAO MAKUU CHADEMA
02: Mahinda: 0715-949019
03: Dady Igogo: 0713-616096
04: John Mnyika: 0754-694553
Fuatilia mwenendo kwa kugonga
Taarifa / Habari za Uchaguzi Mkuu - Upigaji Kura
State of the Nation Report 31st October 2010
www.wanabidii.net
Saturday, October 30, 2010
Mbinu zinazoweza Kutumika Kuiba Kura
Zifuatazo ni mbinu zitakazotumika kuiba kura kesho na zimeanza kutumika mkoani Shinyanga!!!
1.0 Mabalozi wote wa nyumba 10 na viongozi wa serekali za mitaa wanaitwa, wanapewa karatasi 2 za kupigia kura zilizo na vema tayari kwa mgombea wa kijani. Karatasi moja ni ya mume na moja ni ya mke wake. Kesho kila mmoja atakapoingia chumba cha kupiga kura atatakiwa achukue karatasi ingine (ya awali atakuwa kaificha). Akisha piga kura, atadumbukiza kwenye sanduku karatasi zote mbili. Hivyo mjumbe mmoja atapiga kura 2 na mkewe/mumewe kura 2. Jumla 4
Chadema wafanyeje kudhibiti hali hii??? Waweke daftari ambalo kila anaeingia anaandika namba kuanzia 1 hadi mtu wa mwisho. Baada ya kuhesabu kura, zitakazozidi zitakuwa ni zile zilizochakachuliwa!!!!!
Kama itawezekana, kila mpiga kura akaguliwe idadi ya karatasi atakazotumbukiza kwenye sanduku la kupigia kura. Else, wawakague watu kabla hawajawapa karatasi za kupigia kura, kujiridhisha kwamba, hawana vibomu/videsa vya ziada.
Its serious vikao vinaendelea kutimiza azma ya kupiga kura kwa design hiyo, japo maeneo yaliyolengwa ni yale yenye upinzani wa kweli. Mf. Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Mwanza na Mara. DSM inaogopwa sababu ya mwamko na kusambaa kwa taarifa sababu ya teknologia!!
2. Mbinu ya pili ni kutoa karatasi za kupigia kura zisizo na muhuri sambamba na zenye muhuri wa tume ya uchaguzi, ambapo karatasi zisizokuwa na muhuri zitachukuliwa kuwa batili kwa sababu hazijapigwa muhuri wa NEC.
Chadema wafanye nini hapa!!! Kila mtu anapofika kupiga kura, mawakala wapitie kila karatasi anayopewa mpiga kura kuhakikisha kwamba karatasi anayopewa mpiga kura ina muhuri sahihi.
3. Kuchakachua kura zikiwa njiani kwenda kwa msimamizi mkuu wa uchaguzi wa jimbo!!! Kwenye sheria za NEC na taratibu za internal control (Sarbanese Oxley Act), hapa kuna leakage. Hakuna anaeweza kuthibitisha kuto kuchakachuliwa kwa masanduku ya kura njiani kwakuwa mawakala hawana uwezo kusindikiza kura hizo!!!
Naomba kuwashirikisha mbinu hizo chafu kutokea Shinyanga!!! Hali si hali
Mungu awalinde na kuwabariki, awawezeshe nyote kupiga kura kwa umakini na kwa amani na kumpata Raisi wa kutuongoza kwa kipindi kijacho cha miaka mi tano mwenye hekima, akili, busara na hofu ya Mungu ndani yake!!!
Friday, October 29, 2010
FFU WAKIMBIZA WAFUASI WA CHADEMA IRINGA ,DK SLAA AKWAMA KUHUTUBIA
Hapa tupo gado akitua tu Dk Slaa tunaye"
Ila hawa wananchi mbona ni wengi sana itakuwaje hawawezi kufanya fujo"
Jamaa hakuna kulala hadi kieleweke twendeni uwanja mwingine kama huu hapa wamezuia"
Mzee salama hapa ama ?kwani kuna nini ni vita ?"
Hapa tupo kamili kwa lolote "kama wanazungumza
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoa wa Iringa wakiwa wamejipanga kwa lolote katika viwanja vya uwanja wa shule ya msingi Mlandege mjini Iringa ambako ulipangwa mkutano wa mwisho wa mgombea urais wa Chadema Dk Willibrod Slaa ambaye hata hivyo hakuweza kutua katika uwanja huo kama njia ya kukepa mbinu za CCM kutaka kuvuruga mkutano wake huo iwapo angetua katika uwanja huo leo asubuhi
Na Francis Godwin,Iringa
NGOMA nzito Iringa mgombea wa urais kupitia Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbroad Slaa amegonga mwamba kutaka kufanya mkutano wa kampeni bila kibali katika viwanja viwili tofauti mjini Iringa, baada ya Polisi wa kutuliza ghasia (FFU) kutanda katika viwanja vyote kuzuia mikutano hiyo kwa madai kwamba haina baraka za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Polisi waliokuwa na silaha kali na mabomu ya kutoa machozi, walifanikiwa kuwatawanya maelfu ya wafuasi wa chama hicho waliokuwa wakiendelea kukusanyika kwa wingi katika uwanja wa Mwembtogwa mjini hapa kuanzia saa mbili na nusu asubuhi.
Baada ya kutawanywa, wananchi hao walielekea katika uwanja wa Shule ya Msingi Mlandege walikotangaziwa kwamba Dk Slaa angetumia jukwaa la mgombea udiwani wa kata ya Kwakilosa, kuwasalimia wananchi wa jimbo la Iringa Mjini kabla hajaendelea na ziara yake ya mikutano ya kampeni katika majimbo ya Njombe Kaskazini, Njombe Magharibi na Songea Mjini.













