Showing posts with label ZAMANI. Show all posts
Showing posts with label ZAMANI. Show all posts

Thursday, September 2, 2010

KAMATI YA DR SLAA YABAINI SABABU YA RAIS KIKWETE KUENDELEA KUCHAFULIWA JINA ,YALIA NA MADAI YA WALIMU











Mwenyekiti wa kamati ya bunge hesabu za serikali za mitaa Dr Wilbrod Slaa mbunge wa Karatu akionyesha moja kati ya vitabu vilivyokaguliwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa









Katibu tawala wa mkoa wa Iringa Bi.Getrude Mpaka akifuatilia ukaguzi wa kamati ya Dr Slaa leo



Na Francis Godwin,Iringa

KAMATI ya bunge hesabu za serikali za mitaa inayoongozwa na mwenyekiti wake mbunge wa njimbo la Karatu (CHADEMA) Dr Wilbrod Peter Slaa imeziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha zinapeleka madai ya walimu na watumishi wengine katika ngazi zinazohusika badala ya kuishia ngazi za halmashauri jambo ambalo linasababisha Taifa kwenda vibaya ikiwa ni pamoja na Rais kuchafuliwa jina kwa uzembe wa halmashauri .

Akitoa agizo hilo katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo leo baada ya kukagua mahesabu ya halmashauri ya Manispaa ya Iringa ,mwenyekiti wa kamati hiyo Dr Slaa alisema kuwa imefika mahali Taifa limepelekwa pabaya kwa walimu kutangaza migomo ya kudai haki zao hali ambayo imekuwa ikimchafua jina Rais Jakaya Kikwete.

"Taifa limefika pabaya kutokana na hii migomo ya walimu na ukiangalia sana tunaofanya Rais kuchafuliwa jina ni sisi wenyewe hapa....toka sasa uhakiki wa madai ya watumishi ufanyike katika ngazi zote hapa hapa katika halmashauri husika... tungependa kila mmoja alipwe haki zake kama anavyoidai serikali"

Dr Slaa alisema kuwa kwa sasa sura iliyopo ni kuwa serikali imeshindwa kulipa madai ya watumishi wake wakiwemo walimu kutokana na miaka ya nyuma taratibu za kuhakiki madai ya walimu zilikuwa hazifanyiki hali iliyopelekea baadhi ya halmashauri kuwa na madai ya walimu zaidi ya milioni 500 ila hakuna sehemu yeyote katika vitabu inayoonyesha kuwa wanadaiwa na walimu.

Alisema kuwa kwa kuwa madai hayo ya walimu na watumishi wengine yamekuwa yakijulikana ngazi za chini pekee katika ngazi za juu kama Ikulu na ofisi ya waziri mkuu wamekuwa hawajui madai halisi ya walimu na watumishi wake kutokana na kutokuwepo kwa taratibu nzuri za utunzaji wa madai hayo kimaandishi.

Hivyo alisema kuanzia sasa lazima madai ya watumishi kama fedha za likizo ,matibabu na nyingine zinaonyesha kuwa serikali ilikuwa ikilipa miaka yote japo bado kuna madai hivyo alisema lazima kamati yake iweze kujua fedha hizo zilikuwa zikikwama wapi na kuanzia sasa lazima madai yote yahakikiwe na kutunza katika vitabu .

"Tunatambua kuwa fedha hizo zilikuwa zinatolewa na zinaonyesha kulipwa sasa haya madai ya watumishi sisi tunaendelea kufuatilia na kuona ni nani alichukua fedha hizo na kuzitumia kwa kazi gani na kuwa ikibainika hatua za kuchukuliwa kwa wahusika wa fedha hizo itajulikana"

Hata hivyo alisema kuwa hazina ndio ambao walikuwa wakiweka fedha hizo ambazo zilikuwa hazitumiki kulipwa wahusika hivyo ni wazi suala hilo Ikulu kuwa na taarifa juu ya suala hilo kupitia waziri mwenye dhamana japo hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na waziri mwenye dhamana katika kuijulisha Ikulu.

Kuhusiana na utendaji kazi wa serikali iliyopo madarakani chini ya Rais Kikwete kama inafanya kazi kama wananchi walivyotegemea ama lah Dr Slaa aligoma kulitolea ufafanuzi suala hilo kwa madai kuwa kwa sasa si wakati wake kwa kuwa yupo katika kazi hiyo maalum ambayo ametumwa na bunge hivyo atalitolea jibu siku nyingine.

Kamati hiyo ilifikia uamuzi huo wa kutoa agizo hilo baada ya ofisa elimu wa Manispaa ya Iringa Bi Mary Haule kushindwa kujua madia sahihi ya walimu wa shule za sekondari zaidi ya yale ya walimu wa shule za msingi ambayo ni zaidi ya shilingi milioni 50.

Pamoja na maagizo hayo pia kamati hiyo ya Dr Slaa ilisema kuwa katika madai ya walimu kuna madai ambayo waziri mkuu Bw Mizengo Pinda aliyatoa bungeni kuwa kuna hujuma zilifanyika katika uhakiki wa madai ya walimu ikiwa ni pamoja na wale waliotumwa kuifanya kazi hiyo kuongeza madai kwa lengo la wao pia kuweza kujipatia chochote kauli ambayo inapingwa vikali na halmashauri ya Manispaa ya Iringa kuwa hakuna jambo kama hilo .

Hivyo alihoji kuwa kama waziri mkuu alitoa kauli hiyo ndani ya bunge pasipo kuwa na uhakika nayo hivyo ni wazi waziri mkuu alilidanganya bunge ama Halmashauri ya manispaa ya Iringa inapingana na kauli hiyo ya waziri mkuu bungeni .

"Sasa kwa kuwa waziri mkuu aliitoa kauli hii bungeni na mbunge Stephen Galinoma wewe ni shahidi juu ya kauli hiyo na leo unashuhudia hapa Manispaa inavyopingwa ....sasa tunakwenda kuifanyia uchunguzi wa kina ikibainika kuwa waziri mkuu alikuwa mkweli tutashughulika na Manispaa ya Iringa haya yote hapa tunayaweka katika kumbukumbu zetu sasa tukimpata mkaguzi mkuu tutakabana koo"

Dr Slaa alisema kuwa lengo la kamati hiyo sio kwenda kuzilipua halmashauri za wilaya bali ni kuhakikisha fedha za serikali zinatumika kama zilivyopagwa na si vinginevyo ikiwa ni pamoja na vitabu kuandikwa katika usahihi zaidi.

Pia hatua ya tatu ya kamati hiyo ni kuhakikisha kuwa madiwani wenyewe wanasimamia vyema fedha za halmashauri rasilimali nyingine ili kamati hiyo ibaki na kazi ya kusimamia maeneo makubwa pekee.

Alisema kuwa matatizo makubwa ambayo wamepata kuyaona katika halmashauri ambazo kamati hiyo imepata kuzitembelea na kufanya ukaguzi ni pamoja na ugeuzaji wa matumizi ya fedha za miradi tofauti na ilivyokusudiwa na bunge.

Hata hivyo alisema kuwa inapobainika kuwa kuna ubadhilifu ambao umefanyika basi kumjulisha mthibiti na mkaguzi mkuu kufanya ukaguzi upya ili kama kuna mtu amehusika na wizi wa fedha za umma kuweza kuchukuliwa hatua na kuwa toka wamefika katika mkoa wa Iringa kuna wilaya moja pekee ambayo imebainika kuwa na makosa hayo ambayo hata hivyo hakuweza kuitaja wilaya hiyo japo hadi sasa wilaya zilizokaguliwa ni takribani zote ukiacha wilaya ya Kilolo ambayo ukaguzi wake kesho ijumaa.

Katika hatu nyingine kamati hiyo ya imetoa muda wa miezi miwili kwa uongozi wa Manispaa ya Iringa kukamilisha ujenzi wa nyumba za walimu ,vyoo na ununuzi wa madawati ya wanafunzi kama walivyoelekezwa na serikali kupitia fedha walizopewa kwa kazi hiyo.

Pia imejenga mashaka na matumizi ya fedha za umma yasiyo na chenji kuwa lazima katika suala hilo uongozi wa Manispaa ya Iringa umekuwa ukifanya kazi ya kublanzisha mahesabu ya fedha za miradi mezani na sio matumizi halisi ya fedha hizo.

Mbali ya mapungufu mbali mbali ambayo kamati hiyo imepata kubaini katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa bado imeweza kumpongeza mkurugenzi mtendaji wake Bi Terresia Mmbando wa wakuu wake wa idara kwa kazi nzuri ya kusimamia miradi ya serikali kwa kiwango kizuri na kuwa baadhi ya mambo ambayo wamepata kuyaona katika Halmashauri hiyo hayajaonwa sehemu nyingine.

MWISHO

Monday, August 30, 2010

Dr Slaa: I was cleared by Vatican

CHADEMA Union presidential candidate, Dr Wilbrod Slaa (center)  speaks to Daily News journalists on his party�s political agenda in Dar  es Salaam on Thursday
CHADEMA Union presidential candidate, Dr Wilbrod Slaa (center) speaks to Daily News journalists on his party�s political agenda in Dar es Salaam on Thursday
CHADEMA Union presidential candidate, Dr Willbrod Slaa, has defended his record as a Roman Catholic priest, saying he was not expelled. He said he requested to quit the clergy and concentrate in politics to fight poverty.

�The Vatican approved my request and I became a lay. I was not exorcised (expelled) as some of my political rivals may want people to believe," he said.

�I once co-ordinated multi-religious activities and made many friends from various religious denominations. I would like to serve the nation with diligence to stop misuse of available resources that are currently benefiting a few individuals,� Dr Slaa explained.

In an exclusive interview with the 'Daily News', Dr Slaa, claimed that "slow development pace�� in the country was due to lack of a clear national vision.

Dr Slaa urged the government to empower the people instead of over-dependency on foreign financial sources and importation of goods that could be made locally. Dr Slaa said research has shown that there was no country that has developed without serious investment in agriculture.

�Peasantry will get this country nowhere. Tanzania needs well planned agro-based industries under coherent strategies to ensure good returns,� he observed.

Clarifying on his desire to lead the people out of poverty, the presidential candidate said deprivation experienced in the country should not be there because the answer was creative minds and commitment.

He recalled the country�s focus on development under Mwalimu Julius Nyerere that was based on the people, land, good policies and leadership. He, however, blamed CCM and its predecessor, Tanu, for inability to fight poverty effectively for the last 50 years.

Dr Slaa said the Dar es Salaam Port and the country's mineral wealth could be the launching pad towards the nation's prosperity.

He, however, noted that services at the Dar es Salaam Port were poor and the government has demonstrably failed to ease congestion at the facility and the problem was also aggravated by poor railway network.

Chadema's presidential hopeful said in early 1980s Tanzania made tremendous strides towards manufacturing of cars at Nyumbu military workshop in Kibaha.

�I was delighted to meet my fellow countrymen in Ireland in 1981, who were sent by the government for training on manufacture of engines for home made trucks.

�The current Kigoma Regional Commissioner, Colonel (retired) Joseph Simbakalia, was one of the students. The project, which was a brilliant idea, was abandoned for no apparent reasons,� he lamented.

Dr Slaa said 50 years ago Japan was a poor country, but Tanzania now imports from there vehicles and machinery.

He criticised President Jakaya Kikwete for maintaining a huge cabinet. He said the United States with a population of over 300 million has only 14 ministers, while Britain has 20.

"Tanzania, with a population of 40 million has 40 ministers. As a result, three quarters of the country�s budget (11 trillion/-) is spent on running the government operations, instead of making serious investment in education, health, agriculture and other development programmes,� Dr Slaa explained.
daily news
2010-08-26

Tuesday, August 10, 2010

Tanzania: Opposition parties say CUF sidelined them

Tanzanian opposition political parties are crying foul over a decision by the Civic United Front (CUF) to shut them out from the official opposition in the Union Parliament.

CUF is one of the strong parties that posed a serious challenge to the ruling Chama cha Mapinduzi in the 2005 general elections, winning all 19 in parliamentary seats in Zanzibar but losing all the seats on the Mainland.

With 32 MPs in the House, including those in special categories, CUF has surpassed the number of constitutional requirement of MPs ratio – 30 – to empower it form a shadow cabinet. The party leadership announced a 22-member shadow cabinet on January 15.

But the other parties feel that CUF may not be able to use wisely its shadow-ministerial cabinet capabilities, "because the Islanders are not conversant with problems of the mainland – such as those in agriculture."

According to the MP for Karatu, Dr Wilbroad Slaa of Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), CUF already possesses a platform to air its views – in the Zanzibar House of Representatives – and it would have been wiser to it to leave the Union House to other parties "who could speak effectively on behalf of farmers engaged in coffee, cotton and tobacco production, which are not grown in Zanzibar.

Already, Chadema and United Democratic Party have written to the clerk of the National Assembly, asking him to intervene in the matter to conform to House rules.

But opposition leader Hamad Rashid Mohamed (CUF) said his party had taken the decision in accordance with the rules and regulations of the parliament.

Mr Mohamed he was surprised to see the parties raising the issue in the media and writing to the Speaker instead of seeking discussions with CUF first.

But Chadema chairman Freeman Mbowe said the move by CUF was "selfishness."

He said although CUF acted according to the House rules, it didn’t act in the national interests.

He expressed his hope that the rules, which were amended in 2000 to suit the political situation existing at the time, would be amended, so that the official opposition incorporates other parties.