Thursday, October 28, 2010
Tusikubali miaka mitano mingine ipotee
MWAKA 2005 nilikuwa miongoni mwa waliokuwa na shaka juu ya uteuzi wa Jakaya Kikwete kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Lakini baada ya ushindi wake wa kishindo, nilianza kuwa na imani naye, hasa kutokana na kauli zake za kuleta matumaini mapya.
Baada ya miaka 20 ya tawala za Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, nchi yetu ilihitaji mtu mwingine mwenye kuelewa kwa nini inazidi kuwa masikini wa kutupwa licha ya utajiri lukuki, mtu mwenye dhamira ya dhati ya kupambana na rushwa kwa vitendo, si maneno matupu (kwa mfano kutangaza kuwa anawafahamu wala rushwa ila anawapa muda wa kijirekebisha).
Awali, sikuamini kuwa Kikwete angeweza kuipatia Tanzania kiongozi wanayemuhitaji kwa vile hukuwa na rekodi hiyo. Licha ya kwamba urais si taaluma inayosomewa, lakini uongozi bora unaweza kubashiriwa kutokana na rekodi ya nyuma ya kiongozi mtarajiwa hasa kwa vile kabla ya kuwa rais wetu, Kikwete alikwisha kushika nyadhifa kadhaa lakini pasipo rekodi ya kujivunia.
Hofu yangu kuhusu Kikwete ilianza kuyeyuka baada ya kusikia kauli yake wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania ingekuwa kipaumbele chake kikuu pindi akichaguliwa, sambamba na kibwagizo cha Kasi Mpya, Nguvu Mpya na Ari Mpya.
Hotuba yake wakati anazindua Bunge, Dodoma, ilileta msisimko mpya, matumaini na imani kwamba hatimaye sasa tumepata kiongozi wa kuifikisha Tanzania inakopaswa kuelekea. Na hata alipotangaza baraza kubwa la mawaziri (lililojumuisha sura zenye utata), nado niliendelea kuwa na matumaini naye na kukubaliana na utetezi wake kwamba ili afanikiwe kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania angehitaji timu kubwa.
Matumaini yangu yalianza kufifia pale ulipotoa hotuba na kutamka kwamba “nawafahamu wala rushwa kwa majina lakini nawapa muda wa kujirekebisha”. Nilivunjwa moyo na kauli hiyo kwa sababu sijawahi kusikia mahala ambako rushwa ilikoma baada ya kiongozi kutoa muda kwa wala rushwa kujirekebisha. Na labda hapa niulize, hivi ile deadline aliyotoa mwaka 2006 kwa wala rushwa (aliodai kuwafahamu kwa majina) kujirekebisha bado haijaisha? Au ilikuwa indefinite deadline (isiyo na ukomo)?
Baadaye alirejea kauli kama hiyo alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alikotamka bayana kwamba anawafahamu wala rushwa katika sehemu hiyo na kilichobaki ni kuwaumbua tu (nadhani alimaanisha kilichobaki ni kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria). Inasikitisha kuona hadi leo hakuna aliyewajibishwa huku mamlaka husika zikirejesha mpira huo kwake kwa maelezo ya “waulizeni Ikulu maana wao ndio walidai wana orodha ya wala rushwa hapa”.
Tuwe wakweli, hivi kama aliahidi kuwasilisha majina ya mafisadi wa bandarini lakini hajatimiza ahadi hiyo maana yake ni nini? Je, tunastahili kuendelea naye kama ahadi alizotoa ni zisizotekelezwa? Kama anashindwa kutekeleza ahadi anazotoa mwenyewe pasipo kulazamishwa ataweza vipi kutekeleza mambo muhimu ambayo japo hajaahidi ni lazima ayatekeleze?
Ni kweli kwamba kiongozi wa nchi lazima afanye safari za kujitambulisha nje, lakini hicho hakiwezi kuwa ndiyo kipaumbele kwa kiongozi mwenye dhamira ya dhati ya kurekebisha hali ya nchi masikini kama yetu. Hata Barack Obama na David Cameron, viongozi wa mataifa tajiri kabisa duniani, wametuthibitishia kwamba kwenda nje ya nchi kujitambulisha si kipaumbele kwa kiongozi mpya.
Lakini pengine eneo tata zaidi ni la mafisadi. Kusita kupambana na kundi hili kumezua tafsiri nyingi katika vichwa vya watu, nyingi za hizo, hazimsemi vizuri Rais Kikwete kwa vile imejikita imani kwamba kuwaacha mafisadi waendelee ndiko kulikokwamisha “Maisha Bora kwa Kila Mtanzania”.
Ni siri ya wazi kuwa aliingia madarakani kwa nguvu na jitihada za wanamtandao, wengi wao wakiwa watu wenye rekodi zisizopendeza. Kosa kubwa alilofanya ni kutotumia nafasi yake kama Rais kuwadhibiti, matokeo yake wameishia kuutumia urais wake kujinufaisha wao wenyewe.
Matukio mawili ambayo hayatafutika katika historia ya Urais wa Kikwete ni ujambazi wa fedha za EPA na utapeli wa kampuni ya Richmond na ‘binamu’ yake Dowans.
Kuhusu suala la EPA, wengi wetu tunaamini kwamba bado kuna maswali mengi kuliko majibu. Japo inapendeza kuwaona baadhi ya watuhumiwa wakifikishwa mahakamani, bado haieleweki kwa nini hadi muda huu wamiliki wa kampuni iliyokwiba fedha nyingi zaidi, Kagoda, wameendelea kuhifadhiwa.
Ni kweli safari hii pana ushindani wa kutosha kwenye kiti cha urais. Ni kweli pia kwamba kama akipita, Kikwete atakuwa, kwa mujibu wa Katiba, akitumikia kwa muhula wake wa mwisho. Ninachojiuliza ni kama amemudu kufumbia uoza wote huu katika kipindi muhula wake wa kwanza huku akijua fika kuwa baada ya miaka mitano angepaswa kuomba tena ridhaa ya kupigiwa kura, hali itakuwaje katika muhula wake wa mwisho ambao hatahitaji tena kura zetu?
Barua-pepe:
epgc2@yahoo.co.uk
Monday, October 25, 2010
NUKUU ZA DR WP SLAA

- Monduli wanaishi maisha magumu.
- Tanzania bila CCM inawezekana, na kuendelea kukaa na CCM ni maafa makubwa.
- Kama ningesema uongo kuhusu ufisadi wa JK na waswaiba wake, mbona sichukuliwi hatua?
- Ukitukanwa, angalia, puuzia na uondoke. Ukipigwa kofi, mgeuzie na la pili...!
- Sipendi kwenda ikulu huku damu zikimwagwa, au kuwaacha watanzania wakiwa vilema kwa ajili yangu...!
- Nipo tayari kula mihogo ikulu, ili mtoto wa tanzania asome...!
- Siendi kuwa raisi wa Afrika Mashariki, bali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...!
- Kodi ya saruji kutoka Tanzania ni 18%, Kenya 15% na Uganda 16%....! Eti ndio makubaliano yaliyowekeana kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki...!
- Ninazo nyaraka kuwa serikali ya Tanzania imefanya partial payments huko Canada kwa ajili ya mabango ya CCM...!
- Sikatai kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini lazima tufanye maandalizi kuwapatia watanzania elimu itakayowawezesha kuingia kwenye ushindani...!
Ewe Mpiga Kura Nakusihi Usipoteze Nafasi Hii Adimu Jumapili Ijayo
Sunday, October 24, 2010
Ni maafa kuichagua CCM – Dk. Slaa
Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye mdahalo uliokuwa ukirushwa moja kwa moja na Televisheni ya ITV, ambapo alisema kuwa chama hicho kimewafanya Watanzania wawe maskini, kimeendekeza ufisadi na kimeshindwa kutumia rasilimali za nchi kwa manufaa ya walio wengi.
Dk. Slaa alisema hakuna sababu ya wananchi kuwa waoga wa kuwachagua viongozi wapya kutoka upinzani, kwa kuwa hakuna chuo kinachofundisha urais bali kinachoangaliwa ni busara, hekima, kuwashirikisha wananchi na kuweka mbele masilahi ya taifa.
“Kuichagua CCM ni kutafuta maafa zaidi ya haya tuliyonayo, tuache woga wa kuwachagua viongozi wapya, bila CCM Tanzania inawezekana, hata Mwalimu Nyerere alikuwa mpya wakati huo, lakini tulimpa uongozi kwa sababu tulimuamini atatuongoza vizuri,” alisema.
Dk. Slaa alimtupia lawama Rais Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM kwa vijana wa chama hicho kufanya fujo kwenye mikutano ya kampeni ya wagombea wa CHADEMA.
Alisema vijana hao wa CCM maarufu kama Green Guard wamekuwa wakipata mafunzo ya kijeshi, kinyume cha Katiba na sheria za nchi na baadaye huenda kufanya vurugu katika mikutano ya CHADEMA pasipo askari kuwachukulia hatua zozote.
Alisema Rais Kikwete ana jukumu kubwa la kukomesha kundi hilo la vijana kwa sababu yeye ni Amiri Jeshi Mkuu na Mwenyekiti wa CCM, ambayo inawalea na kuwapa mafunzo vijana hao.
Dk. Slaa alisema wananchi wasidanganywe kuwa vyama vya upinzani vinaweza kuyumbisha au kuleta machafuko hapa nchini, bali hali hiyo itaweza kuletwa na chama tawala, ambacho kinakuwa kimeshikilia serikali na vyombo vya ulinzi na usalama.
“Mimi sitaki kwenda Ikulu huku damu ya wananchi wangu ikiwa imemwagika au wengine wakiwa na vilema, nataka niende Ikulu kwa amani na furaha ya wananchi wangu walioshiriki kwenye kampeni na uchaguzi uliokuwa na mazingira bora,” alisema Dk. Slaa
Ufisadi
Alibainisha Rais Kikwete na CCM, wameshindwa kuwashughulikia mafisadi kwa sababu wametokana na zao hilo, kwani hata fedha zilizotumika kumuingiza Ikulu zilipatika kwa wizi uliofanyika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).
Alisema ana ushahidi wa nyaraka wa Kampuni ya Kagoda ambayo ilikwapua zaidi ya sh bilioni 40 na benki zilizohusika katika malipo hayo zinajulikana, lakini mpaka sasa wahusika hawajafikishwa mahakamani.
Alibainisha kuwa Rais Kikwete anahusika na wizi huo, ndiyo maana mpaka sasa hajaweza kumfikisha mahakamani yeye (Dk. Slaa) ambaye alitaja hadharani orodha ya watuhumiwa wa ufisadi akiwamo Rais Kikwete.
“Ninachokisema mimi huwa nina uhakika nacho, kwa sababu nyaraka ninakuwa nazo, mpaka leo hii nadunda mitaani kwa sababu najua Kikwete hawezi kunifikisha mahakamani,” alisema.
Alibainisha kuwa Rais Kikwete hana ubavu wa kupambana na ufisadi kwa sababu hata wale wanaotuhumiwa kushiriki vitendo hivyo huku wengine kesi zao zikiwa mahakamani amewanadi katika mikutano yake ya kampeni kwa kuwaeleza wananchi wawachague kwa madai ni wachapa kazi.
Alisema ni jambo la kusikitisha serikali iliyopo madarakani inabariki wizi wa sh bilioni 155 kupitia Kampuni ya Meremeta ambayo inadaiwa kuwa ilikuwa ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Alisema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisimama bungeni kutetea wizi huo kuwa fedha hizo zilitumika kwa masuala ya jeshi, ilhali jambo hilo si la kweli, bali zililiwa na wajanja wachache, ambapo fedha hizo zilipitia benki moja ya Afrika Kusini.
Katika hatua nyingine, Dk. Slaa alisema elimu bure kwa Watanzania ni jambo linalowezekana, kwa sababu serikali inazo rasilimali za kutosha lakini kutokana na kutozigawanya inavyotakiwa, jambo hilo limeshindikana.
Alisema Tanzania kamwe haitaweza kujikwamua katika lindi la umaskini kama wananchi wake hawatapata elimu bora kama wanayoipata watoto wa vigogo au wa nchi za Uganda na Kenya.
Alibainisha kuwa hivi sasa hapa nchini kuna matabaka matatu katika sekta ya elimu, ambapo tabaka la kwanza lina uwezo wa kuwasomesha watoto wao nje ya nchi huku lile la pili likiweza kuwasomesha katika shule za kata zilizojengwa hivi sasa.
Tabaka la tatu ni lile ambalo halina uwezo wa kusomesha watoto wao hata katika shule za kata.
Mikataba ya madini
Alisema iwapo atapewa fursa ya kuwa rais ataipitia mikataba yote ya madini na kuirekebisha, ili iweze kuwanufaisha zaidi wananchi kama ilivyo kwa wenzao wa Botswana.
Aliongeza kuwa alikwisha kufanya mazungumzo na watu kutoka nchi za nje ambao walimwambia ni jambo la ajabu kwa Tanzania kupata mrabaha wa asilimia tatu katika sekta ya madini wakati wawekezaji wakipata asilimia 97.
Mabadiliko ya Katiba
Alibainisha kuwa katika miaka yake mitano ya mwanzo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali atahakikisha anaifanyia mabadiliko Katiba ya nchi ili kumpunguzia madaraka rais, ambaye amekuwa akiteua watendaji wengi.
Alisema haoni kazi za manaibu mawaziri, hivyo akiingia madarakani atahakikisha hawateuwi na fedha zilizokuwa zikitumika kuwahudumia zitapelekwa kusaidia ujenzi wa shule, zahanati, barabara na huduma nyingine za kijamii.
Utegemezi wa bajeti
Alisema serikali yake itajitegemea katika matumizi ya kawaida, ikiwemo kulipana mishahara na shughuli nyingine, lakini itaendelea kushirikiana na wafadhili na wahisani ili wasaidie miradi mikubwa.
Aliongeza kuwa serikali yake haitakuwa na kisasi na mtu yeyote, lakini pia haitakuwa na huruma na wanaotumia rasilimali za taifa kwa masilahi binafsi.
Masilahi ya wafanyakazi, wazee
Alisema ataboresha masilahi ya wafanyakazi kwa kupandisha mishahara kulinga na taratibu watakazoziweka lakini pia atashusha gharama za sementi (saruji) na bati, ili wafanyakazi waweze kujenga nyumba.
Kuhusu suala la wazee, alisema ataanzisha utaratibu wa kutoa pensheni bila kujali kama walifanya kazi au la, kwani jambo hilo lilifanyiwa utafiti na watu wa Help Age International Tanzania na likaonekana linawezekana.
Kukubali matokeo ya uchaguzi
Alisema atawaandaa wanachama wake kukubali matokeo iwapo mazingira ya kufanyika kwa uchaguzi yatakuwa huru na haki lakini hawezi kufanya hivyo ikiwa hujuma zitafanyika.
Alisema kocha yeyote ambaye atasema kabla ya kuanza kwa mchezo kuwa timu yake itatoka sare au atayakubali matokeo, atakuwa na matatizo, kwani inawezekana akiingia uwanjani refarii akaipendelea timu pinzani.
Kulinda kura
Alisema jukumu kubwa la kulinda kura ni la mwananchi mwenyewe, kwa sababu kura yake ndiyo maji, barabara na huduma nyinginezo, hivyo ni vema kila mmoja akazilinda kama wakazi wa Kigoma, Karatu, Mpanda Kati, Moshi Mjini na kwingineko.
Aionya NEC
Alisema anashangazwa na majibu ya Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu Kiravu, kuwa yeye (Slaa) ni muongo, kwa kumpa tuhuma za kuwapo kwa kontena la kura lililokamatwa Tunduma likiwa na kura za mgombea wa CCM.
Alisema alichopaswa kufanya Kiravu ni uchunguzi, si kukurupuka, lakini ni vema akaelewa kuwa Watanzania wa mwaka 2000 si wa sasa, mambo yamebadilika
Alibainisha kuwa Kiravu alipaswa awaeleze wananchi imekuwaje karatasi hizo zichapwe nje ya nchi wakati Waziri anayeshughulikia masuala ya Uratibu na Bunge, Philip Marmo, alisema zitachapishwa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, lakini hivi sasa zinachapishwa Uingereza.
Dk Slaa: Jukumu la amani si la wapinzani pekee
MGOMBEA wa urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema kuwa jukumu la kuhakikisha amani inatawala wakati wa uchaguzi mkuu si la wapinzani pekee, bali vyama vyote vinavyoshiriki.
Dk Slaa alikuwa akizungumzia kauli za mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete ambaye amekuwa akidai kuwa kuna vyama vinahubiri vurugu na uchochezi na kuwataka viongozi wa vyama hivyo kuacha na badala yake wanadi sera zao.
Jana, Dk Slaa aligeuka mbogo na kusema kuwa damu imeshaanza kumwagiza kwenye baadhi ya maeneo kutokana na vurugu za CCM, lakini hadi sasa Kikwete amekuwa kimya.
“Jakaya Kikwete hatapona katika hili... damu za Watanzania zimeanza kumwagika Mwanza, Musoma, Hai, Mbeya, Iringa, Arusha na maeneo mengine na yeye yupo kimya kwa kuwa wanaomwaga ni CCM,” alisema Dk Slaa.
Alisema tangu ameanza ziara amejionea jinsi Watanzania wengi walivyokubali mabadiliko hivyo, kama ikitokea kura zao zikaibwa, wa kulaumiwa haitakuwa Chadema wala wapinzani, bali ni CCM.
“Jukumu la amani halipo kwa wapinzani pekee... tumeona damu inamwagika maeneo mengi na Kikwete yupo kimya; sasa naonya kama kweli hali hii ikiendelea na ajue amani inaweza kuondoka kwa kuwa haki ya wananchi inaporwa,” alisema Dk Slaa.
Dk Slaa pia alisema kuwa hagombei urais kwa lengo la kuwa afisa miradi anayeahidi kujenga barabara na zahanati, bali anataka kuongoza nchi.
Mbunge huyo wa zamani wa Karatu, ambaye amekuwa akieleza makombora yake kwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete, aliuambia mkutano wa hadhara uliofurika kwenye Uwanja wa Bwawani, Karatu mkoani Arusha kuwa anataka kuwapatia Watanzania ukombozi wa kweli wa maisha yao.
“Mimi si afisa miradi au mipango wa kusema mkinichagua nitajenga zahanati, nitajenga, barabara nitanunua Bajaj," alisema Dk Slaa akionekana kumlenga mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete ambaye amekuwa akitoa ahadi za kujenga barabara, hospitali na kununua pikipiki za magurudumu matatu ili zitumike kubeba wagonjwa.
"Hiyo siyo kazi yangu (rais) kwa kuwa yote hayo yapo katika mipango ya serikali na mgombea yoyote atakayeshinda atatekeleza,” alisema Dk Slaa.
Alisema ahadi nyingi ambazo zinatolewa sasa na Kikwete tayari zilipangwa na serikali na Bunge lililopita hivyo kuahidi kuzitekeleza sasa ni kuwadanganya wananchi.
“Mpango wa ununuzi wa meli mpya kwenye Ziwa Victoria ulikuwepo, miradi hiyo ya Bajaj ilikuwepo na hata hili la elimu ya sekondari si mpango wa CCM uliigwa na serikali,” alisema Dk Slaa.
Katibu huyo mkuu wa Chadema aliwataka wananchi kupuuza matokeo ya tafiti za kura zilizofanywa na Redet akisema kuwa ukweli halisi unajulikana na utaonekana siku ya kupiga kura Oktoba 31.
Katika mkutano huo. Dk Slaa aliwaomba wakazi wa Karatu kumchagua mgombea wa ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Israel Natse na wagombea wote wa udiwani huku wakihakikisha wanalinda kura zao.
“Mwaka 2005 waliniibia kura na nyie mnajua na hata mahakama ilikiri hivyo naomba mwaka huu mlinde kura wasiibe tena,” alisema Dk Slaa.
Mgombea huyo kesho atakuwa na mikutano kwenye miji ya Monduli mkoani Arusha, Hai, Moshi na mkoani Tanga.
Monday, October 18, 2010
PEMBETATU YA USHINDI: KUELEKEA MABADILIKO
Njia ya Dr. Slaa kuingia Ikulu inapitia moja kwa moja katika migongo na mabega ya Zitto Kabwe na Freeman Mbowe. Na pamoja nayo inapitia katika pembetatu ya watu hawa watatu kuongoza shambulizi la mwisho katika wiki hizi mbili zilizosalia kabla ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010.
Kama kuna kiongozi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema anayeamini kuwa ipo nafasi nyingine ya kugombania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kushinda nje ya nafasi hii ya 2010 basi mtu huyo anajidanganya. Kama wapo wanachama na mashabiki ambao wanaamini kuwa wakati wa kugombea Urais na kushinda siyo sasa na hivyo wasubiri hadi 2015 au 2010 watu hao vile vile wanajizuga wao wenyewe. Endapo viongozi, wanachama na mashabiki wa Chama hicho maarufu cha upinzani nchini hawatafanya yote wanayopaswa na wanayoweza kufanya katika wiki hizi mbili za mwisho za kampeni basi ndoto ya kuupata Urais itatoweka kama umande wa alfajiri.
Nalazimika kuandika hili kama kuwatia shime wale wote ambao wanataka kweli mabadiliko nchini kupitia chama hicho kuondoa vizuizi vyote vya kihisia na kiakili na kutumia nafasi hii ya kihistoria kuweza kuigombania ipasavyo nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano.
Mkakati wowote wa kutaka kupata wabunge wengi zaidi na siyo kupata Urais wa Jamhuri ya Muungano ni mkakati uliokubali nafasi ya kudumu ya upinzani. Kama viongozi na mashabiki wa Chadema wanapita na kuhamisha watu wawachague wabunge ili kuwe na wabunge zaidi Bungeni ili kwa kufanya hivyo waanze kusikilizwa zaidi na CCM basi watu hao wanakuwa wamekubali nafasi ya upinzani na hawako tayari kuwa watawala. Mkakati wa kupata wabunge wengi ni mkakati mzuri isipokuwa pale tu unapoendana na lengo zima la kutaka nafasi ya urais vile vile.
Ninasema hili kwa sababu kuwa na wabunge wengi wenye kuzungumza zaidi na wenye kufumua mambo mengi Bungeni wakati bado Rais ni wa chama tawala ni kuongeza kelele zaidi Bungeni na “wapiganaji” zaidi lakini ikiangaliwa kwa ukaribu itaonekana ni kujaribu kuwa na miaka mitano iliyopita tena Bungeni. Namna pekee ya kuwa na wabunge wengi bila ya kuwa na Rais inaweza kufaa kama lengo ni kuwa na wingi zaidi ya wabunge kuliko CCM au chama kingine chochote na hivyo kuwa katika uwezekano wa kumtoa Waziri Mkuu, japo siyo lazima kwani kunaweza kuwa na mbunge mwingine anayeonekana kuungwa mkono na wabunge wengi.
Lakini kama lengo ni kuwa na wabunge wengi tu ili kuongeza idadi na hivyo kuwa na “sauti zaidi” basi lengo hili ni zuri kwa kiasi fulani tu na ni kiasi kile kwamba wingi mkubwa wa wabunge wa CCM (super majority) ukiondolewa basi CCM haitoweza tena kubadili Katiba kama ipendavyo au kupitisha mijadala kirahisi rahisi. Katika mazingira hayo vyama vilivyoko Bungeni vitalazimika kujadiliana na kukubaliana na kujifunza kuachiliana vile vile ili mambo yaende. Hili likifanikiwa basi ni jambo kubwa na jema.
Hata hivyo, chama cha siasa chenye kuona tuzo wanayostahili kwa kazi ngumu ni Bunge zaidi na Ikulu wako tayari mwingine aendelee kuishikilia kinajiwekea kizuizi kisicho cha lazima. Chama cha siasa lengo lake ni kuchukua Bunge na Urais ili kwa kufanya hivyo kiweze chenyewe kutekeleza ajenda zake na ilani yake ya uchaguzi. CCM inapopita kuomba kura na kupiga kampeni hakimpigii kampeni Rais tu bali pamoja na wabunge na madiwani wake. Ni katika kutambua hili CCM inaweza kuwa na uhakika wa kutekeleza sera zake na ilani yake. Vivyo hivyo Chadema kama kinajiamini kuwa kimekomaa na kiko tayari kushika madaraka ya juu kabisa ya utawala ni lazima viongozi wake wote, wanachama na mashabiki wake wawe na lengo hilo wazi kabisa katika fikra zao yaani ni lazima wagombea wa ubunge wa Chadema wachaguliwe, wagombea wa Udiwani nao wachaguliwe na yule wa Urais naye achaguliwe. Kusisitiza kuchagua wabunge na madiwani tu bila kusisitiza kuchaguliwa kwa Rais ili chama kiunde serikali siyo mkakati mzuri.
Katika kufikia lengo hilo kwa upande wa Chadema ninaamin nafasi ya watu hawa wawili haiwezi kukwepeka. Mgombea wa Chadema na mbunge maarufu Bw. Zitto Kabwe ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu ana nafasi ya pekee kumletea Dr. Slaa ushindi. Ukiondoa tofauti zao za ndani ya chama na migongano ambayo kama nilivyowahi kusema huko nyuma ni muhimu kwa afya ya Chama Zitto amekomaa zaidi kisiasa na kwa yeyote ambaye amemfuatilia kwenye kampeni zake na za kuwanadi wagombea wengine kwa hakika amevutiwa na utayari wake. Hata hivyo, bado Zitto hajajionesha kuwa anampigia Dr. Slaa debe ili achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zitto ni lazima atoke na aseme wazi na pasipo utata kuwa anamuunga mkono Dr. Slaa na anamuombea kura katika kila mikutano yake. Asionekane kusita hata kidogo.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema Bw. Freeman Mbowe naye ana nafasi ya pekee katika kumletea ushindi wa kihistoria Dr. Slaa. Hadi hivi sasa ameshafanya makosa makubwa mawili ya kimkakati na ninaamini historia itamhukumu vibaya kama atafanya kosa la tatu na la nne. Kosa la kwanza ni kuamua kugombea Hai tena kitu ambacho kimemlazimu kutumia muda mrefu jimboni humo na kama nilivyosema kwenye Chadema: Kutoka Hapa mpaka Kule CCM wataweka msukumo mkubwa Hai ili kuhakikisha Mbowe arudi Dar au haingii kwenye kampeni za Kitaifa za kumnadi Dr. Slaa. Hili hadi hivi sasa limefanikiwa na asipoweza kujinasua basi atakigharimu sana chama chake kitaifa. Kosa la pili linatokana na hilo la kwanza, kama habari kuwa “Mbowe ana wakati mgumu Hai” zina ukweli kutokana na vyanzo vyangu mbalimbali ninaamini wakati huu “mgumu” hautaisha hadi siku ya kura. Hivyo, Mbowe imemlazimu kufuatilia sana kampeni yake yeye mwenyewe kule Hai na kutokuwa msaada mkubwa kwenye kampeni ya kitaifa na CCM wataendelea kuweka presha zaidi Hai ili kuhakikisha kuwa wanamuangusha. Kumuangusha mtu anayejinadi kuwa ni Kamanda kwenye uwanja wake wa nyumbani itakuwa ni pigo kubwa la binafsi kwa Mbowe.
Lakini pamoja na ukweli wa hali halisi inayoendelea huko Hai ambako katika kampeni za CCM kumetazamwa kama “special case” Mbowe ni lazima anasuke. Ni lazima awe tayari kuitoa kafara Hai ili Dr. Slaa ashinde. Yeye naye anahitajika kuonekana katika mikutano nje ya Hai na sehemu nyingine (kama anvyofanya Zitto sasa) kuanza kuwapigia debe wagombea wengine wa Ubunge na Udiwani pamoja na Dr. Slaa. Hili ni kweli kwani kama kabla ya wiki mbili za uchaguzi Mbowe hana uhakika wa ushindi Hai basi ushindi kwake utakuwa ni mgumu mno. Kamanda mzuri vitani ni yule anayejua ni kita kipi cha kupigana na kipi cha kukiacha. Hivyo, kuna wakati wa vita basi majemedari huamua kupigana katika maeneo mbalimbali lakini maadui zao wakati mwingine hutengeneza kita mahali ili kuwavuta wapiganaji huko huku wao wenyewe wanaendeleza mapambano kwingine. CCM ilijua Mbowe atagombea Hai na walihakikisha kuwa akija hata pingamizi lolote hawaweki lakini watahakikisha wanamtoa katika mtandao wa kampeni ya Dr. Slaa. Bahati mbaya Mbowe ameingia kwenye mtego huu na ni vigumu kujinasua bila kwanza kuwa tayari kutoa kafara Jimbo la Hai. Mimi ninaamini kabisa Mbowe jimbo la Hai atashinda bila hata ya kutumia nguvu nyingi kwani anachokiona kuwa ni presha ya CCM si lolote zaidi ya kile kinachoitwa “drawing the enemy” yaani “kumvuta adui aje”. Mbowe apumzike siasa za Hai na mara moja aende maeneo mengine ya nchi kuwauza wagombea wa Chadema na kumwombea Dr. Slaa kura zaidi.
Ndugu zangu, ushindi wa uchaguzi mkubwa wa kisiasa kwenye nchi mara nyingi hauamuliwi siku ya kwanza ya kujiandikisha kupiga kura au wiki za mwanzo za kampeni. Utafiki wa kisayansi ya siasa unaonesha kuwa wapiga kura wengi hufanya uamuzi wao wiki mbili za mwisho za uchaguzi. Hadi hivi sasa matokeo yote ya kura za maoni yatakuwa na nguvu katika wiki hizi mbili zijazo na siyo yale ya Septemba au Machi. Wiki hizi mbili za mwisho ndizo zitaamua nani anashinda. Ni kutokana na ukweli huo ninaamini kile ambacho Chadema watafanya wiki hizi mbili ndicho hasa kitaamua kama wanaanguka au wanasimama.
Nimesema kuwa kile ambacho “chadema watafanya”. Maanake ni kwamba, ushindi wa Dr. Slaa na wagombea ubunge na udiwani wa Chadema hautaletwa na CCM, TLP au CUF. Hautaletwa na vyombo vya habari na hautaletwa na watu wanaokuja kuwashangilia kwenye mikutano; utaletwa na Chadema wenyewe. Ushindi hautaletwa kama zawadi bali unatakiwa kutafutwa, kupatikana na kuchukuliwa kama lulu iliyopotea. Na ushindi huo hautazuiliwa na CCM.
Kwa uhakika mkubwa naweza kusema kwamba hakuna jambo lolote ambalo CCM na makada wake na hata serikali yake wanaweza kufanya ambalo litaamua kama Chadema inashinda au la. Siamini kabisa kabisa kama Rais Kikwete, Bw. Kinana na Bw. Makamba wanaweza kufanya lolote kuzuia ushindi wa Chadema kama Chadema wanautaka na wanaenda kuuchukua. Kitu pekee CCM inaweza kufanya ni kupunguza makali yake.
Hii ina maana ya kwamba kushindwa au kushinda kwa Chadema kumo mikononi mwao wao peke yao kwa asilimia 1000. Mengine yote yatafuata yenyewe. Lakini ushindi huo utategemea moja kwa moja Pembetatu ya Ushindi (Triangle of Victory) yaani Dr.
Slaa, Freeman Mbowe na Zitto Kabwe. Hawa watatu katika mabega yao wamejibebesha mzigo wa kuiletea Chadema ushindi; naam ule “ushindi wa heshima” kama anavyoita Bw. Kabwe.
Hadi hivi sasa nikiri kuwa Dr. Slaa amefanya zaidi ya vile ambavyo wengi tulitarajia. Kwa kila kipimo Dr. Slaa amejionesha kuwa ni mwanasiasa aliyekomaa na ambaye anaweza kuhimili mikiki ya uchaguzi. Binafsi nikiri kuwa kwa mwanasiasa ambaye ameshambuliwa hadharani maisha yake binafsi (kuacha upadre), maisha yake ya chumbani (kuwa na Bi. Josephine) na kuhimili maumivu ya mkono uliovunjika na kukampeni na vijana wengi akihutubia mikutano mingi kila siku ni wazi kuwa Dr. Slaa ameshajiweka kwenye kaliba nyingine kabisa na kama mgombea sidhani kama wangeweza kumwomba afanye lolote zaidi. Katika wiki hizi mbili za mwisho ni hawa wengine ndio sasa wanaitwa na historia pamoja na wagombea wengine ambao bado wametingwa katika majimbo yao kufanya kile ambacho Umsolopagas alikiita ni “pigo takatifu”.
Ndugu zangu, kama ingekuwa ni ulingoni basi hii ni raundi ya kumi katika pambano la raundi kumi na mbili. Tayari tumeona CCM ikirusha masumbwi yake na Chadema wakirudisha. Hadi hivi sasa watazamaji wanaamini Chadema imeshenda kwa pointi. Na watu wanaamini kuwa ikiendelea hivi hivi katika raundi zilizobakia basi watashinda kwa pointi nyingi tu. Na kama viongozi wa Chadema wataendelea na mbinu zile zile na hotuba zile zile wakiamini kuwa zitawapa ushindi wajiandae kwa mshangao.
Katika mapambano ya ngumi usimdharau bondia mzoefu. CCM ni chama cha siasa na kinajua jinsi ya kufanya siasa (how to do politics). Chadema ni chama cha siasa lakini bado hakijamudu sana jinsi ya kufanya siasa. Ninaamini sasa hivi CCM inachofanya ni kumkumbatia tu huyu bondia mwingine huku ikimvuta muda kumfikisha raundi ya mwisho ambapo itaangusha ngumi kama mvua ili kuhakikisha inamtoa kwa KO. Hivyo, hata kama mnaiona CCM imeshikilia kamba inahema au inaruka ruka kwa mbali msidhani imeshashindwa. CCM bado ni chama chenye nguvu na chenye mbinu za hali ya juu za kisiasa. Yeyote anayewadharau ati kwa vile Chadema inaonekana kushinda asije kujikuta anapigwa na butwaa. Kwani ni mara ngapi tumewahi kuwaona mabondia wanaoongoza mapambano lakini dakika za mwisho wanajikuta hawana ubavu hata wa kurusha ngumi ya ushindi?
Chadema, mashabiki wake na wagombea wake wote wanazo wiki mbili kufikiria ni ngumi ipi na ilenge wapi ili kuhakikisha kuwa CCM ikinyukwa inapata kizunguzungu na kuanza kuona nyota za fedha za EPA zikiyeyuka hewani! Lakini kujiamini kuwa ati Chadema itashinda kwa vile watu wanaishangilia ni kutokujua siasa. Ni matumaini yangu Chadema na viongozi wake watabadilisha mbinu zao za vita, watamshangaza adui na zaidi sana watafanya kile ambacho CCM hata kuwaza kuwa Chadema inaweza kufanya haijawaza. Lakini wakiendelea na mtindo ule ule na mbinu zile zile ambazo CCM inazijua kwa muda mrefu, tusije kujikuta tunashangazwa na kuaza kulia “CCM wameiba kura”. CCM haina haja ya kuiba kura ili ishinde, CCM inahitaji kuchezea wapiga kura kisiasa tu ili ishinde, na nani atawalaumu hiyo ndiyo “siasa”. Chadema wajifunze kujua jinsi ya kufanya siasa dakika hizi za mwisho vinginevyo wasije kujikuta dakika za mwisho wanapatwa kwikwi.
Tayari wana ujumbe wenye kuungwa mkono na watu wengi, tayari wana wagombea viongozi wenye kukubalika na tayari wameshachochea nyoyo za Watanzania kutamani kitu tofauti nje ya CCM. Ndani ya miaka mitano wameikuta ardhi kavu, wameilowesha, wamepende mbegu, mazao yamekua na sasa wakati wa mavuno, Chadema ihakikishe inavuna kiuhakika. Isiionee huruma CCM, viongozi wake wasimuonee huruma Kikwete na CCM bali watoe na wawe tayari kutumia mbinu zote za kisiasa kwenda kupata ushindi. Isije baadaye watu wakaanza kusema “kwanini hamkufanya vile au hivi” na wao wakaanza kutafuta visingizio vya kuhalalisha kushindwa kwao, visingizio ambavyo vitakuwa ni vile vya nje ya chama. Ninaamini kuna mambo kama matatu au manne ambayo Chadema wakiamua kweli kuyafanya siyo tu kwamba watashika hatamu ya uongozi lakini wataonekana kwa haki kabisa wamestahili kufanya hivyo na hakuna mtu atakayeweza kuamua vinginevyo.
Ninachosema ni kuwa Chadema ushindi ni wao kupoteza na Urais ni wao kuukosa. CCM inaombea tu Chadema wasifanye wanachopaswa. Hata ningekuwa mimi, ningeombea Chadema wasipigane kama mashujaa siku ya ushindi. Kwani harufu ya “siku ya ushindi” inanukia kwa mbali. Chadema watafanya kweli? Tuna wiki mbili kuona kwani wananchi wanaweza kufanya yote wanayotakiwa kufanya lakini mwisho wa siku Pembetatu ya Ushindi itasimama pamoja majukwaani?
Naamini tunapoanza kuelekea katika malango ya CCM kuyatikisha na hata kuyafungua kwa nguvu ili hewa mpya ya mabadiliko ipite, hakuna njia nyingine isipokuwa kuona makamanda wa mapambano haya wakinyanyua bendera juu na wakipiga yowe la “ushindi” bila kuona huruma, woga, haya au kusita. Nje ya hapo ushindi wa CCM hautaepukika.
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Saturday, October 16, 2010
Who amongst us fits into the shoes of Nyerere?
ON Thursday was the eleventh anniversary of the death of the Father of this Nation, Founder President Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Going by African tradition, one does not mark the death of a dear one by any festivities such as going on holiday!
It is always a somber and not festive moment. For African animists, they have their own mode of prayers, normally invoking on the spirits of the ancestors of the deceased to either keep well the departed loved one or invoking on them, including the spirit of the departed one, to bless those left behind.
As for the religious ones of today’s major religions, they either say special mass for the deceased or invoke special prayers - du’a or hitma. One is not sure how we marked the 11th anniversary of the departure of the Father of this Nation yesterday, which was a public holiday.
Coming into the midst of campaigns towards elections, the anniversary was certainly low key with only presentations by activists at the University of Dar es Salaam and publishing of bumper editions by the major dailies like this newspaper, which published special editions. But as I have had occasion to point out in this column in the past, it may be appropriate in the future to commemorate Mwalimu’s birthday and death anniversaries separately in compliance with African culture and tradition.
So we could have April 13th every year to celebrate posthumously his birthday anniversary and October 14th his death anniversary. For Mwalimu Nyerere deserves such commemoration because he lives with us and indeed, is a living comprehensive textbook in terms of personal conduct, leadership and vision for this country and the wider world. For today, let us address the question constituting the theme of this subject: Who amongst us fits into his shoes?
Well, if I have included you, the reader of these lines into trying his shoes to see whether we fit into them is for a good reason. As everybody may agree, Nyerere offers a good example for emulation, even by ordinary individuals if one was to take his personal conduct at private level in terms of humility and integrity.
These virtues of humility, especially integrity, makes one stand tall and distinguishes one from others in the pack, isn’t it? But these two virtues can make a huge difference, wouldn’t they, if they are seen in a leader of a nation, especially of poor people like us. Those who saw him in his lifetime may remember that Mwalimu always scorned pomposity in his life style.
He could have opted for top of the market western suits especially tailored for him directly from France or Italy. But he didn’t. He preferred simple suits, easily affordable, the type of suits we called those days ‘Kaunda’ or ‘Chou En Lai’ suits. Such was his life-style – simplicity couched in humility.
A graduate of Edinburgh University, where he earned his Masters Degree, many a reputable universities across the globe had honoured him with honorary doctorate degrees. When people began addressing him, ‘Dr Nyerere’, Nyerere cut them short by these words: “….Oh! No! I will have none of this stuff… I am a teacher (Mwalimu) by profession anyway.
So please just call me Mwalimu…’ In power, Mwalimu never allowed his family to run for political office or run Non-Governmental Organisations (NGOs), least of all his wife and children. If they did, it was only when he had formally retired as Head of State. He also never allowed himself to be overpowered by the trappings of power like awarding himself tenders or businesses.
Seeing the poor condition of his simple house at his home village as he moved closer to retirement, some public institution offered to rebuild and renovate the house for him! One can go on and on in one’s memory lane in so far as Mwalimu’s humility and integrity is concerned. Today, what ordinary people can say without blinking is that Mwalimu Nyerere was not personally a thief.
This explains why even after his retirement he continued to wield unprecedented moral clout and power. He spoke what he himself practised and people believed him because they had empirical evidence in his person! But there is one aspect in his person that made a huge difference and which literally put this country on international map. He knew exactly where to draw the line between personal likes and dislikes and matters of leadership in ethics and national principles.
For the two things, ethics and principles are the ones, which transcend one given leader – they also embody a given nation because they literally translate for a given nation’s self respect. Your memory lane and mine would remember that Tanzania was principled on the question of liberation of other countries in Africa and the principle of relationships with other nations based on sovereignty and genuine independence based on equality and not appendage.
On the latter, Tanzania was taken seriously in all international forums as ‘Africa’s moral voice of conscience.’ The super powers of this world knew the stand of this country, much earlier and they dared not push this country to their line of thinking! At home, everybody knew there was no “friendship” with the president on matters of ethics and national principles and bad leaders knew their place.
The questions to ask ourselves apart from whether we would ever fit into the shoes of Mwalimu Nyerere is what of the many aspects of the qualities of Mwalimu as a human person and a leader have we been able to emulate 11 years on after his death. Of course, there will and there can be only one Mwalimu Nyerere. But surely we have to try, at all levels, to emulate even one aspect of his many virtues, isn’t it?
As Prime Minister Mizengo Pinda asked the other day, does it make sense for a leader or an agricultural field officer to visit peasants at their small farms clad in a three-piece suit or top of the market blazer while the peasants he is visiting are clad in tatters or clothes which have not seen soap for six months?
Makwaia wa KUHENGA is a Columnist for this newspaper. E-mail: makwaia@bol.co.tz
Tuesday, October 12, 2010
Kwanini Dr. Slaa anawakosesha raha?
Hata hivyo kanadokeza kuwa kati ya vitu vyote vinavyowatisha ni masuala ya EPA na Meremeta. Masuala haya mawili hawataki kabisa yaangukie chini ya mtu kama Dr. Slaa ambaye tayari amejionesha kuwa licha ya kwamba hana madaraka kuwatolea uvivu watuhumiwa wa uhalifu bila woga jambo ambalo limemshinda mtu aliyeko madarakani.
Lakini japo hilo linaelezea kutishwa kwa waliko madarakani lakini halitoshi kuelezea kutishwa kwa Chama kizima na kuwafanya wawe kama wanapigwa na ubaridi. Ninajiuliza kwa kadiri siku zinavyokwenda yawezekana watawala wakalazimika kuanza kutumia mbinu za wazi za vitisho kama walivyofanya miaka ile walipoanza kuonesha filamu za mauaji ya kimbari ya Rwanda.
Lakini mbinu hiyo wameanza kuhisi haiwezi kufanikiwa kwani walitegemea wakihubiri juu ya umwagikaji damu basi watu wataanza kukwepa mikutano ya Slaa. Kinyume chake imekuwa kweli kwani watu wanachosema ni kuwa "hatudanganyiki".
Lakini ukweli bado unabakia kuwa kuna hofu ambayo haieleweki kwani siyo wana CCM tu bali hata taasisi nje ya CCM zinaanza kuonesha wazi kabisa kuhofia ajenda kali ya mabadiliko chini ya Dr. Slaa ambayo inavutia watu wengi zaidi (popular agenda).
Kilichowashangaza zaidi CCM kwa mujibu wa ka'nzi ni jinsi ambavyo wasomi (mijini) na wananchi wa vijijini wanavyokubaliana katika kumkubali Dr. Slaa. Huko nyuma watawala walitegemea utengano kati ya makundi hayo mawili huku baadhi ya kundi la wasomi likiiunga mkono CCM. Wanachofurahia hata hivyo ambayo inawapa matumaini kidogo ni kuwa bado CCM ni chama kinachokubaliwa na kupendwea na baadhi ya wafanya biashara ambao wanaamini katika chini ya CCM maslahi yao yanalindwa.
Monday, October 11, 2010
Tafiti za kama wa REDET ziangaliwe kwa macho mawili
Dk Benson Bana
ALHAMISI iliyopita, Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (Redet), ulitoa taarifa ya matokeo ya utafiti kuhusu maoni ya wananchi kuhusu uUchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Matokeo ya utafiti huo yalionyesha mgombea urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete anaongoza kwa asilimia 71.2 dhidi ya wagombea wa vyama vingine.
Mbali ya matokeo hayo ya Kikwete, Redet ilisema matokeo ya jumla yanaonyesha CCM inaongoza katika nafasi zote yaani urais, ubunge na udiwani. Matokeo hayo ni kwa utafiti wa mwezi uliopita.
Akitangaza matokeo hayo Mwenyekiti mwenza wa Redet, Dk Benson Bana alisema katika utafiti huo, Kikwete aliungwa mkono kwa asilimia 71.2 akifuatiwa na mgombea wa Chadema, Dk Willbrod Slaa asilimia 12.3 na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF akipata asilimia 10.1.
Katika utafiti huo, mfumo wa sampuli nasibu unaelezwa kuwa ulitumika kwa kuzingatia idadi ya watu waishio mijini na vijijini ili kupata matokeo ya uhakika.
Utafiti huo ulihusisha mambo mengi kama vile, maoni ya watu kuhusu vyama vya siasa na wagombea, maoni ya wananchi kuhusu uchaguzi wa rais na wabunge, maoni ya watu kuhusu mgombea urais, sifa za mgombea urais wanayemtaka n.k.
Kwa kuwa si rahisi kuzungumzia kila kitu kilichojitokeza katika matokeo ya utafiti huo, nichukue fursa hii kuzungumzia matokeo ya utafiti huo kwa upande wa kitaalama zaidi.
Nimeshawishika kujadili kipengere hicho kutokana na ukweli kwamba, matokeo ya utafiti huo kwa upande huo yanatisha, yameibua zogo.
Bila shaka yamewashangaza watu wengi kiasi kwamba, baadhi ya watu wakiwamo wagombea wenyewe mpaka sasa hawaamini kama kilichotangazwa na Redet ni cha kweli na baadhi wanathubutu kusema kuwa imehongwa.
Mashaka ya usahihi wa utafiti huo unatokana na takwimu zilizokusanya kutoa majibu tofauti na hali halisi ilivyo katika baadhi ya maeneo. Kwa mfano, Pemba ambako inajulikana wazi kuwa ni ngome ya CUF miaka yote tangu uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi ulipofanyika mwaka 1995, taarifa ya utafiti huo inaonyesha CCM inaongoza!
Najua kuwa utafiti huo ulifanyika kisayansi na unatakiwa kupingwa kisayansi, lakini zinapotolewa takwimu zinazokinzana na hali halisi, lazima kuwa na mashaka! Lazima mtu atajiuliza kwamba, hivi katika kipindi hiki kifupi yametokea mabadiliko makubwa kiasi hicho? Sipingi matokeo ya utafiti huo, lakini mashaka yangu yanaweza kuelekea kwa waliohusika kukusanya taarifa kwamba huenda hawakufanya kazi vizuri kwa makusudi, au maelekezo ya kutimiza lengo fulani.
Kwa mtaalamu yeyote anayejua maana ya utafiti ataelewa moja kwa moja kwamba utafiti wa Redet una maana gani. Maana hiyo ataipata baada ya kuingia ndani zaidi ya kile kinachoelezwa hadharani.
Nafahamu lengo la utafiti ni kujaribu kuelezea hali halisi ya wahusika kwa kutumia wawakilishi ndani ya wahusika hao, Ingawa kuna mambo lazima yazingatiwe.
Kwanza, msingi mkuu wa utafiti na ukusanyaji wa maoni huwa watu waliopo katika mazingira sawa sawa na tabia ya kufuata mkondo sawa wa fikra.
Uwezekano huu huwa sawa na kwa maana hiyo, badala ya kuuliza kila mtu kama anaunga mkono fulani. Huwa rahisi kutafuta watu wachache katika mazingira hayo ili kupunguza uwezekano wa kuchukua watu wanaoamua kujitenga kutoka kwa maoni ya watu wengi na njia hutumia hii kama mwongozo.
Pili, tumeelezwa lengo la wazi la utafiti huu, lakini hatujajua lengo lililojificha la utafiti ambalo kikawaida anayelijua ni mtafiti mwenyewe au mteja anayempa kazi ili aweze kuufanyia kazi.
Jambo jingine ni kwamba, tutambue kuwa huu ni utafiti wa kisayansi na hatuwezi kusema kuwa haukuwa halali na ili kuweza kujibu mapengo yaliyojitokeza tunatakiwa kufanya utafiti mwingine.
Jingine ni ukweli ulio wazi kwamba, popote pale, ukiwa madarakani kama unafanya kazi lazima uzalishe wasioridhika, hasa wakati ukisimamia utekelezaji wa sheria mbalimbali.
Kwa muktadha huo huo, upande wa pili lazima watu wakiwa wamekata tamaa lazima watafute tumaini, au mahali ambapo patawapa faraja na faraja hiyo wataipata upinzani.
La mwisho ni kwamba, utafiti wowote wapaswa kufanywa kwa kufuata kanuni ambazo mwishowe yanapatikana matokeo yanayoonyesha ukweli. Ukweli wa utafiti huu hatuwezi kuuzungumzia sababu hatuna kipimo kingine kilichopima kisayansi joto la uchaguzi mkuu.
Yahya Charahani ni mchambuzi wa masuala ya jamii, siasa na utawala.
Anapatikana kwa email: charahani@yahoo.com This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it
Blogu charaz.blogspot.com
Sunday, October 3, 2010
Tuchague viongozi bila kuangalia vyama vyao vya siasa
WATANZANIA wanaonyesha dalili za kuanza taratibu kukomaa kisiasa na pia wanaonekana kupenda mabadiliko kwa kuwa na viongozi waadilifu.
Mchakato wa Uchaguzi Mkuu unaoendelea nchini kwa takribani mwezi mzima sasa, umeonyesha picha hiyo ambayo ni jambo la maana katika maendeleo ya nchi yetu.
Angalau mpaka sasa katika michakato mbalimbali tumeshuhudia ukomavu wa wananchi kushindana kwa hoja na kutoleteana fujo wa vurugu zisizo na maana kama ilivyokuwa wakati wa kampeni za chaguzi tatu zilizopita. Pia tunaona Jeshi la Polisi likitekeleza majukumu yake kutowabughudhi wanaohudhuria na kufuatilia kampeni za vyama mbalimbali.
Ni katika kampeni hizi ambapo tunaona ukomavu mkubwa wa jamii ya Watanzania. Asilimia kubwa ya wananchi, wasomi na wasiosoma wako huru kutoa hoja zao wazi wazi, kueleza mambo yanayowakera na wanasikilizwa siyo na vyama vyote vya siasa.
Wananchi wameonyesha kukomaa kisiasa kwa kubadilika kwa kasi na kujiondoa katika kuelemewa na mapenzi ya kivyama, badala yake wanasikiliza, wanachambua na kubainisha hoja zao.
Kwa kiasi kikubwa wanakosoa pale kwenye upungufu na kupongeza pale panapofanyika mambo mazuri, tunaanza taratibu kuepuka mapambano baina ya vyama kwa vyama na mashabiki kwa mashabiki.
Tatizo linabakia kwa upande wa wanasiasa ambao wanaonekana wanaelendeleza mambo ya kale kwa kupakana matope.
Jambo hili linapaswa kuachwa na badala yake wanasiasa wetu wajifunze kueleleza kampeni zao katika sera za maendeleo na namna ya kuitekeleza.
Kimsingi uamuzi wa kuwachagua viongozi kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge, ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na urais bara na visiwani, haustahili kufanyika kwa misingi ya rangi, kabila au dini.
Kwa maana hiyo Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ulenge kuwachagua viongozi wenye dhamira ya kweli ya kuwaletea maendeleo wananchi na taifa kwa ujumla. Viongozi hao wanapaswa kuwa na nia isiyotiliwa shaka kuwa watawakwamua wananchi kutoka katika ufukara unaowakabili.
Kwa maana hiyo, Watanzania wenzangu, tusichague rais au viongozi kwa mazoea. Kama ni wa chama tawala anaonyeshe uwezo hali kadhalika kama wa chama cha upinzani ana uwezo achaguliwe ili aweze kulisaidia taifa hili kuingia katika karne nyingine ya maendeleo. Ni vizuri kubadilika kimawazo na mtazamo ili kulita mapinduzi yake kweli, kama Marekani walivyobadilisha historia ya nchi yao na dunia nzima kwa kumchagua Mmarekani mweusi, Barak Obama kuwa rais wa taifa hili kubwa na imara kiuchumi na nguvu ya kijeshi.
Nina hakika kama wangelikuwa na dhana ya mazoea na ubaguzi, Obama asingeota kuingia Ikulu hata siku moja. Suala la maendeleo ni suala pana ambalo halihitaji chama, dini wala kabila, bali linahitaji viongozi na wananchi wenye dhamira ya kutaka maendeleo.
Wakati umefika kwa watu wote wasiopenda siasa za kulumbana na za visasi, kuunga mkono siasa za maendeleo; bila kujali kabila, chama au hali. Kinachoshangaza ni kwamba, sasa hivi (wakati wa uchaguzi) zinajitokeza siasa za kuwahonga wapiga kura, vitisho kwa wananchi, uongo na hata za ushirikina ambazo ni kinyume cha maendeleo ya demokrasia nchini.
Tumaini jipya kupata viongozi sahihi na wenye nia ya kuliendeleza taifa letu, lipo kwa uchaguzi mkuu ujao ambao ukimalizika hatutausikia wala kuuona tena hadi mwaka 2015. Tumaini la kuwapima viongozi, sio kwa maneno yao tu; bali kwa matendo yao. Ni wakati wa kuwatambua kwa matendo yao.
Wanaohubiri kupinga dhuluma, huku nyuma wakishiriki na kushirikishwa kutoa rushwa ili wachaguliwe tuwatambue kwa matendo yao. Wale wanaojinadi kuwatetea wananchi huku wakiwazunguka, kisha kuwanyanganya ardhi na mali zao bila kuwalipa fidia inayostahili, pia tuwatambue kwa matendo yao. Baada ya hapo kura yetu iamue kwa haki kwa kumpa anayestahili.
*Yahya Charahani ni mchambuzi wa masuala ya jamii, siasa na utawala.
Anapatikana kwa email: charahani@yahoo.com This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it
Blogu charaz.blogspot.com
Saturday, October 2, 2010
Dk Slaa: Nimeisikia sauti ya Mungu ndiyo maana ninagombea urais
DK WILBROD SLAA
Swali: Ilikuwaje ukaamua kuingia katika kinyang’anyiro cha urais dakika za mwisho?
Jibu: Ukweli ni kwamba sikuwa na ndoto ya kugombea nafasi hii. Ilikuwa ni siku ya pili tangu nichukue fomu ya kugombea ubunge wa jimbo la Karatu, lakini nikaitwa kwenye vikao vya chama nikapendekezwa kugombea urais. Kwa kweli niliugua siku mbili kwa sababu nafahamu uzito wa nafasi hii. Unajua hata Mwalimu Nyerere alishasema kuwa Ikulu ni mzigo. Hata hivyo ilinibidi kuukubali uamuzi wa viongozi wenzangu.
Licha ya kamati kuu ya chama kuamua hivyo kulikuwa na ushawishi kutoka kwa watu mbalimbali walionishauri nigombee urais; Kuna wanafunzi zaidi ya 400 waliotia saini zao wakipendekeza mimi nigombee urais. Kwa hiyo hao pia walinitia moyo.
Pamoja na kuwa chama chetu tuna utaratibu wa kupata wadhamini 25 kwa mgombea urais, mimi niliwashauri wenzangu tuzunguke mikoani ili kuona kama kweli nakubalika huko.
Tumezunguka mikoa 19 ukiwamo mmoja wa Zanzibar, kwa kweli watu wametupokea…. Kuna baadhi ya mikoa zile fomu za udhamini walikuwa wakizigombea. Wengine walikuwa wakizisaini hadi usiku na ilitubidi kuwasha taa za gari ili wasaini. Kwa hiyo nikaona kuwa kuna sauti ya Mungu.
Swali: Pamoja na kusikia kilio cha wengi waliokutaka ugombee urais, wewe binafsi kitu gani cha ziada kilikusukuma?
Jibu: Nchi yetu ina matatizo makubwa. Ufisadi na wizi ndiyo uliotawala katika serikali ya CCM. Hata chakula cha wafungwa magerezani kinaporwa na askari. Fedha za miradi ya maendeleo zinahamishiwa kwa watu binafsi. Watanzania tunapewa pipi badala ya kilo ya nyama. Hayo ndiyo tunaambiwa maendeleo maana kila siku wanatulisha pipi, kwa kweli ni gharama kubwa kuiacha CCM iendelee kututawala.
Licha ya Mwalimu Nyerere kutaja maadui wakubwa watatu ambao ni Ujinga, umasikini na maradhi, CCM imeongeza adui wa nne ambaye ni ufisadi.
Tatizo jingine ni umasikini uliokithiri ambapo tangu mwaka 2001 hadi 2008 Watanzania ambao ni masikini wa kutupwa wameongezeka kutoka 11.4 milioni hadi 12.9 milioni.
Kwa kweli hapa inaonyesha wazi kwamba Tanzania tunahitaji uongozi utakaoweza kubadilisha haya. Fedha za EPA zingeweza kujenga shule zaidi ya 1000.
Tulipobadilisha Azimio la Arusha na kuunda Azimio la Zanzibar ambalo hadi leo hakuna kumbukumbu zozote zilizoandikwa na kuwekwa bayana zilizotokana na Azimio lile, lakini pale ndipo tulipopoteza msingi mkubwa wa uadilifu na hapo ndipo ulipoanza ufisadi.
Tatizo jingine ni mfumo mbovu wa uendeshaji wa serikali unaosababishwa na Katiba mbovu.
Kwa ujumla tumeona kuwa tatizo kubwa lililopo ni ukosefu wa uongozi.
Tanzania ya sasa inahitaji kiongozi mwenye uwezo wa kuongoza, anayekubalika, mwadilifu na chama chenye sera zenye kuweza kuleta mabadiliko.
Swali: Nini vipaumbele vyako kama utafanikiwa kuwa rais wa Tanzania?
Jibu: Kwanza nitajenga mfumo mpya wa serikali kwa kubadilisha Katiba. Katiba ya sasa inampa mamlaka makubwa mno rais. Rais anachagua kila kitu mpaka mkurugenzi wa shirika la kulala na kunywa pombe. Mtu analiangusha shirika moja anahamishwa na kupelekwa katika shirika jingine.
Katiba tuliyonayo inaweka hatima ya watu zaidi ya milioni 40 mikononi mwa mtu mmoja. Rais ndiye anayeamua ni wizara ngapi ziwepo.
Wenzetu Marekani wako zaidi ya milioni 200 lakini wana mawaziri 14 tu. Uingereza wako 75 milioni lakini baraza lao lina mawaziri 20. Lakini Watanzania tuko 40 milioni tunakuwa na baraza la lenye mawaziri hadi 47au 67.
Kazi kubwa ya Manaibu waziri waliopo sasa ni kujibu maswali Bungeni ambayo hata hivyo huyajibu juu juu tu.
Wote hao wahudumiwe mashangigi ya Sh 200 milioni na mahitaji mengineyo. Bado hapo unazungumzia makatibu wakuu na watumishi wengine. Mkuregenzi anabadilishiwa fenicha kila mwaka.
Mzigo wote huu wanatwishwa walipa kodi. Badala ya kodi ya maendeleo kuleta maendeleo ina kazi ya kuhudumia viongozi wa serikali tu.
Nikifanikiwa kuingia madarakani nitabadilisha Katiba ili tuwe na mawaziri 20 tu au hata 15. Nitawapa madaraka wananchi katika maamuzi ya serikali tofauti na sasa ambapo wananchi wenyewe hawakushirikishwa kuiunda Katiba yao.
Katiba iliyopo Ibara ya 8 inasema kuwa mamlaka yote ya serikali yanatokana na wananchi, lakini kihalisia hivyo sivyo inavyofanyika. Hivyo tunaona kuwa ipo haja ya kufanya mabadiliko makubwa ya katiba na hayo ndiyo yatakayoleta mabadiliko katika mfumo mzima wa serikali.
Kipaumbele kingine ni huduma za jamii, tutaboresha elimu. Elimu kwa sasa imeshuka sana. Wakati wa Mwalimu Nyerere kulikuwa na kisomo cha manufaa ambapo Tanzania ilisifiwa na Unesco kwa kufikia kiwango cha asilimia 70, lakini sasa imeshuka hadi asilimia 40.
Takwimu za Mpango wa maendeleo ya sekondari inaonyesha kuwa, serikali ilitakiwa kujenga shule 22,000 lakini hadi sasa imejenga shule 300 tu.
Ahadi kwenye bajeti zipo, lakini hazitekelezwi. Fedha za kashfa ya EPA tu zinaweza kujenga shule bila kuchangisha mtu.Kwetu sisi elimu ya lazima itakuwa ni kidato cha sita.
Kipaumbele kingine ni huduma bora za afya ambapo tutaimarisha afya ya msingi na kuipa kipaumbele katika bajeti.
Huduma nyingine ni maji, leo Watanzania wengi hawapati huduma ya maji licha ya kuwa na vyanzo vingi vya maji.
Niliwahi kwenda Mtwara ambako nilikutana na wananchi wa huko. Baadaye nikaletewa maji ya kunywa, nilidhani ni pombe nikataka kuijaribu, nikaambiwa hayo ndiyo maji ya kunywa. Ilibidi twende umbali wa kilometa 15 nikayaone maji wanayochota. Hali ni mbaya.
Kwa upande wa kilimo, nako hatufanyi vizuri. Tumekuwa tukiomba chakula kila mwaka wakati nchi yetu inaweza kuzalisha chakula kingi, hii ni aibu! Tatizo ni ufisadi, kuna taarifa katika Mpango wa Maendeleo wa sekta ya kilimo (ASDP) asilimia 80 ya bajeti yake imepotea kutokana na wizi na semina za kujitengenezea posho.
Hii ni aibu kabisa, Kila mwaka tunaomba msaada wa chakula kutoka nje. Ni mwaka huu kwa sababu tu mvua zimenyesha sana. Lakini Rais Kikwete anasema kuwa mafanikio yamepatikana kutokana na mkakati wa kilimo kwanza wakati mkakati wenyewe una mwaka mmoja tu tangu uanzishwe. Kazi ya serikali ni kutoa kauli mbiu tu kila mwaka, kaulimbiu hazizalishi!
Bilioni 21 zilizochezewa, zikaitwa za Kikwete hatujui zimekwenda kwa nani.
Kama tungekuwa na mikakati mizuri ya kilimo Tanzania inao uweza kulisha nchi nyingine za Afrika.
Kuhusu miundombinu , Tanzania inapaswa kuwa na treni inayotumia umeme na siyo kuendeleza treni zinazotumia dizeli tangu wakati wa ukoloni. Usafirishaji kwa njia ya malori unaotumika sasa una hasara kubwa kwa serikali ukilinganisha na usafirishaji kwa njia ya reli.
Ni gharama kubwa kuendelea kuvumilia kutawaliwa na CCM. Hakuna utashi wa kisiasa, hakuna anayechukua maamuzi na wala hakuna utawala wa sheria. Nchi ina ‘double standard’ katika kuchukua maamuzi ya kisheria; anayeiba kuku au Sh500 anafungwa lakini anayeiba mabilioni anaachiwa huru na hata anaambiwa kuwa akirudisha atasamehewa.
Swali: Ni vipi utalishughulikia suala la rushwa?
Jibu: Serikali yangu haitakuwa na msalie Mtume na wala rushwa, ni ‘zero tolerance’ kwa ufisadi. Rasilimali zilizotumika vibaya zitarejeshwa serikalini.
Swali: Je, unadhani Chademaina ubavu wa kuiondoa CCM madarakani?
Jibu: Tunaweza kuwaondoa endapo haki itatendeka.
Tatizo ni kuwa hakuna ‘level ground’ ya siasa hapa nchini.
Lakini kwa kuwa wananchi wamechoka na wanasema kuwa safari hii hawakubali tena kudanganywa, tuna imani kwamba Chadema ndicho chama mbadala. Amani wanayoiimba CCM ni amani ya hofu, hakuna amani kwa mtu anayekula mlo mmoja kwa siku.
Swali: Katika uchaguzi kuna kushina na kushindwa, je nini itakuwa hatima yako kisiasa endapo utashindwa?
Jibu: Kwanza sijutii kugombea nafasi hii na ikiwa sikubahatika kuipata basi naweza kuwa Spika wa Bunge kwani nafasi hiyo inaweza kushikwa na hata mtu asiye mbunge.
Kadhalika hata kama hilo halitawezekana sitajuta kwa sababu nina imani kwamba nitaendelea kuwatumikia Watanzania.
Mbila: Nimefuata mageuzi ya kweli Chadema
GEORGE Mbila ni Mgombea udiwani kata ya Ubaruku Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya kupitia tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Kabla ya hapo alikuwa ni diwani katika kata hiyo kuptia chama cha Wafanyakazi Tanzania (TLP). Je, nini kimemfanya akihame chama hicho na kukimbilia Chadema?
Mbila mwenyewe anaeleza sababu kuu ya kufanya maamuzi hayo kuwa ni kupoteza mwelekeo kwa TLP.
“Nilikuwa diwani wa kata ya ubaruku kwa tiketi yaTLP sasa nimehama sipo tena kwenye chama hicho na sasa nagombea kwa awamu ya pili lakini kwa kupitia chama changu kipya cha Chadema kwani chama cha TLP kwa sasa kimekosa mwelekeo na hivyo kusababisha wanachama wake kuyumba” anasema Mbila.
Anasema kuwa kabla ya kukihama chama hicho alifanya uchunguzi wa kina ili kuweza kubaini chama ambacho kina sera zinazomlenga mwananchi ambaye ndiye mpiga kura.
Nimebaini kuwa Chadema ndiyo chama pekee ninachoweza kukitumikia katika kuwaletea maendeleo wananchi wa kata ya Ubaruku.
Mbila anazitaja sera za Chadema katika uchaguzi huu wa mwaka 2010 zilizomvutia ni pamoja na Elimu kutolewa bure kuanzia madarasa ya awali hadi kidato cha sita ambapo anasema kuwa hilo linawezekana na katika sekta ya afya.
Anasema hata sera ya Chadema ya kuongeza mishahara ya wafanyakazi inatekelezeka kwani kama diwani analipwa posho ya kikao kimoja sh 45,000, kwa wafanyakazi pia itawezekana.
Akielezea mambo aliyoyafanya katika kipindi cha miaka mitano iliyopita katika kata yake anasema kuwa katika kipindi hicho ameweza kufanikiwa katika sekta mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuwa na ushikiraikiano mzuri na wananchi na uongozi mzima wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali na hivyo kupata nguvu ya kuamua kugombea tena kwa awamu ya pili.
Anaeleza kuwa katika kipindi cha miaka mitano kwenye sekta ya elimu ameweza kuhamasisha na kufanikiwa kujengwa madara 12 na ofisi mbili za Walimu katika shule za kwa mpango wa MMEM.
Anazitaja shule hizo na idadi yake ya madarasa kuwa ni pamoja na shule ya msingi Mwanawala amefanikiwa katika ujenzi wa madarasa mawili na ofisi moja, Rujewa Mission madarasa manne, Ibohola madarasa manne,Urunda darasa moja na mpakani darasa moja na ofisi moja.
Mafanikio mengine katika sekta ya elimu ni pamoja na ujenzi wa nyumba 10 za Walimu kwa mpango wa MMEM ambapo katika shule ya Mwanawala nyumba mbili, Mahongole nyumba moja , Ibumila nyumba moja, Imlilo Songwe nyumba mbili, Mpakani nyumba moja, Utyego nyumba moja, Rujewa mission nyumba moja na Mkombe nyumba moja.
Katika shule za sekondari anasema kuwa, amefanikiwa kujenga madarasa 30 ambpo katika suhule ya sekondari Mbarali madarasa 21, Imalilo Songwe tisa na majengo ya utawala na hosteli moja ya wasichana katika shule ya sekondari Imalilo Usongwe na jumla ya madawati 590 yamechangwa katika kipidi hicho kwa shule za sekondari za Mbarali na Imalilo Usongwe.
Mbila anaeleza kuwa katika sekta ya maji ameweza kuhamasisha na kusimamia kupeleka miradi ya maji katika kijiji cha Utyego Mwakaganga kwa mpango wa DADS wenye thamani ya sh 62 miioni ambapo halmshauri ilitoa sh 52 milioni na wananchi walichangia sh10 milioni na nguvu kazi.
Anasema kuwa miradi mingine ni pamoja na ujenzi kisima cha maji katika kijiji cha Mwakaganga wenye thamani ya sh32 milioni na mradi wa maji ambao ulifadhiliwa na benki ya dunia katika kijiji cha Ubaruku uliogharimu sh 211 milioni ambapo maji hayo yanahudumia vijiji Viwili katika kata hiyo ya Ubaruku.
Katika miundo mbinu ya barabara anaeleza kuwa katika kijiji cha Utyego kwa mpango wa Tasaf kijiji hicho kimejengewa barabara kiwango cha changarawe yenye urefu wa kilometa tano (5km) na Mbarali hadi Mwanawala kilometa 13.
Anasema kuwa kupitia utaratibu waliojiwekea wa kutengeneza barabara kila mwaka wamefanikiwa kujenga barabara za Ubaruku mjini zenye urefu wa kilometa 12 ujenzi wa makaravati 10 katika sehemu korofi.
Anaeleza pia katika kipindi hicho miaka mitano katika sekta ya kilimo na mifugo kwa kushirikiana na wananchi ameweza kubuni mradi mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji unaoitwa mwendo mtitu ambapo katika bajeti ya mwaka 2009/2010 halmshauri ya Wilaya ya Mbarali ilitoa milioni 20 kwa ajili ya upembuzi yakinifu katika mradi huo.
Anasema kuwa katika bajeti ya mwaka 2010/2011 ya halmashauri hiyo imetenga milioni 18 kwa ajili ya kutengeneza banio katika mradi huo na halmashauri inaendelea kutafuta mfadhili kwa ajili uchumbaji wa mifereji na kwamba vijiji vitakavyohusishwa ni pamoja na Mwakaganga, Hurunda, Imalilo Usongwe, Mwanawala, Igumilo na Nyelegete.
Mgombea huyo anaeleza kuwa katika kipindi hicho waliweza kuanzisha ujenzi wa machinjio ya ng`ombe wenye gharama ya milioni 15 ambapo ujenzi huo upo katika kijiji cha majengo.
Aidha anaeleza kuwa katika sekta ya Afya pia ameweza kupata mafanikio katika kipindi hicho cha maika mitano ambapo zahanati moja iliweza kujengwa katika kijiji cha Imalilo Usongwe wenye thamani ya sh 12 milioni, ujenzi wa nyumba mbili za waganga katika zahanati ya ubaruku na kituo cha afya Rujewa Mission zenye gharama ya sh16 milioni kwa kila nyumba.
“Pamoja na hayo yote niliweza kuomba ufadhili kituo cha malezi (UMATI) wa kutujengea kituo cha kutolea ushauri nasaha ambapo tayari tumeshafanyiwa lakini pia nimeweza kuishauri halmashauri kuipandisha zahanati ya Rujewa Mission kuwa kituo cha afya na ikawa hivyo” anasema
Anasema kuwa pia ameweza kuishauri Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali kuweza kuwalipia ada watoto yatima 190 katika shule ya sekondari Mbarali na Imalilo Usongwe.
Mimi mwenyewe nina watoto 10 ninaowalipia ada na wengine wanne tayari wameshamaliza kidato cha nne.
Mbila anaeleza mambo ambayo anatarajia kuyafanya endapo kama atachaguliwa kwa mara nyingine kuwa ni pamoja na kutekeleza sera za chama cha Chadema na kuhakikisha kata ya Ubaruku inakuwa mji mdogo ili kuweza kusogeza katibu huduma za kijamii kwa wananchi.
Anasema kuwa atahakikisha shule za sekondari zinakuwa na kidato cha tano na sita na kuhakikisha umeme katika shule ya sekondari mbarali unafika na kwamba ni mpango ambao tayari umeanza na mpaka sasa sh 1.4 milioni zimeshachangwa na maandalizi yanaendelea kwa ajili ya kazi hiyo.
Mamabo mengine anayotarajia kufanya ni kujenga hosteli za wanafunzi wasichana na kuhamisha ujenzi wa barabara katika meneo korofi na kufikisha maji katika vijiji ambavyo bado havijapata maji na katika sekta ya afya ni kuhakikisha kila kijiji kina zahanati .
Kutokana na jitihada zake za maendeleo katika kata hiyo, Mbila anaamini kuwa atachaguliwa tena katika nafasi hiyo,
“Naamini wananchi watanichagua tena kutokana na kuwa wananipenda na kuniamini kwakuwa nimeshirikiana nao vizuri katika kipindi cha miaka mitano iliyopita”.
Mbila ana elimu yake ni ya kidato cha nne aliyoipata mwaka 1990 katika shule ya sekondari ya Meta iliyopo jijini Mbeya.
Baada ya hapo mwaka 1991 hadi 2000 alijihusisha na biashara za ng`ombe mkoani Dodoma. Mwaka 2000 hadi 2006 alikuwa katibu wa wafanyabiashara wa mchele kata ya Ubaruku na 2005 hadi 2010 amekuwa diwani wa kata ya ubaruku kupitia chama cha TLP.
Friday, September 17, 2010
Wameshindwa miaka 25 wataweza miaka 5?
Baada ya Baba wa Taifa Mwalimu J. K. Nyerere kusoma alama za nyakati
na kuelewa kuwa kwa uwezo wake wa kibinadamu aliweza kuwafikisha
Watanzania mahali alipowafikisha aliamua kuachia "ngazi" au kama
tulivyoita wakati ule aliamua kung'atuka. Shujaa wangu alitambua kuwa
uongozi una kikomo chake cha uwezo wa mwanadamu na vyovyote vile
ilivyo alitambua kuwa Tanzania ni lazima itakuja kutawaliwa na watu
wengine nje ya yeye mwenyewe.
Hivyo, akaliandaa Taifa kuwa na viongozi wengine na akamuachia Mzee
Ali Hassan Mwinyi kushika usukani. Mwinyi akaingia na Ruksa kwa miaka
kumi ya kile ambacho kinajulikana kama ufunguaji wa uchumi wetu kwa
sekta binafsi. Hii iliaminika kuwa ingekuwa dawa ya kulileta taifa
letu katika mafanikio ya mtu mmoja mmoja. Naye alipomaliza miaka yake
kumi akamuachia Mkapa ambaye naye aliingia kwa kubinafsisha taasisi na
makampuni mbalimbali yaliyokuwa ya umma kwa nguvu kubwa. Mkapa akawa
mtu aliyefungua uchumi wetu kwa wawekezaji wa ng'ambo kwa kiasi
kikubwa akisimamia upitishwaji wa baadhi ya sheria mbovu kabisa kuwahi
kutungwa na watu huru.
Alipomaliza naye miaka yake kumi ya majaribio ambayo iliisha kwa
mlolongo wa kashfa ambazo hazijawahi kutoka katika taifa hili
akamuachia usukani Rais Kikwete ambaye naye aliahidi kuendeleza
"mazuri" yaliyofanywa na serikali zilizopita na kuleta mapya kwa kile
alichokiita "kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya". Kikwete alipoingia
aliingia kwa kujumlisha yale ya Mwinyi (Ruksa) na yale ya Mkapa
(Ubinafsishaji) kwa nguvu zaidi lakini akaongeza na ya kwake ambayo
ameyasimamia miaka hii mitano inayoisha. Yeye kaja na Uchumi wa
Wawekezaji akiamini kabisa kuwa bila ya wawekezaji wa kigeni Tanzania
haiwezi kuendelea na hivyo akitumia nadharia ya ruksa (ya Mwinyi)
amezidi kufungua sekta na sehemu mbalimbali za uchumi wetu kwa
wawekezaji wa kigeni hata katika mambo ambayo ukiyakodolea kwa karibu
yanashangaza (kama uchimbaji wa vyoo vya shule!)!
Kikwete naye kama Mkapa kabla yake amesimamia serikali iliyogubikwa na
mlolongo wa kashfa ambazo kuzirudia tena kunaweza kuwa ni kashfa vile
vile.
Miaka ishirini na mitano ya watawala watatu ilitarajiwa ingeweza
kufuta na kurekebisha matokeo ya utawala wa Rais mmoja aliyekuwa
madarakani kwa karibu miaka 24 hivi. Lakini nusu karne ya watawala
watatu mbalimbali wakiwa na faida ya ulimwengu wa kisasa, uliotulia
kutoka katika vita baridi, chini ya Afrika iliyo na amani zaidi na
mahusiano ya kimataifa ambayo yametengemaa kuliko wakati wowote ule
katika historia yetu. Watawala hawa watoto wamekuja na kila mpango na
miradi ya "maendeleo" ambayo wameijaribisha. Kuanzia mipango ya
"kufufua uchumi" ya miaka ya themanini na mipangao ya MTUKUTA,
MKURABITA na MMEM n.k ya miaka ya 2000!.
Kusema kweli wamejaribu. Wamejaribu kutawala na kufanya yote yaliyo
ndani ya uwezo wao. WAmejaribu kurekebisha muundo wa serikali,
wamejaribu kupigana na rushwa, wamejaribu kubadilisha elimu ya msingi,
sekondari na ya juu, wamejaribu kuleta utawala bora. Naam! Wamejaribu
saana kama timu ambayo licha ya jezi nzuri, na makocha wazuri
imeendelea kufungwa katika mechi zake mbalimbali hata zile ambazo
walitarajiwa angalau kutoka sare. Wamejaribu kuliongoza taifa kwa
miaka 25. Na wamefanikiwa katika kujaribu.
Wamefanikiwa kujaribu kuongeza vitu mbalimbali na ni kweli chini yao
idadi ya vitu mbalimbali imeongezeka. Ukiwasikiliza kwa makini utaona
wanasifia idadi zaidi kuliko ubora. Kwao wao maendeleo ni kuongezeka
kwa idadi. Watasema wameongeza idadi ya vyuo, walimu, shule, majengo,
n.k Wameanza kuwa kama Korea ya Kaskazini! Wanajivuna katik akuongeza
idadi. Lakini macho yetu yanatufanya tuwe mashuhuda wa kushindwa
katika majaribio yao.
Bado jiji la Dar ni miongoni mwa majini machafu kabisa, bado elimu ya
juu ina matatizo makubwa katika ubora na upatikanaji wake, hospitali
zetu bado hazijafikia kiwango cha kisasa zikiendelea kuwa mlundikano
mkubwa wagonjwa, mipango yetu ya uokoaji bado ni mibovu kabisa kama
tulivyoshuhudia juzi mtu aliyekuwa kwenye mtaro kwa masaa ishirini na
nne akiojaribiwa kuokolewa kwa njia za enzi za ujima! Katika miaka yao
ya robo karne bado kuna watoto wetu vijijini na mijini ambao wanasoma
kwa kukalia matofali huku madara yao yakiwa yameezekwa nyasi wakati
mtu mmoja anajengenewa jumba analo"stahili" kwa bilioni 3, huku wao
wakijigawia bilioni karibu thelathini kila mwaka kwa ajili ya samani
na chai huku wakiahidi kuleta bajaji kupeleka mabinti, mama na dada
zetu hospitali wakati wa kujifungua!
Wamejaribu ndugu zangu. Kwa miaka 25 wamejaribu kushindwa na kwa
hakika wameonesha jinsi wanavyozidi kushindwa. Kinachoshangaza ni kuwa
wanataka miaka mingine mitano ya majaribio mengine makubwa. Yaani
wanataka kujaribu kutuahidi kuwa yale ambayo wameshindwa kuyafanya kwa
miaka 25 wataweza kuyafanya kwa miaka mitano kwa kutumia viongozi wale
wale, wenye sera zile zile wakiongoza na itikadi ile ile ya
"majaribio".
Kumbe swali kubwa ambalo wapiga kura wa Tanzania wanakabiliwa nalo na
ndilo kubwa litakalotakiwa kuwaongoza kupiga kura katika uchaguzi huu
mkuu ni hili: Je, wanaamini utawala wa CCM uliodumu kwa miaka 25
katika majaribio yaliyoshindwa unaweza kufanikiwa katika miaka mitano?
Je, kama wameshindwa kuboresha shule za msingi kwa miaka 25 wataweza
kweli kufanya hivyo kwa miaka mitano? Kama wameshindwa kutafuta namna
nzuri ya kutoa elimu ya juu kwa miaka 25 ya uliberali wa kiuchumi
wataweza kweli kufanya hivyo kwa miaka mingine mitano? Je wananchi wa
Dar ambao wanaishi katika mojawapo ya majiji yaliyopangwa vibaya
zaidi, machafu na yenye changamoto za kudumu za maji, umeme na usalama
kwa miaka 25 kweli wanatarajia kuwa maisha yao yatakuwa tofauti na
hali zao kuinuliwa kwa miaka mitano ijayo? Kweli wakazi wa Dar
wanaamini chini ya watawala wale wale hospitali ya Mwananyamala,
Temeke na Muhimbili zitakuwa bora zaidi miaka mitano ijayo kuliko
miaka 25 iliyopita?
Naam, wapo wanaomini kuwa inawezekana. Naam ni imani tu. Na wengine
wataapia kabisa kuwa inawezekana. Lakini msingi wa imani hiyo ni nini
isipokuwa njozi kama za Alinacha? Wale wale walioshindwa miaka
ishirini na mitano wataweza kweli miaka mitano?
Waliokataa kufanya marekebisho makubwa ya Katiba miaka ishirini na
mitano wataweza kuleta mabadiliko miaka mitano bila mabadiliko makubwa
ya Katiba? Walioshindwa kutunga sheria nzuri za uwekezaji na sera
nzuri za misaada ya kigeni kwa miaka ishirini na mitano wataweza kweli
kuleta mabadiliko katika miaka mitano ijayo?
Ndugu zangu, tunapoendelea kutafakari ujio wa uchaguzi mkuu ni lazima
tujiulize katika dhamira zetu kama tunataka mabadiliko makubwa miaka
mitano chini ya uongozi mpya, wenye sera tofauti na za sasa na wenye
maono makubwa zaidi au kuendelea kwa kujaribisha watu wale wale ambao
tunajua tayari wameshatuonesha kuwa wanashindwa?
Kama tumekuwa kwenye basi ambalo dereva wake amekuwa akipata ajali za
mara kwa mara na kusababisha maafa na majeruhi miaka 25 tuendelee
kumchagua dereva yule yule kwa vile ati tumemzoea na kwa vile tayari
tunajua kuwa anaweza kupata ajali nyingine au tuamue kumpatia dereva
mwingine ambaye anakuja na gari jingine na utaalamu mwingine wa
uendeshaji wa gari hilo?
Katika uchaguzi huu wapo watakaoingia kwenye gari la kwanza kwa vile
wamelizoea na wanajua kuwa hata ajali ikitokea wanaweza wasidhurike.
Lakini ni majasiri wale wanaotaka kuingia kwenye gari jipya chini ya
dereva mpya. Hapo pana tofauti kati ya wenye hofu na majasiri.
Kutokana na mazoea wengine watapanda gari la kwanza na hatuwezi
kuwashangaa kwani ndilo gari pekee lililokuwepo kijijini kwa muda
mrefu, lakini nuru mpya na mwanga mpya umeanza kuangaza, gari jipya
lipo kijijini, dereva mpya kashika usukani, anasema twende!
Waliozoea gari la zamani lenye ajali za mara kwa mara na waende
kulipanda kwa furaha, lakini wanaotaka kutafuta njia mbadala
wanalazimika kutafuta usafiri mwingine. Kwani, gari lililoshindwa
kupanda mlima kwa miaka 25 litaweza vipi kupanda kwa miaka mitano
likiwa na dereva yule yule, makonda wale wale na ubovu ule ule? Labda
kuna wakati inabidi hata tutumie pikipiki!
Thursday, September 16, 2010
Dk Slaa: Tumechoka kupiga debe, sasa tunataka usukani
Dr Willibrod Slaa
KILA chama cha siasa lengo lake kuu ni kushika dola ili kupata fursa ya kutekeleza ilani yake.
Kila chama huwa kina mpango mkakati au mbinu za kutumia katika kuwahamasisha na kuwakampeni wananchi, ili wakichague chama husika na wasikichague chama kingine.
Chadema kwa kutumia mgombea wake wa urais Dk Wilibrod Slaa anasema, “Lengo langu ni kuing’oa CCM na kwa maana hiyo sina njia nyingine ya kufanikisha azma yangu zaidi ya kutafuta machafu yao na kuyaweka wazi kwa wananchi.”
Dk Slaa anataja sababu 13 zinazowapa Watanzania uhalali wa kuiondosha madarakani CCM, ili kuondokana na upigadebe ndani ya miaka 15 tangu mfumo wa vyama vingi uingie nchini.
Akizungumza katika mikutano mbalimbali ya kampeni Dk Slaa anasema umefika wakati wa Watanzania kuachana na upigadebe na kuipa Chadema usukani wa kuendesha gari kwa miaka mitano ijayo.
Akitaja sababu hizo, Dk Slaa anasema:
Sababu ya 1: Ni kwamba Rais Jakaya Kikwete amewatukana na kuwadhalilisha kinamama wa Tanzania kwa kuwaahidi kuwanunulia bajaji 400 ili kubebea wajawazito.
“JK amewatukana Watanzania, utamwekaje mama anayeumwa uchungu na hali ya bajaji ilivyo mpaka afike salama katika kituo cha afya. Lakini wakati waziri wake mwanamke akitembelea gari la Sh200 milioni anataka kuwapandisha bajaji Watanzania wanaotaka kuleta Watanzania wapya, amewadhalilisha,” anasema Dk Slaa.
Dk Slaa anasema kuwa ahadi hiyo ni hewa kwani alishaitoa bungeni wakati akizungumza na wabunge miaka mine iliyopita na hakuitekeleza.
“Kama ameshindwa kuitekeleza alipoitoa bungeni miaka minne iliyopita leo anaitoa tena, atawezaje kuitekeleza? Au atuambie kama bajaji hizi ni nyingine au ni zile zile alizoahidi 2006? Na kama ni nyingine je, zile alizipeleka wapi?” Anahoji Dk Slaa.
Sababu ya 2: CCM inapaswa kung’oka kwa sababu baada ya Mwalimu Nyerere kuondoka madarakani walifuta Azimio la Arusha lililoleta umoja, upendo na kupiga vita ufisadi wakaja na Azimio la Zanzibar na kuwagawa Watanzania kimatabaka.
“Nimekaa bungeni kwa miaka mitano naomba nakala ya Azimio la Zanzibar nimeshindwa kuipata hata wazanzibari wenyewe hawana. Huu ndio mwanzo wa matabaka na ufisadi nchini,” anasema Dk Slaa.
Sababu ya 3: Tanzania hivi sasa inaongozwa na manyani wakubwa wanaoishi kwa kukwapua mali za watanzania bila ya huruma.
Anasema, “Hata baba wa taifa akifufuka leo na kuja kuona hali ya Tanzania ilivyokuwa mbaya kimatabaka katika kipato, basi atamuomba Mwenyezi Mungu afe ili arudi kaburini.”
“Makamba anasema natukana, lakini sina lugha nyingine ya kusema, fisadi ni fisadi tu na mwizi ni mwizi tu hana jina jingine, nimehangaika katika makamusi sijapata jina mbadala la mwizi” anasema Dk Slaa.
Sababu ya 4: Ni kuongezeka mara dufu kwa safari za nje za raisi Kikwete huku mabilioni ya watanzania yakipotea kwa safari hizo.
“Fedha zetu zinaisha kwa safari za nje, huku faida yake ikiwa ni chandarua hata dawa ya kupuliza hapati. Lakini nawambia watanzania ziara za JK hazijaleta faida yoyote katika uwekezaji nchini,” anasema Dk Slaa.
Anasema hamzungumzii rais kama cheo bali anamzungumzia mgombea wa CCM katika nafasi ya uraisi, hivyo anachofanya ni kumkosoa yeye na chama chake (CCM) na kueleza nini Chadema itafanya iwapo itashinda.
Sababu ya 5: Rais Kikwete aliahidi kujenga uwanja mpya wa ndege jambo ambalo hajalitekeleza hadi sasa miaka mitano imeisha na kwamba anakuja tena na ahadi kama hiyo.
“Nimezunguka mikoa yote na naendelea kuzunguka sijaona uwanja mpya bali viwanja vyote vya ndege ni kama malisho ya ng’ombe,” anasema Dk Slaa.
Sababu ya 6: Chanzo cha umasikini wa Watanzania ni wabunge wa CCM ambao wanashindwa kuwatetea Watanzania wanapokuwa bungeni.
Sababu ya 7: Rais Kikwete hafai kuwa rais tena kwa sababu hasomi na kwamba kila siku anarudia kuahidi mambo aliyoshindwa kuyatekeleza katika awamu yake ya kwanza.
“Utashangaa baadhi ya wakati anatoa ahadi ambazo alishazitoa na hajazitekeleza. Kama hii ya bajaji hata ukienda katika vitabu vya kumbukumbu ya bunge (hansard) imo, lakini unashangaa anairudia baada ya miaka mine kupita,” anasema.
Sababu ya 8: Ni kuwapo kwa matabaka makubwa katika viwango vya mishahara ya watumishi wa Umma nchini.
“Leo polisi wetu wanalazimika kuvuta kitu kidogo kwa wananchi masikini kwa sababu ya matabaka haya, mkitupa ridhaa yenu tutafumua mfumo huu ndani ya siku 100 na kuondoa matabaka,” anasema Dk Slaa.
Sababu ya 9: CCM imeshindwa kupambana na ufisadi ambao unazidi kuwakandamiza watanzania kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi.
Sababu ya 10: Rais Kikwete anavunja sheria alizozisaini mwenyewe jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi.
“Kifungu 21 (1) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi aliyoisaini kwa mbwembwe nyingi, kinazuia mgombea kutoa ahadi jukwaani, Kikwete ametoa ahadi nyingi kama mgombea, je, hajui sheria,” anahoji Dk Slaa.
Sababu ya 11: Dk Slaa anasema kutokana na kutowajali watanzania CCM waliingiza kinyemela kipengele katika sheria ya gharama za uchaguzi bila ya kujadiliwa bungeni na wao walithibitisha.
Sababu ya 12: Anaitaja kuwa ni ahadi ya maisha bora kwa kila mtanzania kutotekelezwa ipasavyo na serikali ya CCM na ndio mana wengi mnaishi katika nyumba zilizozekewa matope.
“Mkitupa ridhaa yenu tutafuta kodi katika vifaa vyote vya ujenzi ili muweze kujenga nyumba bora kwa sababu maisha bora yanaanzia nyumbani,” anasema Dk Slaa.
Sababu ya 13: Rais Kikwete aliahidi kujenga vyumba vya madarasa 22,000 lakini kwa takwimu za serikali baada ya miaka mitano wamejenga vumba 300 tu.
“Hatuwezi kuwa na serikali inayojisifu kwa kujenga vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo, huku kukiwa hakuna walimu, maabara, maktaba na maji ya kutumika katika vyoo,” anasema Dk Slaa.
http://www.mwananchi.co.tz/makala/-/4720-dk-slaa-tumechoka-kupiga-debe-sasa-tunataka-usukani
Wednesday, September 15, 2010
Arcado Dennis Ntagazwa: Yatima mlala njaa na mchunga mbuzi aliyegeuka kigogo kitaifa
Mwandishi Wetu | Septemba 1, 2010 |
AGOSTI 16, mwaka huu, Mwandishi Wetu, Godfrey Dilunga, alifanya mahojiano na Arcado Dennis Ntagazwa, aliyekuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, Pili na ya Tatu. Aliwahi kuvuliwa uraia na baadaye kukata rufaa na kushinda kesi. Katika mahojiano hayo, Ntagazwa ambaye amehama CCM kwenda CHADEMA na kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Muhambwe, Kigoma, anazungumzia masuala mbalimbali na kushauri kuhusu mwelekeo wa Taifa…endelea.
Raia Mwema: Kwa faida ya wasomaji wasiokufahamu kwa undani, tueleze kwa muhtasari historia yako.
Ntagazwa: Naitwa Arcado Dennis Ntagazwa. Nilizaliwa Desemba 4, 1946. Ni mtu mzima kimsingi, sidhani kama ni kijana, isipokuwa ukienda kwa Wakorea msemo wao kwamba ujana huanzia miaka 60 basi kwa Wakorea nina miaka yangu minne ya ujana kwa maana hiyo.
Lakini pia tunao msemo katika lugha yetu ya Kiha walituachia wazee wetu wanasema; asazugomba, kusaza ni kuzeeka, kugomba ni kutaka.
Kwamba ukitaka kuzeeka utazeeka lakini kama hutaki hautazeeka, hiyo ndiyo maana ya wazee wetu na nadhani walitaka kutuambia uzee dawa.
Kwa upande wa elimu namshukuru Mungu pamoja na kwamba nimekuwa kwa kudura za Mwenyezi-Mungu kwa sababu marehemu baba yangu Ntagazwa alifariki wakati mimi natambaa.
Na mama kaniacha nikiwa na miaka kati ya mitano au sita kwa hiyo Mungu aliwapenda zaidi wazazi wangu lakini aliwapa watu wenye mapenzi mema moyo wa kumlea huyu kichanga wa Ntagazwa na mkewe walionitangulia mbele ya haki.
Raia Mwema: Pengine kabla hujaendelea, kwa hiyo ulilelewa na mmoja wanafamilia kutoka kwa mmoja wa wazazi wako?
Ntagazwa: Sisi katika mila na desturi zetu tulikuwa na kaka yetu mkubwa katika maana pana kwa sababu mama yake na huyo kaka yetu aliolewa na marehemu baba.
Sasa yeye (kaka) alikuwa ni mtu mzima ana wake zaidi ya mmoja na kwa mila zetu sisi mke mkubwa ndiye anapewa jukumu la kulea kama ilivyotokea kwangu mimi wazazi wangu wote walipofariki na kaka mkubwa akachukua jukumu la kunilea.
Sasa Mwenyezi Mungu wa ajabu na ndiyo maana nasema matendo yake yanatisha kama nini. Mke mkubwa huyo wa marehemu kaka yetu aliyechukua jukumu la kunilea alikuwa ni mama mwema sana kwa sababu alikuwa na wanawe wakubwa tu kama wa miaka 18 na kuendelea.
Kwa hiyo mimi nilikuwa kama kitoto chake kichanga, alinipenda sana mama yule Mwenyezi Mungu amrehemu. Lakini naye nilipofika darasa la pili mama yule naye Mwenyezi-Mungu akamwita.
Kwa hiyo ukawa utaratibu ule ule mke mkubwa zaidi kati ya wale wake zake kaka waliobaki akapewa jukumu la kunilea, yeye alikuwa na wanawe karibu wa rika langu.
Kwa kweli hapo sasa niliipata joto ya jiwe wanasema, kwa sababu kwa kweli moja ya vitu ambavyo vilifanya nikaanza kwenda shule ya bweni kuanzia darasa la tatu hadi namaliza chuo kikuu ni kwa sababu mama yule kwa kuwa alikuwa na watoto wa rika langu nilikuwa nikienda shule kwa kawaida darasa la pili, sisi mwaka 1956 tulikuwa tunaanza masomo kipindi cha mchana baada ya saa sita.
Sasa nikienda shule atawapikia wanawe watakula chakula cha mchana, mimi nikitoka shule naambiwa nikachunge mbuzi, nitakapotoka kuchunga mbuzi tayari wanakuwa wamekwishakula chakula cha jioni.
Kwa hiyo yalikuwa maisha magumu kwa maana hiyo lakini namshukuru Mungu alinipa akili sana kwa wakati huo.
Raia Mwema: Turejee katika elimu sasa.
Ntagazwa: Nilisoma shule ya Msingi inaitwa Kizazi Primary School mwaka 1955 na 1956, mwaka 1956 mwishoni nikaenda kusoma Shule ya Msingi Kabanga wilayani Kasulu darasa la tatu na la nne zote za bweni.
Sasa hiyo ilinipa wanafamilia na wanajamii pale kidogo kwa sababu nilikuwa sipo muda mrefu nyumbani, ninapokuja likizo wanakuwa na hamu ya kuniona lakini ukishapita mwezi tena yanarudi yale yale (kukosa chakula) lakini ilikuwa ndiyo nakaribia kurudi shule baada ya likizo.
Na nilisoma kwa taabu kwa sababu sikuwa na mtu wa kunilipia ada kwa sababu mimi kaka yangu mkubwa aliishia darasa la nne na kwa kweli alikuwa anahangaika sana kutafuta fedha nisome.
Mara alikuwa anakwenda kufanya vibarua Uganda kwenye mashamba ya miwa mara atakwenda kufanya vibarua manamba kwenye mashamba ya mikonge kule Tanga kwa hiyo nilikuwa kama ninavyosema Mwenyezi Mungu alikuwa ananipenda. Kulikuwa na baadhi ya watu wenye nia njema walioamua kuchukua mahala pa wazazi wangu waliokuwa marehemu kwa wakati ule.
Kwa hiyo, baada ya masomo pale Kabanga, nilikwenda darasa la tano na la sita Ujiji-Kigoma, hii ni seminari ndogo, ambako nilisoma darasa la tano na la sita mwaka 1959 na 1960 na baada ya hapo niliendelea na seminari darasa la saba hadi la 12 Seminari ya Mtakatifu Joseph Kaengesa Sumbawanga.
Kwa hiyo Kabanga-Ujiji-Kaengesa hadi darasa la 12 sikuendelea na seminari baada ya hapo nilikuja darasa la 13 na 14 Saint Francis College ilivyokuwa inaitwa siku hizi ni Pugu Sekondari.
Baada ya hapo nilikwenda Jeshi la Kujenga Taifa Mkuyu-Handeni, Tanga na Oljoro Arusha kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Makerere kwa ajili ya mafunzo ya shahada ya sheria.
Raia Mwema: Baada ya safari ya kielimu, kwa faida ya wasomaji turejee safari yako ya kikazi baada ya elimu ya Makerere.
Ntagazwa: Baada ya kumaliza Chuo Kikuu nilibahatika kwa kweli kufanya kazi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu nilikuwa Idara ya Usalama wa Taifa.
Nashukuru Mungu nilifanya kazi na kiongozi wa Idara hiyo mwadilifu na makini sana (sasa marehemu) Emilio Charles Mzena.
Raia Mwema: Kumbukumbu gani au kuna jambo gani kubwa kutoka kwa marehemu Mzena linalokufanya uamini moja kwa moja alikuwa mwadilifu.
Ntagazwa: Ngoja nikwambie. Unajua Idara ya Usalama wa Taifa ndiyo roho ya nchi na zile taarifa ambazo chombo kile kinakusanya na kuzichambua na kuziwasilisha kwa viongozi wakuu wa nchi ili wafanye uamuzi ndizo zinafanya nchi iheshimike na kiongozi ajue nchi inaelekea wapi na huyu baba alifanya kazi hiyo vizuri sana.
Nakumbuka wakati mmoja alikuwa ananiambia na aliniambia ilikuwa inafika mahali wakati ule Rais ni Mwalimu Nyerere.
Anamwambia ndugu Rais…wakati ule ilikuwa ndugu si mheshimiwa. Kwa hiyo anamwambia ndugu Rais hawa mawaziri wako wanaokwenda kunywa pombe kwa vilabu wanaropoka siri za serikali na wahudumu wa baa na kitu kama hicho mimi utakuta nimekwishawafungia kwenye nyumba za idara za usalama utakuja kuwachukua huko.
Kama wanataka kunywa pombe zao na mambo mengine wakanywe pale Leaders Club (eneo mahususi kwa viongozi Kinondoni-Dar es Salaam, kwa wakati huo) pale watakuwa wanaongea wao kwa wao.
Hiyo inalinda heshima ya serikali na vyombo vyake, siri za serikali hazitavuja kama leo hii. Mimi nadhani gazeti mojawapo nadhani liliwahi kuandika kwamba waziri mmoja wa awamu hii anakwenda kunywa pombe anaropoka na kusema ngojeni nitakapokuwa Waziri Mkuu mtanikoma.
Aah, sasa kwani uwaziri ni kukomoana au kutumikia watu?
Raia Mwema: Kwa hiyo kigezo hicho ndicho dhahiri kinakufanya umkumbuke Elimio kama mwadilifu na mwenye msimamo kikazi asiyebabaishwa na matakwa binafsi ya viongozi.
Ntagazwa: Naam, ni kigezo ambacho nilimwona yule Emilio Mzena kama kiongozi mwadilifu sana.
Raia Mwema: Lakini wanasema wakati mwingine Idara ya Usalama wa Taifa ubora wake unategemea vile vile yule aliyepo juu kwa maana ya Rais…kwamba anafanyia kazi taarifa za idara hiyo au anazipuuza na kufanya anayotaka na hatimaye kuvuruga baadhi ya matarajio ya nchi.
Huoni kwamba wakati ule Mwalimu Nyerere alikuwa mtiifu kwa idara hii na ndiyo maana kulikuwa na udhibiti mkubwa wa maadili?
Ntagazwa: Ni kweli kwamba na Mkuu wa nchi naye alikuwa ni mwadilifu lakini pia zile taarifa za chombo alikuwa anazisoma kwa umakini mkubwa na nina uhakika pia alikuwa na washauri makini sana na waadilifu pale alipokuwa na shaka.
Alipokuwa na shaka kuhusu masuala fulani aliomba ushauri bila hata kuwaonyesha taarifa hizo lakini ni kitu anasema nina suala hili sasa ningependa ushauri wenu.
Mwalimu Nyerere alikuwa na kawaida anamwambia Katibu wake, Joseph Butiku…Joseph hivi mzee Sengerema mnajua yuko wapi…mimi ningependa siku moja ninywe chai naye…ni agizo atatafutwa yuko wapi, kama yuko Mwanza ataulizwa mkuu wa mkoa ataambiwa mkuu wa mkoa mtafute mzee nadhani alikuwa mkoani Tabora yule Mzee Sengerema.
Mtafute huyu mzee Mwalimu Mwalimu anataka kuonana na wewe. Watafanya utaratibu watamsafirisha na watamwambia si kwamba kuna jambo lolote la kutisha au la ajabu usije ukafa kihoro…watamwambia unajua ninyi na Mwalimu ni watu wa rika moja, pengine kwa sababu Mwalimu ni mpenzi wa bao anapenda mcheze wote akafunge.
Kwa hiyo atakuja na akija yule mzee Mwalimu kama anakitu ni kweli watakunywa chai au watakula chakula lakini kwenye maongezi kama kuna kitu atamwambia hivi Mzee Sengerema katika hali ya namna hii mlikuwa mnafanyaje…alikuwa anatafuta ushauri kwa namna ya kawaida kabisa lakini anajua anatafuta ushauri kwa mtu ambaye atampa ushauri wa kweli na wa hali halisi katika hali aliyomweleza.
Nadhani viongozi wengi wanafanya hivyo, najua, ni imani yangu, lakini kama hawafanyi hivi ni shauri yao wenyewe.
Raia Mwema: Lakini wanasema kwa hali ilivyo sasa Idara hii ya Usalama uliyowahi kuifanyia kazi wakati mwingine inatumika kuandaa taarifa za majungu ili kuwakomoa watu fulani fulani?
Ntagazwa: Wala sio uongo. Unakumbuka wakati mmoja baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995 iliendeshwa kesi Mahakama Kuu kwamba Ntagazwa si raia.
Kipindi hicho Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ndiye alikuwa kiongozi wetu. Kwa bahati nzuri kipindi hicho mpaka leo ninao rafiki zangu kwenye Idara ya Usalama wa Taifa.
Kwa sababu nasema ni bahati kufanya kazi pale, ukichanganya na kusoma seminari na kufanya kazi pale maisha yakikuchachia kosa ni lako, huna wa kumlaumu ni wewe wa kujilaumu.
Maadili ya kiroho umefunzwa, utendaji kazi serikalini hata kabla hujaingia serikalini umekwishaufahamu. Sasa katika kesi ile, nakumbuka nilisingiziwa kwamba marehemu mama yangu alionekana akitokea Burundi kanibeba mgongoni.
Lakini kesi ile ilikuwa ya kutunga na yuko mama yetu mkubwa hata majuzi wakati wa tarehe mosi mwezi huu (Agosti) nilibahatika kumwona. Yule mama ana miaka zaidi ya 120 sasa hivi, bahati mbaya haoni lakini anatembea na anasikia na kuelewa nani anayezungumza naye…yuko kijijini.
Wakati wa kesi ile aliniambia wewe hivi mwanangu wanaosema marehemu mdogo wangu walimwona akiwa anatoka Burundi amekubeba wewe mgongoni mbona hawakuja kuniuliza?
Siku unazaliwa wewe nilikwenda pale kwenye kitongoji alichokuwa ameolewa mama yako, nimemkuta marehemu baba yako anahaha, hapakaliki kwa sababu mdogo wangu alikuwa katika uchungu wa kukuzaa wewe.
Nilipotokea akasema namshukuru Mungu ndiye amekuleta kamhudumie mdogo wako yuko katika uchungu wa kujifungua. Mimi ndiye nimekukata kitovu, kitongoji kile pale cha Kasana, kijiji cha Nyarugusu, wilayani Kibondo, nani anasema wewe umezaliwa Burundi?
Nikamwambia mama yangu wale walikuwa kwenye mradi wa fedha na ni kweli kabisa zilikuwa zimetumika kama Sh milioni 200 kwa kazi hiyo ya kusema mimi si raia.
Raia Mwema: Kwa nini unaamini walikusingizia, unadhani walikuwa wanalenga nini?
Ntagazwa: Walichokuwa wanalenga baadaye niliambiwa. Unajua nimekwambia nilikuwa nimekua kwa sababu Mwenyezi Mungu alikuwa ananipenda, amewapa watu wema kunilea kama mtoto wao, kwa hiyo mimi napenda watu.
Na kwa sababu napenda watu, sipendi kuona watu wakionewa. Sasa katika lile pori la Moyowozi, mimi nilikuwa nasema wananchi wanaokaa vijiji vya jirani na pori lile wafaidike na shughuli zinazofanyika kule na hiyo ndiyo sera ya serikali kwamba rasilimali za Taifa zitumike kupambana na maradhi na ujinga.
Kwa hiyo mimi nikatetea watu wanufaike, sasa, baadaye na kwa sababu wakati huo nilikwishakuwa Waziri wa Ardhi, Maliasili na Utalii najua nini kinaendelea. Unapewa kibali cha kwenda kuwinda wanyama kadhaa, mwindaji au mwenye kitalu kile anawawindisha wale wawindaji aliowaleta zaidi ya idadi ya wanyama walioorodheshwa na kwa maana hiyo huo ni wizi wa rasilimali zetu.
Na mwananchi hapati kile kiasi kinachotakiwa. Sasa mimi kwa kuamua kulizungumzia hili ikaonekana huyu bwana namna ya kumnyamazisha kwa sababu anasema bungeni, ngoja tuseme si raia ili atoke bungeni. Sisi tuendelee kufanya mambo yetu ndiyo ilikuwa jambo hili.
Raia Mwema: Aliyekuwa nyuma ya mpango huo bila shaka alikuwa mtu mzito. Je, alikuwa mwanasiasa au mfanyabiashara?
Ntagazwa: Wakati huo alikuwa mfanyabiashara, siku hizi ni mfanyabiashara na mwanasiasa mkubwa tu nafikiri ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. Sitaki kumtaja mimi ni mwanasheria.
Lakini si hayo tu. Unajua baada ya ile kesi Kigoma kuamuliwa kuwa Ntagazwa si raia na kuondolewa kwenye ubunge nilifanya mchakato wa kupinga, kukata rufaa, nikaenda Mahakama ya Rufaa ikasema kesi ile ilikwenda kienyeji mno kwa hiyo tunarudi katika hali ya kabla ya uamuzi wa Mahakama Kuu iliyoketi Kigoma kwa hiyo nikarudi kuwa mbunge.
Niliporudi bungeni nikachaguliwa kwenye Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria na baadaye pia nilichaguliwa na wabunge wenzangu kuwa Mwenyekiti wa Bunge, naendesha vikao vya Bunge, siku moja sasa ndiyo nakuja kwenye lile suala la taarifa za ovyo za chombo hiki (Idara ya Usalama wa Taifa).
Siku moja (mwaka 1998, baada ya rufaa ya kesi kukamilika mwaka 1997) wakati naendesha Bunge mheshimiwa Waziri Mkuu Sumaye (Frederick) kaniletea kiji-note…mheshimiwa Ntagazwa baada ya kuahirisha Bunge naomba tuonane nyumbani. Sasa kwa sababu unaendesha Bunge inabidi uwe makini sana pale kwenye kiti, nilichokifanya baada ya ile note ni kumtazama Waziri Mkuu alipokuwa ameketi na kuinamisha kichwa kuonyesha kwamba nimepokea ujumbe wake.
Lakini naona Mheshimiwa Waziri Mkuu haikutosha ile, akaniletea kwa kutumia wale wahudumu wa Bunge maandishi na nilipoletewa pale mezani nikafungua….ni taarifa ya usalama, uraia wa mheshimiwa Ntagazwa.
Niliposoma hivi kichwa cha habari, nilimtazama kwanza Waziri Mkuu aone kwamba nimeipokea, nilipomtazama hivi nikaiweka pembeni (ile taarifa) literary kwa Kiingereza sikuitilia maanani taarifa ile kwa nini kwa sababu wakati ule nadhani ilikuwa kwenye Bunge la mwezi wa 10 au 11 hivi, taarifa ile ni ya uongo iliandikwa na mtu mmoja ambaye nadhani alikuwa bado haamini ushindi wangu kwenye Mahakama ya Rufani hapana kwa sababu ya fedha zilizotumika kuniondoa bungeni.
Sasa taarifa ile mimi nilikuwa nayo tangu mwezi wa nne na ndiyo maana nilipoletewa kwenye mwezi 11 (bungeni na Waziri Mkuu) niliona si lolote si chochote, lakini pia marafiki zangu wakati ule walikuwa wamesema bwana ee sisi tumeambiwa hili suala kwamba Ntagazwa si raia halitakiwi kusikika serikalini si kweli walikwishagundua kuwa ilikuwa hadithi ya kutunga.
Ndiyo nakuonyesha sasa kwamba Idara ile nayo inatumika lakini si hilo tu, Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa wakati ule alikuwa bwana Apson aliniambia bila uficho…Idara ilikuwa wakati wenu (Ntagazwa) na Mzee Mzena.
Raia Mwema: Alidiriki kusema hivyo bila kujali ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara?
Ntagazwa: Ndiyo, aliniambia. Sasa hivi bwana ukituletea taarifa ukiwapa vijana wetu ukasema nao vizuri wataandika taarifa ya ovyo dhidi yako na itapelekwa serikalini.
Sasa nikasema balaa gani hii kwa sababu kile chombo ndiyo roho ya nchi. Ndiyo roho ya serikali, na unasikia siku hizi nani kapeleka hela wapi utadhani ni sadakalawe kama alivyowahi kutueleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, pata pataye.
Kwa hiyo kuna vitu vinaogofya kusema kweli, lakini nadhani wanajitahidi lakini bado wamsaidie sana kiongozi wetu (Rais).
Raia Mwema: Kwa uzoefu wako, unadhani nini hasa kimesababisha kupwaya kwa hii Idara ya Usalama wa Taifa kiasi hicho kwa mujibu wa maelezo yako? Nini kimetokea..
Ntagazwa: Nadhani, unajua Baba wa Taifa, nadhani alikuwa anaongozwa na Mwenyezi Mungu. Unajua aliwahi kutuambia hivyo hivyo, alisema ukikuta dimbwi la maji ya mvua, chukua glass ya maji chota kutoka kwenye hilo dimbwi, maji yale hayatakuwa na tofauti na maji yaliyobaki kwenye dimbwi.
Hawa maofisa wa usalama wa Taifa si wanatoka kwenye jamii yetu. Jamii ya Watanzania leo ikoje? Huwezi ukasema ni jamii ambayo tuna uchu wa kuzingatia maadili, ukweli, uadilifu na mema yale unayoweza kusema hapa yapo maadili ya kumpeleka mtu kwa Mwenyezi-Mungu muumba wake. Sidhani kama unaiona hiyo wazi wazi.
Raia Mwema: Katika mazingira hayo, tufanye nini kama Taifa?
Ntagazwa: Katika mazingira haya ambayo maadili yameporomoka ni kama vile utu hauthaminiwi kama ule msemo wa hapendwi mtu inapendwa pochi. Hapendwi mtu kinachopendwa ni fedha. Kinachotakiwa mimi kwa maoni yangu kwa kweli si mapinduzi lakini kuna kitu wanaita moral rearmament sasa Kiswahili chake kwamba katika maadili haya ya dunia na ahera, kuwe na kitu kama mwamko mpya ili ile jamii ithamini utu wa kila mtu na katika kuthamini utu wa kila mtu pia iainishwe kwamba sisi binadamu ni viumbe wa Mwenyezi Mungu.
Raia Mwema: Lakini nani atakayefanya hayo yote, wakati karibu wote tunaonekana tumepotoka kimaadili, tukiongozwa na viongozi.
Ntagazwa: Itabidi wajitokeze wachache wa kujitoa si mhanga lakini kujitoa sadaka kwa sababu tunajua wewe na mimi tukichunguza dhamiri zetu tunajua kwamba tumepotoka.
Sasa tunahitaji watakaokuwa majasiri wa kusema upotofu huu si sawa na waliseme bila haya, bila kuchoka. Ni lazima tuanze mahali.
Raia Mwema: Wapi pa kuanzia kusema hayo kutoka kwa vinywa vya majasiri unaozungumzia. Je, ni kutoka kwenye dini, siasa, taasisi za elimu au wapi?
Ntagazwa: Mimi nadhani tuanzie kwenye taasisi za elimu kwa sababu huko ndiko tunajenga Taifa la leo, kesho na keshokutwa. Najua utaniuliza huko kwenye taasisi za elimu walimu je?
Walimu si hawa wa vodafasta, bado tunao waalimu wastaafu ambao walitufundisha sisi, bado tunao. Lakini lazima tuanze mahali, hatuwezi kuendelea hivi halafu tukajidanganya eti tuko salama kitaifa.
Raia Mwema: Tuje kwenye siasa ingawa tumegusia kidogo. Umewahi kuwa mbunge, waziri na kuwahi kufanya kazi na watu wenye uchungu na nchi ambao baadhi wengine sasa hivi wamegeuka mafisadi, wakiwamo waliowahi kuwa karibu na Mwalimu Nyerere. Unazungumziaje ‘kizunguzungu’ hiki.
Ntagazwa: Kwanza, namshukuru Mungu nimebahatika kufanya kazi chini ya uongozi wa mwasisi wa Taifa letu, Mwalimu Nyerere na kweli kipindi kile nilikuwa mchanga mwaka 1983 nina kama miaka 10 tu nimetoka Chuo Kikuu akaniteua kuwa Naibu Waziri wa Fedha, Waziri akiwa Cleopa Msuya.
Nimefanya kazi pale kusema kweli nashukuru ilikuwa ni shule kubwa ni mahali ambapo nimejifunza mengi.
Moja ya vitu ninavyokumbuka pale wakati ule kuingiza kompyuta nchini ilikuwa lazima vikao vifanyike. Watalaamu kama ninyi ilibidi mkae vikao kwanza.
Mnakaa kwanza wataalamu mnasema huyu anaingiza kompyuta nchini kwa nini na anastahili au hastahili. Mkishamaliza ninyi wataalamu taarifa kikao lazima zije katika dawati la Naibu Waziri atie saini kwamba anaruhusiwa kama mlivyopendekeza wataalamu.
Raia Mwema: Huo ni mchakato unaohusu kuingiza kompyuta za wizara?
Ntagazwa: Hapana ni za wataalamu wa nje waliokuwa wamekuja kufanya kazi za Serikali nchini. Ilikuwa wataalamu wa nje hawaruhusu kuingia na kompyuta mpaka kamati zikae na kujadili.
Sasa baada ya kufanya kazi na Mwalimu, nilibahatika pia kufanya kazi na Mzee Ali Hassan Mwinyi, ni kiongozi ambaye alijitahidi kufanya kazi vizuri.
Unajua nasema kwenye siasa ukali pia unatakiwa lakini usiwe mkali kama nyati aliyejeruhiwa, uwe mkali katika kusimamia misingi hasa ya kutekeleza sera, sheria, kanuni na taratibu, mtu akikiuka mnapambana.
Nilikuwa nasema hivi nilipokuwa serikalini, kuna makosa ya aina mbili. Kuna makosa ya makusudi, hayo hayana maelezo lakini kuna makosa ya kibinadamu kwamba unatarajia katika uamuzi huu tuliofanya matokeo yatakuwa A na uamuzi ule ummeufikia baada ya kuangalia maeneo yote, wanaita scenarios zote na mkakubaliana kwamba tunaamua A na tunarajia matokeo yatakuwa B.
Inakuja kutokea matokeo sio B wala C pengine yanakuwa D lakini kwa sababu mlikwenda kwa utaratibu unaojulikana ambao yeyote angefanya uamuzi kama mlioufanya maamuzi yake yanamaelezo yanayoweza kueleweka.
Lakini makosa ya makusudi unaamua kufanya uamuzi nje ya sheria, kanuni na utaratibu. Utamweleza nani kwamba kosa hili hukulifanya kwa makusudi na kwa malengo mahususi unayoyajua wewe. Haya ndiyo makosa ya makusudi.
Sasa kuna viongozi wengine ni wapole na waadilifu mpaka ukasema pengine siasa si eneo lao kwa Kiingereza ukasema it’s not their way of calling.
Siku moja atanisamehe Makamu wa Rais na mgombea urais wa Zanzibar nimewahi kufanya naye kazi kwa miaka mitano nikiwa Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira.
Nakumbuka ataniwia radhi lakini si vibaya kusema, nilimwambia mheshimiwa makamu (wa rais) mi nadhani kati ya watakatifu waliopo hapa duniani wewe ni mmojawao.
Ndiyo, baba yule ni mwadilifu, ni mtaratibu hutosikia anapayuka hata kidogo, tunao watu wa namna hiyo. Ni tunu kutoka kwa Mwenyezi Mungu mnapopata viongozi wa namna hiyo.
Raia Mwema: Lakini huo uadilifu na upole tafsiri yake ni nini kwenye masuala ya uongozi, na hasa uongozi tunaotarajia utoe tija kitaifa.
Ntagazwa: Unajua kitu kimoja kizuri, ukiwa na kiongozi mwadilifu, mpole…mtakatifu kama nilivyosema hivi utakapofanya makosa ya makusudi utathubutu kumtazama hata machoni? Hali yake hiyo ya uadilifu…tuseme kama hali ya ukamilifu hivi utathubutu kufanya mambo ya ovyo ukiwa chini ya uongozi wake na ukamtazama usoni…si rahisi kwa sababu uso umeumbwa na haya?
Wanasema ukitaka kujua kama mtu anasema uongo wewe mtazame machoni…ana kwa ana…sasa wewe una kiongozi mwadilifu pengine mtakatifu hivi…mkamilifu, wewe unafanya madudu yako, wanaita mchoro, unafukuzia rushwa na uchafu mwingine katika eneo analoongoza utathubutu kufanya hivi?
Kwa hiyo ule uadilifu wake unafanya na wale walioko chini yake watimize wajibu kama inavyotakiwa na kwa manufaa ya jamii.
Raia Mwema: Hebu sasa jitathmini mwenyewe. Kwa kukaa kwako madarakani, ukiwa waziri au hata Idara ya Usalama wa Taifa. Jambo gani unajivunia?
Ntagazwa: Yapo mengi lakini labda sijui nichukulie wakati ule ulipotolewa uamuzi wa watumishi wa Serikali kuuziwa nyumba. Nilipoteuliwa kuwa waziri baada ya uchaguzi wa mwaka 2000, niliamua kukaa kwenye nyumba yangu, Kimara Temboni.
Niliamua kukaa nyumbani kwangu kwa sababu moja, nyumba ile nimeijenga kwa shida na imenichukua muda sana. Nakumbuka marehemu mke wangu alisema Mungu akituwezesha kujenga nyumba hii si wanaweza kusema tumeiba.
Nikamwambia mwalimu (mke alikuwa mwalimu) atakayesema tumeiba tunaweza kukataa lakini pia shahidi mkuu ni Mwenyezi Mungu na kama ningekuwa mwizi sidhani kama ingenichukua miaka 18 kujenga nyumba moja.
Namshukuru Mungu amenipa uhai mpaka nikakamilisha, nilianza kufyatua matofali mwaka 1986 nikawa najenga taratibu mpaka fremu za madirisha nilizoweka mpaka kumaliza kuta zilibadilika rangi na nilikuja kumalizia kwa mfano kuweka tarazo ni wakati namwoza binti yangu wa kwanza, Chimpaye anasoma Marekani si kwa gharama za serikali licha ya kuwa serikalini.
Nimeanza kufyatua matofali 1986 nilipofanya hesabu nikaona ni miaka 18 mpaka nyumba inakamilika. Ni nyumba ya ukubwa wa vyumba vitano, vyenye kujitegemea kila chumba.
Kuna pia chumba kwa ajali ya kusali, nilifikiria siku nitakapokuwa mzee pengine sitaweza kwenda kanisani kwa hiyo naweza kumwita padre pale nikasali.
Kwa sasa chumba hicho nakitumia kama ofisi. Kwa hiyo niliamua kukaa kwenye nyumba yangu kwa sababu hiyo sasa ilipoamuliwa watumishi na viongozi wa Serikali kuuziwa nyumba mimi sikuwa nakaa nyumba ya Serikali.
Baadaye nilitafutiwa nyumba ya Serikali, nikaambiwa kuna nyumba hapa, nikaenda nikaoina nyumba yenyewe ilikuwa kwenye bonde hivi, nilichofanya ni kwenda kulipia ile offer, nadhani ilikuwa ni Sh 1,500 hivi kuchukua zile fomu baadaye nikaambiwa nahitajika kulipa Sh zaidi ya milioni 30, nikasema yarabi nitazitoa wapi mimi.
Kwa hiyo nadhani kati ya mawaziri waliokuwa wakiitwa askari wa miavuli ni Waziri Ntagazwa ambaye ni mjinga wa kutupa ambaye hakupata nyumba kwa utaratibu huo na namshukuru Mungu maana pengine ingenisumbua kwenye dhamiri yangu kwamba hivi kweli ingawa ulikuwa ni uamuzi rasmi serikalini lakini ulikuwa wa haki bin haki?
Hilo ni moja, lakini la pili, siku moja nadhani ilikuwa mwaka 2007 nilikutana na mtu mmoja akaniambia unanikumbuka? Akaniambia mimi nilikuwa pale Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati ukiwa waziri pale anasema mheshimiwa leo hii mimi najiuliza; hivi ungetaka kuwa tajiri wa kutupa nani angekuzuia?
Nikamuuliza, tajiri wa kutupa kwa kufanyaje? Akasema ukiwa Waziri wa Ardhi, Maliasili na Utalii…viwanja viko chini yako, magogo msituni, vitalu vya uwindaji viko chini yako, uvuvi chini yako.
Nikamwambia ningeweza kuwa tajiri wa kutupa lakini dhamiri yangu ningeipeleka wapi? Akasema hiyo dhamiri yako ingekuwa shauri yako wewe.
Kwa hiyo unaona ni vitu ambavyo unakubali kutumikia na sio kujinufaisha lakini watu wanakushangaa. Lakini nina uhakika aliyeniumba (Mungu) hanishangai ndicho anachotarajia nikifanye.
Raia Mwema: Ni jambo gani unalojutia ulilowahi kufanya au kushuhudia katika kipindi chako ukiwa kiongozi kitaifa.
Ntagazwa: Kuna wakati mmoja (enzi za Rais Ali Hassan Mwinyi) alikuja mzee mmoja simkumbuki jina, nikiwa Waziri wa Ardhi, Maliasili na Utalii kulikuwa kumetolewa viwanja eneo fulani na mzee huyo alikuwa amepata kiwanja kihalali hapa Dar es Salaam.
Nakumbuka kiwanja chake kilikuwa namba 163 sasa inaelekea kiwanja namba 161 au 162 aliweka vifaa vya ujenzi asiweze kufika kwenye kiwanja chake.
Sasa unajua katika hali hiyo yanapoanza masuala ya ujenzi kiwanja chake kingeweza kumezwa katika utaratibu wa kupora.
Alikuja kutulalamikia wizarani, niliwaita wataalamu nikawaambia jamani huyu mzee ni sawa na baba yetu kumhangaisha si jambo jema hata kidogo kwa nini tusimtafutie kiwanja cha ukubwa ule ule katika block ile ile.
Kikatafutwa kiwanja akapata akaandikiwa ofa akalipia tukawa tumemaliza tatizo lake. Mheshimiwa Rais Ali Hassan Mwinyi alipoanzisha utaratibu wa kusikiliza kero za watu pale Lumumba (Ofisi za CCM-Dar es Salaam) huyu mzee alikwenda pale kulalamika kwamba mimi Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii hawakunisaidia chochote kuna mtu aliyepora kiwanja changu.
Sasa uzuri wakati ule Balozi Matern Lumbanga alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii ambaye baadaye alikuwa Katibu Mkuu Kiongozi.
Akiwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi baadaye waliondoa maliasili na utalii wakaipeleka kwingine. Kwa hiyo kwa sababu ndiyo ilikuwa wizara inayohusika na suala la mzee huyo Lumbanga akaitwa kutoa maelezo.
Sasa wakati huo Lumbanga, watu hawakujua na wengi hawajui lakini nimesoma naye darasa la 13 na 14 Pugu ni mtu mwenye msimamo na maadili.
Akamwambia mheshimiwa Rais naomba nikwambie kwa dhati mzee huyu hana shukurani. Huyu mzee alichokwambia kwamba kuna mtu ameingilia kiwanja chake na amekuja wizarani kulalamika ni kweli lakini alichokifanya Waziri Ntagazwa alituitisha wataalamu akasema jamani huyu mzee tusiendelee kumsumbua, tafuteni kiwanja cha ukubwa ule ule katika block ile ile ili kama thamani ya eneo isipungue, akapata kiwanja mpaka leo anacho. Kama anakulalamikia huyu hana shukurani. Hiyo ilinisononesha kidogo.
Raia Mwema: Tuingia kwenye siasa. Tueleze kumetokea nini CCM hadi mzoefu kama wewe ukimbie, wengine wanaweza kutafsiri kama umekimbia matatizo badala ya kuyakabili.
Ntagazwa: Nimechomoka kwa sababu ukiisoma Katiba ya CCM katika malengo yale kuhakikisha kwamba rasilimali za Taifa zinatumika kupambana na ujinga, maradhi na umasikini, nikihusisha na pori la hifadhi la Moyovozi linalopakana na Wilaya ya Kibondo na Wilaya ya Kakonko ambayo ni mpya na nadhani mpaka Bukombe huko yale yanayotokea hapana. Haiwezekani yakawa yanatokea na ukasema ni vyombo vilivyo katika Serikali ya CCM hapana.
Kwa nini nasema hivyo; mosi, unapopata taarifa serikalini kwa maana ya wilaya na mkoa na unapata taarifa hizo kwa wanafamilia kwamba zaidi ya watu 21 wameuawa katika pori hilo la hifadhi lazima mshituke. Si kitu cha kujivunia kwamba mmefanya siri, hilo moja.
Februari mwaka jana zilitolewa taarifa baadhi yetu tunaotoka mkoani Kigoma kwamba watu 21 au zaidi wameuawa katika Pori la Hifadhi la Moyovozi. Ni kweli wameingia katika eneo kinyume cha sheria lakini tuna utaratibu wa kisheria. Mtu akiingia kwenye eneo kama hilo anaitwa jangili na anatakiwa kupelekwa kwenye vyombo vya sheria si kuuawa.
Lakini hivi karibuni kitu ambacho kimefikia kunisononesha ni kwamba CCM hii ya leo, mimi nadhani kilichopo ni zile herufi CC na M, si CCM iliyorithi mazuri ya TANU pamoja na CCM ya wakati wa Mwalimu Nyerere.
Ameingia mwananchi katika Pori la Hifadhi la Moyovozi, bahati nzuri maofisa wa wanyamapori wamefanya kazi yao nzuri amekamatwa.
Lakini yule mwananchi amekatwa sikio na ofisa wanyamapori kapelekwa mahakamani kesi inaendeshwa na ni sahihi kabisa ameingia kwenye hifadhi kinyume cha sheria mimi sitetei hata kidogo uvunjifu wa sheria, kapelekwa mahakamani ambao ni utaratibu kabisa unaokubalika katika utawala bora.
Ofisa yule ametoa ushahidi wake kuiambia Mahakama amemkamata wapi na mambo mengine akamaliza, mshatakiwa akamuuliza maswali mawili ninayoyakumbuka.
Mshitakiwa alimuuliza; shahidi nakuuliza uliponikamata nilifanya vurugu yoyote akasema hapana kama ungefanya vurugu ningekushona risasi, akamuuliza sawa kwa nini ulinikata sikio akajibu nilikukata sikio ili niweze kukutambua kama utarudi tena porini.
Nimekwambia nilivyokuwa na nilivyolelewa na nilivyosoma, siamini kama majibu ya namna hii yanaweza kutoka kwa mtumishi wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi. Majibu ya namna hii yanaweza kutoka kwa muasi wa Lord’s Resistance Army kule Uganda.
Sasa ukiona mambo ya ovyo ovyo ya kiwango hicho yanafanyika na haya mengine tuliyoshuhudia kwenye mchakato wa kura za maoni wakiimba..tumechoka kuonewa …tunataka haki zetu! Chonde chonde hamko salama.
Amani inakwenda kutoweka. Tuombe Mungu tusifike huko, lakini nimekwambia hivi unafika mahali kila mmoja wetu anakiri kwamba si sawa. Wengi tu katika CCM nina uhakika wanayaona si sawa lakini watakapokaa kwenye vikao rasmi kwa sababu ni mfumo, sasa mfumo unatawala wewe na mimi tunapotoa kasoro moja au nyingine wala, yote weka chini ya busati mnaendelea kama vile hakuna kilichotokea, si sahihi tutauana…haifai, tumuombe Mungu tusifike huko.
Kwa hiyo ni sababu kubwa, nimeona hakuna tegemeo kwa sababu mfumo umekwishakujikita na mfumo huu popote duniani hakuna mfumo unaofanya kazi ya kujimaliza hata siku moja. Mifumo yote inafanya kazi ya kujifanya iwe endelevu.
Raia Mwema: Kwa nini uliamua kwenda CHADEMA badala ya vyama vingine tofauti na CCM.
Ntagazwa: Jibu ni jepesi sana. Nakumbuka kuna wakati nadhani alikuwa anazungumzia juu ya vyama mbalimbali vya siasa, Mwalimu Nyerere akasema ukisoma karibu Katiba za vyama vyote ni Chama Cha Demokrasia na Maendeleo ndiyo Katiba yake inashabihiana na Katiba ya TANU na ile CCM ya wakati wa Mwalimu.
Na ndiyo maana kwenye salamu ya CHADEMA tunasema CHADEMA wanaitika vema, CHADEMA tumaini jipya la Watanzania, tunajivunia nguvu ya umma.
Ni kweli binadamu lazima uishi kwa matumaini kama huna matumaini utajinyonga sasa hivi na katika utaratibu huu, demokrasia ya mfumo wa vyama vingi vya siasa lazima kuwa na chama unakiona ni mbadala ambacho kinaweza kuiondolea jamii mfumo huu wa sasa unaolea uovu.
Raia Mwema: Unakwenda kugombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Jimbo la Muhambwe, Kigoma. Katika kampeni wewe ndiye utakayekibeba CHADEMA au chama hicho ndicho kitakubeba kwa maana ya nguvu zako kisiasa kwa kulinganisha na mtandao wa CHADEMA huko.
Ntagazwa: Hapana. Unajua ukitaka kulinganisha CHADEMA na CCM, CCM wana mtandao mkubwa tu. Bahati mbaya wanauvuruga kwa kutokukemea maovu ambayo dhahiri yanaonekana na ni kwa sababu watu wetu wanakabiliwa na umasikini wa kipato na hali kwa maana ya weledi wa nini kinapaswa kufanyika na viongozi wetu kwao…viongozi wetu wajibu wao ni upi na haki yangu mimi raia ni nini na vile vile na mimi nina wajibu kwa jamii ili twende pamoja.
Huwezi kulinganisha mtandao wa CCM na chama kingine chochote cha siasa nchini na kwanza ukumbuke kuwa mpaka leo CCM ni chama dola.
Katika suala hili la kwenda kugombea Muhambwe, CHADEMA wana mchango mkubwa sana tutakavyokwenda kumshinda mgombea wa CCM.
Wanajua sifa zake, simjui kwa jina wala sitaki kutaja jina lake lakini moja ya sifa zake wanazopaswa kujua ni katika kura zile za ovyo ovyo za maoni…na mengineyo. Alipata alama nzuri tu kwenye chama, hilo wanalijua, kama hawalijui basi ni mfumo umefunika lakini si kwamba ukweli huo haupo.
Kwamba mgombea wao ametumia haki yake ya kikatiba kwenda mahakamani amekashifiwa na padre katika ibada lakini katika kesi ile kamchukua padre kamjumuisha mwalimu wa msikiti na waumini wengine inajulikana kesi ile imekwisha Mahakama Kuu lakini nadhani utaratibu wa rufani unaendelea siwezi kwenda zaidi.
Lakini nina hakika wakiondoka kwenye mfumo wanamjua mgombea wao na ni ukweli kwamba ahadi moja ya CCM inasema nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa manufaa ya wote, hii ni ahadi ya CCM na enzi zile wakati wetu ulikuwa unatoa ahadi kwa kiapo.
CCM katika Jimbo la Muhambwe katika karne ya 21 ya Sayansi na Teknolojia, wamemsimamisha mgombea ambaye hakumaliza hata elimu ya msingi ameishia darasa la sita, hiyo ni kweli. Sasa kama ni dharau kwa wapiga kura wa Muhambwe sijui.
Raia Mwema: Lakini hadi hapo hawajavunja sheria na Katiba ya Tanzania inataka mtu anayejua kusoma na kuandika, unasemaje kuhusu matakwa haya ya Katiba.
Ntagazwa: Ndiyo lakini unakwenda na hali halisi katika mazingira. Sheria imepitishwa na Bunge ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo ninayo imeandikwa Kiingereza, mbunge huyu mtarajiwa wa CCM Muhambwe ataisoma, ataielewa? Ataifafanua na kuitafsiri na kuisimamia?
Raia Mwema: Unakwenda kugombea Muhambwe, wapiga kura wa Muhambwe watarajie nini kama kura zitatosha?
Ntagazwa: Watu wa Muhambwe, kura zitatosha kwa sababu mwaka huu hakichaguliwi chama, anachaguliwa mgombea na hata wizi wa kura uliokuwa ukifanyika tumekwishagundua walikuwa wanafanyaje, tutaweka majeshi ya kulinda kura.
Raia Mwema: Umesema walikuwa wanaiba kura na sasa mtawadhibiti, kwa hiyo ulipokuwa CCM mlikuwa mkifanya hivyo vitendo?
Ntagazwa: Mimi nilikuwa sifanyi wizi kwa sababu kwanza nilikuwa siendi kugombea kwa kujiamulia binafsi. Nilikuwa naitwa, wazee wananiambia walishawahi kuniambia sikiliza mheshimiwa Ntagazwa wewe ni mtoto wetu hata kama una mvi.
Tunasema hivi kama kuna kitu tulichokukosea sisi wazee wa Muhambwe, usichukue fomu (ya kugombea ubunge). Lakini kwamba kuna kitu ulichotukosea wewe hapana, tunakuomba ukachukue fomu.
Mara zote nilizogombea imekuwa hivyo na mimi nimekuwa nikishinda si kwa mbinu za wizi au rushwa, hapana. Safari hii kwa nguvu ya umma salama yetu katika CHADEMA, wapiga kura wa Muhambwe tutashinda.
Kitu ambacho watarajie nimekwishawaambia mambo mawili. La kwanza, wameanza kulima tumbaku na mimi najua kama mwana-mazingira tumbaku ni adui wa mazingira na hasa misitu.
Nimewaambia hivi, kilimo cha tumbaku na hifadhi ya mazingira vinaweza kwenda pamoja. Wanaotaka hiyo tumbaku ni kampuni ya ATTT ya Marekani na wamesema hawajapata tumbaku yenye ubora popote duniani kama tumbaku ya Kibondo.
Sasa nimewaambia kwa kuwa hawa wanataka tumbaku, lazima kuwe na programu ya kilimo cha tumbaku itakayonufaisha wakulima, wanunuzi wa zao hilo na wakati huo huo kulinda hifadhi ya mazingira.
Raia Mwema: Una ushauri gani kwa wanasiasa wenzako, ndani ya kambi ya upinzani na katika CCM.
Ntagazwa: Sote tunatakiwa kuwa na nidhamu katika vyama vyetu lakini isiwe nidhamu inayotuondoa karibu na Mwenyezi Mungu. Siasa si jambo la mwisho bali ni nyezo ya kuturahisishia kwenda kwa Mwenyezi Mungu kwa kadiri tunavyotimiza wajibu wetu. Siasa ni fursa ya kutumikia waja wa Mwenyezi Mungu.
http://www.raiamwema.co.tz/news.php?d=2549
