Monday, August 30, 2010

Lipumba Amfagilia Dr. Slaa

Quote: Akizungumza wakati wa kutangaza majina ya wagombea wa nafasi ya ubunge na uwakilishi yaliyopitishwa na Baraza Kuu la Uongozi, Dar es Salaam jana, Profesa Lipumba alisema pamoja na umakini wa Dk. Slaa, lakini amechelewa kutangaza nia yake hiyo na kuwa yeye yuko tayari kupambana na wanaoitafuna nchi.

“Awali Slaa, (Freeman) Mbowe, Dk. (Sengodo) Mvungi, (Augustino) Mrema, wote waliweka bayana kuwa hawatagombea, na sisi kupitia mchakato wetu tukaamua kugombea tukijua kuwa kuna mambo mengi ambayo tunayadai bado hayajatekelezeka na watu wamechoka hususan vijijini ambako sisi ndio tutakwenda,” alisema Profesa Lipumba na kuongeza: “Slaa ana haki ya kufanya hivyo na Chadema kina haki kumsimamisha.

Slaa ni rafiki yangu, na ninajua kuwa ni mtu makini na aliyefanya mambo mengi mazuri hususan katika Bunge kwa kushirikiana na wabunge wa vyama vingine vya Upinzani, lakini amechelewa kutangaza nia yake.

Namtakia kila la heri. Ila mimi nitasimama kupambana na mapapa, sangara na nyangumi wa rushwa.”
Source: Habari Leo Kwakweli kauli hii imetoka mdomoni kwa mtu makini anayeelewa ni nini anafanya kwa maslahi ya taifa. Kauli ya Lipumba inaashiria kwamba endapo Dr. Slaa angetangaza nia mapema, basi yeye Lipumba angeweza kujitoa ili kumpisha Slaa. Natamani akina MS KN na Tumain waseme lolote kuhusu hili.

Dr Slaa kumaliza matatizo ya walimu na Polisi

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya chama cha Chadema dr. Wilbroad Slaa amesema endapo atashinda urais katika uchaguzi mkuu wa oktobar mwaka huu jambo la kwanza atakalolishughulikia litakuwa ni kuboresha mishaharana maslahi ya walimu,askari polisi na wafanyakazi wa kada mbalimbali nchini.

Dr. Slaa amesema hayo mjini Morogoro jana katika mkutano wa hadhara wa kuomba kudhaminiwa kuwania urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Chadema.

Amesema amekuwa akistaajabu kuona wabunge wakilipwa fedha nyingi wakati askari wanaowalinda wananchi na mali zao wakilipwa mishahara na maslahi duni licha ya kufanyakazi katika mazingira magumu


Aidha amesema endapo atafanikiwa kuingia Ikulu suala lingine atakalolipa kipaumbele cha kwanza ni suala la maslahi ya walimu ili waweze kufanyakazi yao vizuri na kuboresha taaluma nchini.

Naye mfuasi wa chama hicho mwanasheria mashughuli nchini bw. Mabere Marando amesema muda wa kampeni utakapofika ataueleza umma wa watanzania namna viongozi wa ccm walivyoshirikiana kwa maslahi yao binafsi kukwapua fedha katika akaunti ya madeni ya nje

Dr Akiwa Bungeni


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (kushoto ) na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, Dr. Wilbrod Slaa (katikati) baada ya kusoma hotuba yake ya Kuahirisha bunge

wosia wa baba

wosia wa baba waendelea

wosia wa baba


Dkt Wilboard Slaa Akizungumza na Omar Kwaangw'


Mbunge wa Jimbo la Karatu (CHADEMA) Dkt Wilboard Slaa akizungumza nje ya Ukumbi wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini(CCM) Omar Kwaangw' juzi jioni mara baad ya kikao cha 11 cha mkutano wa 18 unaoendelea mjini Dodoma kumalizika.Picha na mdau Tiganya Vincent-MAELEZO-Dodoma

DR SLAA na Mhe Masha

Mbunge wa Nyamagana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Lawrence Masha
(shoto) akiteta na Mbunge wa Karatu na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mh. Dr.Wilbroad Slaa, kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma