Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akitoa salamu za chama hicho kwa Familia ya Mwalimu Nyerere, wakati vongozi mbali mbali na wabunge wa chama hicho, walipomtembela Mama Maria Nyerere (katikati) nyumbani kwake Butiama jana. Kulia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilibrod Slaa


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, wakati viongozi mbalimbali wa chama hicho walipomtembelea Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Butiama hii leo.


Mbunge wa jimbo la Kawe, Halima Mdee (CHADEMA), akiweka shada la maua katika kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, wakati viongozi na baadhi ya wabunge wa chama hicho, walipomtembelea Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Butiama leo. (Picha na Joseph Senga)





Mama Maria Nyerere akiteta jambo na katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, wakati viongozi wa Chama hicho na baadhi ya wabunge, walipomtembelea nyumbani kwake Butiama